Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na nikiri kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii lakini katika taarifa ya Mwenyekiti aliyowasilisha utashangaa kwamba hakuna suala lolote linalozungumzia juu ya Faru John, hakuna suala lolote linalozungumzia juu ya Loliondo, ni burning issues kwa sasa hivi, Watanzania walitaka wapate majibu, lakini Kamati haikuweza kwenda ili kuweza kupata kielelezo ili kuleta Bungeni, ni jambo la kushangaza. Sijui ni Kamati ipi ambayo inaweza ikalifanyia kazi zaidi ya Kamati ambayo ilikuwa maalum kwa ajili ya kuleta masuala haya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwa haraka, niongelee suala la kulinda corridors wanakopita wanyama, kama tulivyosikia kwenye taarifa ya Kamati ya Maliasili na Utalii, Wizara iliamua kuzuia maeneo ambayo ni mapito ya wanyama. Nazungumza hili kwa sababu wanyama ambao wanatoka Saadani kwenda Wamimbiki, Mvomero, Mikumi kuelekea mpaka Ruaha wananchi wamevunjiwa nyumba zao katika Wilaya ya Mvomero wakijumuisha pia wananchi wa Manispaa ya Morogoro kutokana na kupisha hizi corridor za wanyama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini cha kushangaza Serikali imewavunjia wananchi nyumba hizi, haikuwalipa fidia lakini Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imejengwa kwenye mapito hayo ya wanyama. Kama ni sheria ni lazima ikate pande zote mbili. Kuendelea kuwavunjia wananchi nyumba zao bila kuwalipa fidia huku Serikali ikiendelea kuweka majengo ya Halmashauri na kujenga nyumba za wafanyakazi si kuwatendea haki wananchi. Naomba Wizara iangalie upya suala hili na kama kuna uwezekano walipe fidia kwa wananchi hawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye mambo mengine ya migogoro ya wakulima na wafugaji Mkoani Morogoro. Ziko Kamati mbalimbali ambazo zimeundwa na Bunge hili lakini mpaka sasa hivi hakuna taarifa zozote ambazo zimefanyiwa kazi kusaidia kupunguza migogoro hii. Tunashuhudia watu wanapigwa mikuki ya midomoni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumemsikia Rais akifuta hati mbalimbali za mashamba. Tatizo ni ardhi, kwa nini mashamba hayo yasirudi yakawasaidia wananchi wa Wilaya za Mvomero na Kilosa ambako ndiko kwenye matatizo na migogoro ya kila siku? Hati hizi ambazo zimefutwa kwa nini ardhi hizi zisigawanywe kwa wananchi? Mpaka sasa ardhi zile zimeendelea kuwa mashamba pori pamoja na kufutwa huku wananchi wanaendelea kuwa na migogoro kutokana na uhaba wa ardhi. (Makofi)
Suala lingine ni kuhusu korongo lililojengwa la kuwatenga wakulima na wafugaji Wilayani Mvomero. Suluhu ya migogoro hii si kuendelea kuwatenga wakulima na wafugaji. Jamii hizi zinategemeana, hawa ni Watanzania, wanashirikiana lakini Serikali imeendelea na msimamo wake wa kuendelea kujenga korongo lile mbali na kwamba tulisema lisitishwe ili kutafuta suluhu kati ya makundi haya mawili ambayo yameendelea kuwa na migogoro ya siku hadi siku. Serikali imeendelea kutumia fedha zaidi ya shilingi milioni 17 kuendelea kuchimba korongo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mambo ambayo tunahitaji Wizara husika iyafanyie kazi ione. Kuna Kamati Maalum ya kutataua migogoro ya…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.