Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa, mimi nataka nichangie mambo machache na nataka nijielekeze kwenye Kamati ya Mambo ya Nje na Usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, dhana ya usalama ina mitazamo mingi, lakini usalama wa nchi yoyote duniani huanza na raia wake. Raia ndiye mlinzi namba moja wa nchi yake. Unaweza ukawa na jeshi kubwa, lina vifaru vingi, bunduki nyingi, askari wengi lakini raia kama hawako tayari kulinda usalama wa nchi yao, nchi hiyo haiwezi kuwa na usalama, itakuwa na utulivu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kitakwimu duniani, Tanzania ni moja kati ya nchi 20 za mwisho ambazo raia wake wanafuraha. Raia wanapokuwa hawana furaha, kuna mambo mengi yanayochangia. Sasa msingi wa yote haya ni nini, ni haki. Jambo la kwanza ambalo kama Taifa muhimu kabisa kulipa kipaumbele katika kuhakikisha usalama wa nchi yetu unaendelea kushamiri ili mambo mengine yaweze kufanikiwa ni haki za raia kuheshimiwa na haki hizi ni haki za kiraia, lakini vilevile haki za kiuchumi. Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mifano michache. Leo Bunge sisi tunapitisha sheria, nataka nitolee mfano sheria ya SUMATRA. Basi lenye kubeba abiria 40 ili lipate leseni ya SUMATRA linatakiwa kulipa shilingi 80,000. Ukiangalia cost per unit maana yake kila kiti cha abiria ni shilingi 2,000. Lakini bodaboda ili afanye biashara yake anatakiwa alipie SUMATRA shilingi 20,000 maana yake kiti kimoja kile cha abiria yeye anakilipia shilingi 20,000 hakuna haki. Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanafunzi wa Chuo Kikuu anaenda chuoni hana uhakika wa maisha yake, mfanyabiashara anayeenda sokoni kufanya biashara yake hana uhakika wa kufanya biashara yake katika mazingira salama. Maana yake tumetengeneza sheria nyingi ambazo hazimfanyi mtu masikini kuweza kuwa na uhakika wa maisha yake, hii ni hatarishi kwa usalama wa nchi yetu. Kwa hiyo, mimi ningeshauri Serikali, hakuna jambo la msingi kuliko jambo lolote kama haki za raia kuheshimiwa. Tunapoanza kujenga msingi wa kukandamiza haki za raia katika nchi, tunajenga Taifa la watu wanaonung‟unika ambao hawatakuwa na uzalendo katika moyo wao, ambao hawatokuwa tayari kulipigania Taifa hili. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu za dunia za United Nations za mwaka 1974, Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi ya 107 katika nchi ambazo raia wake wanafuraha, leo imeporomoka, ni swali muhimu la kujiuliza. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kama Taifa tulikuwa na heshima yetu katika medani ya kimataifa, heshima ambayo ililijenga na kuijenga taswira ya nchi hii kutokuungana na watu wanaokandamiza watu wao, leo Serikali iko katika mchakato wa kufungua Ubalozi wa Israel. Mwalimu alim-consider Muisraeli kuwa ni mkandamizaji wa haki za watu duniani ambaye amekalia kimabavu Taifa la watu wengine, sisi tumeondoka kwenye msingi uliojenga Taifa hili kwa muda mrefu. Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikitika sana, African Union kuichukua nchi ya Morocco kuiingiza katika Jumuiya ya Nchi za Afrika na sisi kama Taifa hatujatoa stand mpaka leo, ni jambo la kusikitisha sana kama nchi. Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru.