Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti na mimi nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia Kamati hizi ambazo ziko mbele yetu leo, nitaanza na upande wa Wizara ya Ulinzi. Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1974 aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwalimu Nyerere, aliwaondoa watu wawili kutoka Jeshini, Mkuu wa Majeshi na Mnadhimu Mkuu na kuwapeleka kwenye shughuli za kiraia. Mkuu wa Majeshi akawa Waziri wa Vijana na Michezo na Mnadhimu Mkuu akawa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Sukari la Taifa. Huyu ambaye alienda kuwa Waziri na baadae Balozi tayari amefanyiwa taratibu za kijeshi za kustaafishwa na kupata mafao yake inavyostahili. Huyu ambaye alikwenda kuanzisha SUDECO mpaka leo tunavyozungumza, Jeshi halijamfanyia taratibu za kustafishwa kama mwanajeshi. Toka mwaka jana mwezi Februari nimekuwa nikileta swali hapa Bungeni kuhusiana na Kanali Kashmir kuhusu haki yake ya kustaafishwa kama mwanajeshi ili aweze kupata haki, swali hilo limekuwa likipigwa danadana, napata majibu kwamba Wizara ya Ulinzi haina majibu bado. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba leo Waziri wa Ulinzi alieleze Bunge hili Tukufu, Mzee huyu ambaye sasa ana miaka 80 wanataka apoteze maisha kabla ya kupewa haki zake? Kwa sababu siyo yeye aliyetoka Jeshini kwenda uraiani, ameondolewa na Amiri Jeshi Mkuu Mwalimu Nyerere. Mwenzake aliyetoka naye Mkuu wa Majeshi wa zamani amestaafishwa rasmi wakati wa utawala wa Mzee Mkapa, tatizo ni nini kwa Kanali Kashmir? Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kunaanza kujengeka hisia, Kanali Kashmir ni Mtanzania mwenye asili ya kiasia. Kuna hisia zinaendelea miongoni mwa Watanzania wenye jamii ya kiasia kwamba yeye anatengwa kwa rangi yake, wakati ni mtu ambaye alilitumikia Jeshi letu na aliitumikia nchi hii kwa uzalendo wa hali ya juu sana. Kwa hiyo naomba leo Waziri wamenikwepa kwenye maswali sasa at least Kamati imekuja na ninaiomba Kamati pia kama majibu ya Waziri hayakutosheleza imtembelee Kanali Kashmir apate haki yake na tumuombe Mungu ampe uhai mpaka hapo aweze kupata haki yake kabla Mwenyezi Mungu hajamchukua, ana umri wa miaka 80 sasa hivi. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ninataka kulizungumzia ni Sera ya Mambo ya Nje. Sasa hivi kuna tatizo kidogo, nakubaliana kabisa na ndugu yangu Mheshimiwa Chumi kwamba ni lazima Sera ya Mambo ya Nje ibadilike kuendana na wakati lakini kuna tatizo la kubadilisha misimamo bila kufuata misingi ya Sera ya Mambo ya Nje. Ni kweli tumempokea Mfalme wa Morocco hapa siyo nchi ya kutengeneza maadui lazima tutengeneze marafiki, lakini unapompokea si lazima uhoji kile ambacho umekuwa ukikisimamia kwa takribani mika 40? Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wetu hakwenda kwenye vikao vingine vyote vya AU, vikao viwili hakwenda, inawezekana kuna maelezo ya kwa nini Rais hakuhudhuria vikao vya AU, lakini kikao cha AU kinachohusiana na kuirudisha Morocco Rais amekwenda na humu ndani Wizara ya Mambo ya Nje haijatupa maelezo yoyote kuhusiana na haki za watu wa Saharawi. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Azimio la Umoja wa Mataifa Azimio Namba 2285 la mwaka 2016 linalotaka kura ya maoni ya watu wa Sahara Magharibi kuamua hatima yao. Sasa juzi wenzetu wa SADC wamepiga kura kukataa Morocco kurudishwa ndani ya African Union. Sisi tuko SADC, tunahitaji maelezo ya Serikali tulipigaje kura yetu? Haya siyo mambo ya kuchezea, tukiacha watu wafinyange finyange Sera ya Mambo ya Nje ambayo ndiyo imetengeneza nchi hii hatutakuwa na nchi, kwa sababu ukishavunja principles unabaki nani wewe? Mheshimiwa Mwenyekiti, the same thing to Israel mimi sipingani kabisa kufungua Ubalozi Israel, kuna watu wetu wengi Watanzania wanahitaji huduma za viza, wanahitaji huduma za kibalozi kwa ajili ya Hijja wanapokwenda Israel, lakini sisi ni waumini wa two state solution. Tumekwenda UNESCO, tumepiga kura, kura yetu inaendana kinyume na maamuzi yetu ya two state solution, kura tuliyopiga Paris tarehe 16 Oktoba mwaka jana. Tunaambiwa na Afisa wa Mambo ya Nje ambaye alipiga kura ile pamoja na Israel kinyume na maelekezo ya Wizara ya Mambo ya Nje kwamba amechukuliwa hatua, tunahitaji maelezo ya Serikali, hapa kwa sababu hizi ni matters of principle.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufungua Ubalozi Misri waligombana na Israel wana Ubalozi, there is no problem about that, lakini tunachokitaka ni kuhakikisha kwamba yale mambo ambayo tunayasimamia yale tusiende kinyume nayo. Ninaomba Kamati ya Mambo ya Nje na wakina Mheshimiwa Msigwa Wajumbe huko wananisikia, haya ndiyo mambo ya kwenda kui-pin down Serikali kwenye Kamati, kwa sababu ni principle atakuja mtu hapa atavuruga tu, anaweza akaanza akasema kwamba apartheid was right, kwa sababu tu tumevuruga vuruga misingi ambayo tunayo. (Makofi) Jambo la mwisho napenda nimpongeze Rais kwa kufanya uteuzi wa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya, hii Waheshimiwa Wabunge ndiyo kazi ya Bunge. Tusingepiga kelele humu ndani na kuikumbusha Serikali kwamba kuna jambo hili... (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji) MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Zitto,