Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono taarifa za Kamati zote mbili. Nataka niseme mambo machache na jambo la kwanza ni suala la maji, ninaiomba Wizara ya Maji mchakato wa maji wa Ziwa Victoria na utekelezaji wake tunatarajia sana watu wa Mikoa ya Tabora na Singida utekelezaji wa mradi huu, tumeusubiri kwa muda mrefu ingawa kuna matumaini madogo, tunaomba, tulitarajia mwezi huu wa pili mkandarasi angekuwa site, tungeomba jambo hili litekelezwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kwenye maji fedha zinazoenda kwenye Mfuko wa Maji chanzo chake ni mafuta. Amesema Mheshimiwa Nsanzugwanko ni muhimu sana base ambayo Kamati ya Bunge inayosimamia section hii i-demand kutoka Serikali mahitaji halali ambayo yalitakiwa yaende kwenye mfuko ili siku nyingine wakija kwenye Bunge hapa watuambie matarajio yalikuwa ‘X’ kilichopatikana ni ‘Y’ ili Bunge liwe na picha halisi ya nini kinaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, narejea nilisema mwezi wa tisa nasema na leo; hakuna dhamira ya Serikali kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji. Nilitahadharishe Bunge kwamba tusiingizwe kwenye mkenge tukadhani hili ni tatizo la Mheshimiwa Tibeza, siyo tatizo la Mheshimiwa Tizeba tu wala siyo tatizo la Waziri wa Ardhi tu na wala siyo tatizo la Waziri wa Maliasili, hili ni tatizo linalotakiwa kuchukuliwa na Serikali collectively. Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maji, Wizara ya Mifugo na Wizara ya Ardhi waje kwenye Bunge la Bajeti watuletee mpango wa Serikali juu ya kumaliza mgogoro wa wakulima na wafugaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu na la mwisho ni hii dream tuliyonayo, dream hii imekuwepo toka Serikali ya Awamu ya Kwanza kujenga Taifa la kujitegemea la viwanda, Serikali ya Awamu ya Pili, Awamu ya Tatu, Awamu ya Nne na Serikali ya Awamu ya Tano. Ninachokiona makosa yale ya toka enzi za Mwalimu Nyerere yanafanyika leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kosa la kwanza tuna-focus kuwekeza kwenye viwanda ambavyo ukitazama objective yake ni import substitution industry, ni wrong. Lazima tufike mahali Serikali ielewe hakuna industrialization kama hatujaamua kuwekeza kwenye sekta ya kilimo. Hakuna industrialization kama Wizara ya Viwanda, Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati na Wizara ya Miundombinu hawatokuja collectively na kuwa na master plan ya kutujengea viwanda katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwijage atakuwa anakuja hapa anatuambia njoo nikupe kiwanda. Mimi nimempa eneo hekta 200 Nzega, mpaka leo nataka niwaruhusu wananchi walime hakuna hata hope. Nataka nitoe mfano mwingine, leo hii tumbaku ina tozo na ushuru almost 16 lakini ukizitazama pamoja na silent ziko 19, Mheshimiwa Tizeba anajua.
Mheshimiwa Rais wakati anaomba kura alisema ataondoa tozo kwa wakulima, leo Nzega mkulima wa Idudumo akilima mpunga anaanza kutozwa kuanzia anavyotoka njiani nyumbani kwake na mageti mpaka anafika mashineni kuuza gunia lake moja, tunaongeza umaskini kwa watu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, safari hii hatujaweka bajeti ya pembejeo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge, hasa wa Chama chetu cha Mapinduzi, tusiwe tayari ku-fall into the pressure ya Serikali. Tumepitisha bajeti ya ajabu sana ya Kilimo mwaka huu hapa sisi, ambayo haina fedha ya bwawa, Mheshimiwa Dkt. Tizeba Waziri wa Kilimo wala Wizara ya Maji hawana uwezo wa kutujengea mabwawa ya wafugaji, hana fedha za pembejeo, tunasema mawakala walipwe tutaambiwa tu bado wanachunguza, Mheshimiwa Dkt. Tizeba hana lugha nyingine, kaapa yule, lakini hakuna fedha za kuwalipa, this is the bitter truth…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)