Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi, nianze kwa kusema kwamba na mimi ni Mjumbe wa Kamati hii, kwa hiyo ninaunga mkono hoja na nipongeze Wajumbe wenzangu wa Kamati pamoja na Mwenyekiti wa Kamati, ninaamini tumefanyakazi nzuri na tunaiomba Serikali ipokee ushauri ambao tumeishauri kwa ajili ya manufaa ya Taifa letu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama Mjumbe nilitaka nizungumze kwa ujumla mambo yanayohusiana na amani na utulivu wa nchi yetu. Ripoti ya utafiti iliyotolewa na Instituteof Economics and Peace inazungumzia na inaonesha kwamba Tanzania ni nchi ya 64 kati ya nchi 64 ambayo ipo hatarini kutoweka kwa amani. Kwa hiyo, Kamati yetu inahusika na mambo ya nje, ulinzi na usalama na ili ustawi wa amani katika nchi yetu ni lazima eneo hili liendeshwe kwa weledi, kwa utaalam, huku demokrasia ikishamiri katika nchi yetu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imetaja ma-group manne ya nchi namna ambavyo yana-exercise utawala wake. Inasema pale ambapo kuna full democracy kunakuwa kuna amani ya kutosha na kunakuwa na maendeleo ya kutosha kwa sababu watu wanakuwa na uhuru wa kutoa mawazo yao, watu wanaweza waka-challenge na kukosoana kwa amani kwa sababu kuna full democracy. Kwa hiyo, katika ripoti hii inaonesha kwamba kukiwa na full democracy nchi huwa ina flourish. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imeeleza vilevile kuna frauddemocracy, democracy ya kiasi; kunapokuwa kuna democracy ya kiasi kunaanza kuwa na viashiria vya uvunjivu wa amani. Kipengele cha tatu kuna hybrid regime ambayo ndiyo Tanzania tunaangukia hapo kwamba tuna utawala wa kichotara ambapo kuna aina fulani ya demokrasia, lakini kuna aina fulani ya udikteta. (Makofi) Katika ripoti hii inasema nchi yoyote ambayo inaangukia katika eneo hili inakuwa kwenye hatari ya kupoteza amani na Tanzania tupo kwenye hatari ya kupoteza amani kwa sababu tupo kwenye hybrid regime. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni authoritarian regime ambayo hiyo ni ya kidikteta kabisa ambako bado hatujafika na tumeona madhara ya kuwa na regime za namna hii. Kwa hiyo, tunapozungumzia suala la ulinzi na usalama ni jambo la msingi na ni jambo la muhimu sana tukifuata taratibu, sheria na kanuni tulizojiwekea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyazungumza yote haya kuweka kama msingi. Taifa letu ili tusiingie kuwa eneo la mwisho kabisa ambalo ni hatari, ni lazima tuzingatie sheria na taratibu ambazo tumejiwekea wenyewe. Kwa hiyo, ningeomba vyombo vya ulinzi na usalama na ningeomba watawala wanaohusika sheria ambazo tunazitunga hapa tukizifuata wote tutajikuta tunaiweka nchi yetu katika usalama na hatimaye uchumi wa nchi yetu utakua. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nikiangalia Wizara ya Mambo ya Ndani nataka nimnukuu Mheshimiwa Kafulila jana ali-tweet, amezungumzia tuna chombo kwa mfano hiki cha National Drug Control Council ambapo ndani ya chombo hiki yupo Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani, ambao hawa wote wanashughulika na chombo hiki kwa ajili ya kudhibiti pamoja na Waziri wa Afya naye yumo na wengineo. Hawa wote ni chombo ambacho kimeundwa kwa ajili ya kudhibiti dawa za kulevya na kipo kisheria. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimezungumzia masuala ya ulinzi, kila Kiongozi ana mipaka yake na kila Kiongozi amepewa majukumu yake. Kuna chombo kama hiki nilitaka niulize Wizara ya Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Mwigulu upo hapa, kumetokea kitu gani badala ya hiki chombo kushughulika na masuala ya msingi kama haya ambayo sisi sote tunaunga mkono vita ya kupambana na dawa za kulevya, leo siwaoni Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri wa Afya mkishughulika na mkitoa matamko kwa sababu ninyi ndiyo wenye chombo hiki, tunamuona Makonda ndiyo amebeba bango la nchi nzima ambaye ni kiongozi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam sawa tu na Mheshimiwa Amina Masenza, Mkuu wangu wa Mkoa pale Iringa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Mheshimiwa Makonda yeye ndiyo abebe bango na chombo kikubwa ambacho kinatakiwa kifanye kazi hiki kikae kimya. Ningeomba haya mambo Serikali ijaribu kufafanua, kwa sababu haya ndiyo mambo ambayo yanasababisha utengamavu na utulivu wa nchi yetu upotee bila sababu. Mtoto aliyehongwa na mama yake huwa tunamuita mummy’s boy au mummy’s girl lakini inaonekana Makonda labda ningemuita daddy’s boy. Kwa sababu anaweza akasema chochote anachotaka wakati wowote hajui na mipaka yake, hii inaweza ikatuletea matatizo katika nchi yetu. