Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kupata nafasi hii ili niweze kuchangia Mpango huu wa Miaka Mitano na Mpango huu wa mwaka mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na elimu; ukiangalia Mpango huu umejikita zaidi kwenye mambo ya viwanda ili kubadilisha uchumi wa Taifa letu na maisha ya wananchi wa Tanzania. Nilikuwa najaribu kupitia mpango wote kwenye suala la elimu sijaona kama tumewekeza vya kutosha kwenye suala la elimu. Ninapoongelea suala la elimu, elimu inayoendana na viwanda tumewekeza kwa kiasi gani, Mpango huu umetaja kiwango gani, kiasi gani cha pesa ambazo tumeziwekeza kwenye vocational training.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukichukulia kwa mfano Mkoa wa Mara, ndiyo Mkoa ambao umetoa Kiongozi mkubwa katika Taifa hili, ambaye ndiye amesababisha na ninyi mmekaa kwenye hivyo viti vya mbele hapo, Mwalimu Nyerere. Mkoa wa Mara hauna Chuo cha VETA hata kimoja, hauna Chuo Kikuu hata kimoja, Mkoa wa Mara watu wake ni maskini kweli, hakuna kiwanda cha kueleweka, Mkoa wa Mara hauna hospitali ya Wilaya, iko shida kweli kweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashindwa kuelewa vizuri kwamba nilivyokuwa nasikia Tanzania ya Magufuli itakuwa ni nchi ya viwanda nilitegemea nitaona humu fedha za kujenga viwanda, sijaona! Sasa sijui ni viwanda vya namna gani maana nilitegemea Mkoa wa Mara tutapata pale kiwanda, vijana wetu watapata ajira, kumbe hamna ni blah, blah tupu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, iko hivi mmesema elimu bure 20,000/= sekondari, lakini wanaojenga madarasa ni wazazi, hawa wananchi wetu maskini ndiyo wanajenga madarasa, ndiyo wanajenga shule, asilimia 90 ya shule zinaendeshwa na wazazi, wewe umesema umeondoa 20,000/=. Iko hivi, wewe chukua asilimia 90 jenga madarasa, peleka madawati, acha wazazi walipe hiyo 20,000/=, hapo tutakuelewa lakini kama wazazi ndiyo wajenge madarasa wapeleke madawati, msiwadanganye Watanzania Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natokea Serengeti, ni Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Jimbo ambalo kwa miaka mingi limeongozwa na CCM lakini hakuna hata kipisi kimoja cha lami, hata mita moja ya lami hakuna, hospitali ya Wilaya hakuna, Wilaya ya Serengeti kuna wengine hawajui iko Mkoa gani, iko Mkoa wa Mara! Nimeangalia hapa hata kwenye miundombinu ya barabara wanasema mikoa yote imeunganishwa na barabara ya lami, nikajiuliza hivi Mkoa wa Mara na Mkoa wa Arusha umeunganishwa na barabara ya lami, barabara aliyoiasisi Mwalimu Nyerere ya kupita Butiama kwenda Arusha mpaka leo, Mheshimiwa Magufuli alikuwa Waziri wa mambo ya barabara, hata mwaka jana hakuja kuomba kura Serengeti maana barabara haijapita pale, lakini walimpa kura nyingi kuliko Lowassa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, walimpa kura nyingi eeh! walimpa kura nyingi wanataka kumpima waone kwamba uaminifu walioufanya kwake je, yeye atakuwa mwaminifu kwao, asipokuwa mwaminifu 2020 hawampi, habari ndiyo hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokuwa nasema ukienda kiuhalisia kwenye vijiji vyetu, kuna upungufu wa madarasa na baada ya kusema elimu bure watoto wamefurika mashuleni, madarasa hakuna, madawati