Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi japo nilikuwa najua nina dakika kumi, nimeshtukiziwa ziko tano, anyway nitajaribu kuzitumia hivyohivyo. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kuunga mkono na kupongeza Serikali kwa maamuzi yake ya kufungua Balozi katika nchi sita ikiwemo Israel, Korea, Algeria na nyinginezo pamoja na Uturuki. Itakumbukwa wakati fulani hapa alipofanya ziara Mfalme wa Morocco ilitokea hali kama ya sintofahamu kwamba kwa kuwa sisi tunaunga mkono Polisario inakuwaje tunapokea ugeni kutoka Morocco, lakini nieleze tu kwa uzoefu wangu kwamba misimamo mbalimbali haikuzuii kuwa na bilateral relations ndiyo maana hata Polisario headquarters yao ipo Algeria, lakini bado wana uhusiano Algeria na Morocco. Vivyo hivyo sisi msimamo wetu kuhusu PLOunajulikana lakini ndiyo maana tunafungua Ubalozi Israel kwa sababu tunapokwenda kujenga uchumi wa viwanda lazima tufungue milango zaidi ya kiushirikiano na nchi ambazo zimepiga hatua katika nyanja mbalimbali, mfano nchi ya Israel wako mbali katika teknolojia ya kilimo cha umwagiliaji, kwa hiyo naunga mkono sana jitihada hizo za Serikali. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema kwenye Kamati na mimi ni Mjumbe wa Kamati, kuchanganya fedha za ziara za viongozi na fedha za Wizara zinaonyesha picha kubwa kwamba Wizara hii ina fedha nyingi, lakini kumbe fedha zile siyo za kwake, matokeo yake Wizara inashindwa kufanya kazi nyingi za msingi. Mfano mmojawapo ni ukarabati wa majengo ya Kibalozi, tuna eneo kule Maputo ambalo tumepewa na Serikali ya Msumbiji toka mwaka 1978, liko eneo ambalo ni prime, lakini mpaka leo halijajengwa. Sasa ni muhimu sana Serikali ikaanza kuangalia maeneo kama hayo ambayo ni prime lakini tumepewa zaidi ya miaka karibu 40 sasa hivi, tuone tunayafanyaje ili hata wale waliotupa wasije wakajatua kutupa. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu mikataba; ukiangalia katika ripoti ya Kamati mikataba zaidi ya 43 bado haijaridhiwa na Bunge na hapa niseme jambo moja, Wizara ya Mambo ya Nje kazi yake ni kuratibu masuala haya, ninaishauri Serikali tuwe na kitengo maalum kama kitakuwa chini ya Waziri Mkuu au Ofisi ya Rais ambacho kitakuwa kinafuatilia masuala yote kama haya. Tumeona mikataba mingi inasainiwa, lakini Wizara za kisekta zinashindwa ku-finalize kuifanya ile mikataba ifikie hatua ya kutekelezwa ikiwa ni pamoja na kuifikisha kwenye Bunge letu kwa ajili ya kuridhia. Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuondokane na jambo hilo pengine tungekuwa na kitengo maalum, kwa sababu ninavyofahamu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje hawezi kumuagiza Katibu Mkuu wa Kilimo au Viwanda na Biashara kwamba jambo hili mbona halijatekelezwa, lakini tukiwa na kitengo maalum cha kufuatilia masuala kama haya inaweza ikatusaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo pia linagusa Wizara ya Fedha, wawekezaji wengi ukizungumza wanalalamika sana kuhusu double taxation na protection of investment. Ukizungumza na Jumuiya za Kibalozi zinasema kwamba wawekezaji wao wangependa kuja kuwekeza lakini kwa sababu hatuna mikataba ambayo inaruhusu double taxation kuondolewa na protection of investment inawa-discourage. Kwa hiyo, niombe Wizara ya Fedha ishirikiane na Wizara ya Mambo ya Nje kwa ukaribu kwa sababu hata kama tunataka kukusanya pesa tu bila kujenga misingi imara ya wapi tutakusanya tutakuwa hatuwezi kufikia malengo tunayokusudia. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho au la pili kutoka mwisho kutokana na dakika chache nilizonazo ni kuhusu wahamiaji hasa wale ambao tumewapa uraia kule Ulyankulu. Kwa kweli Serikali ya Mkoa wa Tabora na Serikali ya Wilaya ya Kaliua inatumia muda mwingi na resources nyingi katika kuhangaika na masuala yaliyopo kwenye maeneo yaliyokuwa ya wakimbizi ya Ulyankulu. Kwa jinsi tulivyotembelea Kamati wanasema, sijui kama lugha hii itakuwa nadhifu, lakini jambo lile ni kama vile kumbemenda mtoto, sasa ku-deal nalo its very delicate. Tumewapa watu uraia, wanataka kuwa na nchi ndani ya nchi, sasa jambo hili tujifunze wakati ujao, sisi tulikuwa nchi ya kwanza kutoa uraia kwa watu wengi duniani kwa wakati mmoja, tutizame jambo hilo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.