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda siyo mtaalam wa mambo ya uchunguzi. Mwenyekiti wangu wa Kamati umekaa kwenye kitengo hicho utaweza kutusaidia. Polisi wamesomea, wanaweza kufanya investigation ya mambo haya, sasa watu wote tumekaa kimya nchi hii where are the lawyers? tuna Tanganyika Law Society,where are thelawyers, tunapoona mambo yanaenda vibaya tumekaa kimya. Where are thejudges hatuoni Majaji wakitoa matamko kuonesha kwamba kila mtu akae kwenye msimamo wake ili nchi yetu iweze kuwa na utulivu na amani, watu wote wamekaa kimya, tunalipeleka wapi Taifa ambalo kila mtu akiamka asubuhi anaamua kufanya jambo analolitaka na wachungaji wamekaa kimya, lakini wengine tunaona wakipewa zawadi wanasema at least mimi nasema hapa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana kuna checks and balance, wahenga/wataalam wa mambo ya utawala walivyoamua kuweka mihimili mitatu hawakuwa wajinga, waliona anaweza akatokea kichaa mmoja akaamua kufanya anavyotaka, Bunge letu hili lipo kwa ajili ya kazi hiyo mambo yanapokwenda hovyo lazima tusimame kama muhimili kumrudisha nyuma yule anaekwenda vibaya na maamuzi tuliyoyafanya. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, my question is where are the judges in thiscountry and where are the lawyers, tunawasomesha kwa gharama kubwa wanasoma sheria ili iweje? Lengo tunataka tukae katika nchi yetu kwa usalama na haki. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imezungumza vizuri sana juu ya jinsi ambavyo amani inaweza kutoweka. Lakini kwa sababu ya muda ninataka kusema Bunge hili kwa sababu ya kutokujua au kwa makusudi tulitoa maamuzi ambayo mengine ni ya hovyo katika nchi yetu, ni wakati sisi kama watunga sheria na muhimili ambao ni wa muhimu katika Taifa letu tufike mahali tujitafakari. Kwa mfano, tulipitisha sheria ambayo inaminya upatikanaji wa habari ambayo inawasaidia watu wachache, hii sheria tulipitisha hapa lakini mwisho wa siku itatugeuka ni kiashiria ambacho kinaweza kikasababisha tuvunje amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Bunge letu hili ambao ni muhimili muhimu katika taifa letu limekosa uhuru, limekuwa ni Bunge ambalo linaminywa, hatuwezi kuikemea Serikali tena, why are we here? Mheshimiwa Mwenyekiti, tupo hapa kufanya nini kama hatuwezi kuidhibiti Serikali na tunapoidhibiti Serikali siyo maana yake tunataka kuiangusha, tunataka itembee katika mkondo wake ili amani yetu itulie na ndiyo kazi ya Bunge. Kazi ya Bunge ni kuidhibiti na kuisimamia Serikali ienende kama inavyopaswa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mwenzangu hapa ametoa mwongozo tunaye Katibu wa Bunge hapa anayetakiwa atuongoze tunapokaa hapa; sasa leo anaenda kwenye vyombo vya habari anasema Bunge limekosea. Na yeye anafanya kazi yetu ya Bunge hatujaajiriwa na yeye hapa with duerespect, anafanya kazi ya Bunge hajatuajiri yeye sisi hapa; anatakiwa afuate maagizo yetu. Na ana wataalam wanaotushauri anatakiwa atuelekeze where are we heading? Haya ni masuala tunahitaji tujadiliane siyo kwa kugombana ni kwa kujadiliana wote kwa pamoja. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine la pili ni Serikali kupiga marufuku vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara, huko ndiyo tunaweza kuona mambo mengi ambayo yanaenda hovyo, tukaongea kwa uhuru, tukaisaidia Serikali ienende vizuri. Haya mambo tunakaa kimya tunashangilia mtu mmoja anaamua halafu tunakaa kimya watu wote, where are we heading? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine Asasi za Kiraia zikijaribu kuzungumza nazo zinazuiwa na zinakatazwa, haya ni masuala ambayo tunapaswa tujiulize tunakwenda wapi. Ni maoni yangu kwamba ni vizuri tukasonga mbele na ni vizuri tukatafakari kama Bunge, je, tunafanya wajibu wetu, tunatimiza wajibu wetu kama muhimili? MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa, dakika moja tu.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niseme hii nchi yenye Bunge kibogoyo, TAKUKURU kibogoyo, vyombo vya habari bubu, NGO bubu na siasa bubu, polisi kibogoyo na National Drug Control kibogoyo, hatuwezi kuepusha michafuko katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe wote kwa pamoja na kwa kumalizia dakika ya mwisho kabisa mchungaji mmoja kule Ujerumani wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia aliwahi kusema; “Silence in the face of evil it is evil itself, God will not hold us guiltless not to speak is to speak, not to act is to act.” Kwa hiyo, hatupaswi tukae kimya katika haya mambo haya mabaya, ningewaomba Wabunge tushirikiane wote kwa pamoja tuulinde muhimili wetu, nashukuru sana.