Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii kwa uchache nizungumze yale ambayo nilikuwa nimepanga niweze kutoa kama ushauri kwa Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisiwe mbali saa nyingine kwa baadhi ya maelezo ambayo wenzangu wameyatoa, moja hasa likugusa kwenye bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka huu. Ni lazima tukubali ukweli kwamba tumepitisha bajeti ambayo siyo practicable, haifanyi kazi ile bajeti ni ndogo na hasa tukizingatia kwamba kwa kiwango kikubwa tumepunguza pembejeo kutoka kuwahudumia wakulima 999 mpaka kuwahudumia wakulima 300, hapa hatujawatendea haki wakulima wa nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zimeelekezwa katika maeneo mengine lakini pembejeo zimeshuka sana, sasa tuna ukame ambao umekabili nchi yetu, tulichokuwa tunatakiwa ni kuongeza nguvu kwa yale maeneo ambayo yamepata mvua ili wananchi wale waweze kuzalisha kwa wingi kuweza kufidia maeneo ambayo yalikuwa yamekosa mvua kwa kipindi hiki, ingeweza kuiweka nchi yetu kuwa salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hii ya ukosefu wa mvua bado katika Ukanda wetu wote wa SADC unazikabili nchi zote hizi na ukosefu wa mvua.
Kwa hiyo, ukame utaendelea na ukosefu wa chakula utaendelea. Nchi pekee wanayoitegemea ni Tanzania, Tanzania yenyewe uzalishaji wake umekuwa wa kusuasua, tunakimbilia wapi, hapo ndipo pa kujiuliza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba bajeti ijayo tukubaliane Waheshimiwa Wabunge tuhakikishe kuna maeneo lazima yawe ya kipaumbele na tuhakikishe Serikali inasikiliza kilio chetu. Tulipendekeza kwa nguvu zote kwamba bajeti ya pembejeo ipande tukapendekeza fedha wapewe NFRA waweze kununua chakula kwa msimu uliokuwepo, NFRA hawanunui chakula wanangoja bajeti ya Serikali, chakula wananunua walanguzi na watu wengine wakianza kununua wao bei zimeshapanda.
Kwa hiyo, tuwatake NFRA wanunue chakula mwezi wa tano kwa yale maeneo yenye uzalishaji ili kuwepo na chakula cha akiba kujihami kwa hali ambayo inaweza kujitokeza huko mbele tunapokwenda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kusisitiza ni kwamba nchi hii hakuna kitu ambacho kimeonesha mwelekeo mzuri kama Mfuko wa Maji na tozo ya shilingi 50, tuliishauri Serikali msimu uliopita kwenye bajeti ipandishwe iwe shilingi 100, leo hii miradi yote iliyofanyika inaonekana katika Majimbo yetu ni kwa shilingi 50 ambayo imeweza kutengeneza zaidi ya bilioni 75 ambazo zimekwenda katika maeneo yetu mbalimbali. Kwa hiyo, nitoe wito wa Waheshimiwa Wabunge, bajeti ijayo tuiombe Serikali hiki kilio itusikie, ipandishe hadi shilingi 100 ambapo tutakuwa na uhakika kwa mwaka zaidi ya shilingi bilioni 300 na miradi yote ya maji itaweza kufanya kazi au itaweza kumalizika kwa wakati pasi na kutegemea tu pesa kutoka Serikalini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba fedha zaidi ziangaliwe maeneo ya utafiti, Tanzania tuna matatizo ya kupata mbegu ambazo zinatumika katika maeneo yetu, asilimia 70 sasa hivi ya mbegu tunaagiza nchi za nje. Tatizo kubwa ni zile tozo za wale watafiti au wale wazalishaji mbegu wa hapa nchini, lakini ukizalisha mbegu nchi za nje au nje ya Tanzania unakuwa na duty free. Hivyo, makampuni ya uzalishaji mbegu yamekimbilia Zambia, Malawi, Zimbabwe, yanazalisha halafu yanaleta Tanzania kwa sababu kuingiza Tanzania ni bure. Kwa hiyo, kitendo hiki kinawavunja moyo watafiti, kinavunja moyo makampuni ya uzalishaji mbegu, hivyo basi kila mmoja anaona bora akazalishe nje au aende akanunue mbegu Belgium na afunge Tanzania halafu auze ndani ya nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine kinacholeta athari zaidi ni baadhi ya mbegu zinazotoka katika nchi hizo hazifanyiwi uchunguzi, matokeo yake zinaleta athari za maradhi kwa watu mbalimbali na hasa kwenye ugonjwa wa kansa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine linaloleta athari hapa…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Rehani.