hakuna, sasa nawauliza CCM fedha za kujenga madarasa ziko wapi humu, kwenye Mpango wenu mbona hausemi, ziko wapi? Mheshimiwa Waziri unisaidie utakapokuja hapa uniambie hela za madarasa na madawati ziko wapi humu au ndiyo zile za Bunge bilioni sita zitatosha? (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda vijijini kwenye shule za msingi, ninakotoka Serengeti nimeenda Shule ya Msingi Gwikongo haina dawati hata moja, mimi nimeamua kama Mbunge niwe mfano nisaidie angalau tupate madawati machache kwenye shule ile, lakini wamekuweko Wabunge miaka na miaka, dawati hata moja hakuna, ni shule hiyo! Wilaya ambayo imeongozwa na CCM muda mrefu, dawati shule ya msingi hakuna, halafu mnasemaje mipango, mipango gani hii! Upungufu wa Walimu ukienda shule za msingi, kuna shule moja ina walimu wawili tu, tangu uhuru mpaka leo wapo wawili, halafu mnasema wanafunzi wanafaulu wanakwenda wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, CCM mnamsaidia shetani kazi nawaambia ninyi, maana mnatengeneza majambazi wengi, vibaka wengi, ambao baadaye watakuja kuwatesa ninyi wenyewe, maana ninyi ndiyo mtakuwa matajiri, watawaibia ninyi wenyewe. Unafikiri kama akimaliza darasa la saba, kamaliza form four hana ajira unafikiri atafanya kazi gani, atalala na njaa na wewe unashiba hapa, atakushughulikia!
Mheshimiwa Mwenyekiti, iko shida, ukienda sekondari Walimu wa sayansi ni kilio, hivi viwanda mnavyosema mnaanzisha siyo maana yake sayansi, Physics, Chemistry, Biology, Mathematics Walimu wako wapi? Walimu wa Sayansi wamekimbia Ualimu maana Ualimu haulipi, hata mimi ni mwalimu wa sayansi nimekimbia kwa sababu hali ni ngumu. (Makofi)
Walimu wanalia, walimu wa sayansi unakuta Mwalimu ni mmoja ana vipindi 50 kwa wiki, Mwalimu wa art ana vipindi vinne kwa wiki lakini mshahara unajua ni ule ule, hiyo biashara ngumu mzee! Kwa hiyo, walipeni walimu wa sayansi vizuri. Vijana wanapomaliza wamefaulu vizuri sayansi form four na form six wanaenda kwenye udaktari, wanaenda kwenye mambo mazuri na hata ninyi ambao mko hapa, wengi ambao mmesoma sayansi mmekimbia huko, wengi siyo walimu! Naomba Waziri unapokuja tuambie mmefanya nini kuhusu elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu mapato. Serikali ya CCM ni ya ajabu sana, wakiona Halmashauri za Wilaya zimetengeneza vyanzo vizuri vya mapato wanabeba, kule Serengeti tulikuwa na bed fee wakabeba, nimesikia sasa hivi wanataka wachukue property tax.
MHE. MARWA R. CHACHA: Sasa ninyi kwa nini msitengeneze vyanzo vya kwenu huko Serikali Kuu, Halmashauri itengeneze vyanzo vya mapato, ninyi mbebe, halafu madawati sisi tutatoa wapi tuwapelekee wale watoto, yaani ninyi mnachukua fedha zote mnakula, eeh mnatumia zote, kwa mfano, mimi nimekuwa Diwani tangu 2010, miaka yote Capital Development Grant (CDG) 26 percent ndiyo inakuja, mnafanya nini? Hamuwezi kufanya chochote.
Nawaambia CCM pumzikeni tupeni CHADEMA hapa tuongoze nchi tuwaoneshe mambo, maana mmeshindwa! nenda kwenye pembejeo ni kilio, kila kitu ni kilio, ukija nimepewa mahindi ambayo mkulima wangu ameenda amepanda hayakuota, sasa hivi wanapaka rangi wanasambazia wananchi kule hiyo ndiyo Serikali ya CCM. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.