Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimwa Mwenyekiti ahsante, ningejua kama Mheshimiwa Zitto ana utamu huu ningempa hizo dakika tatu lakini ngoja niendelee. Hilo la mwendelezo ni la msingi sana kwamba amemteua Kamishna na mimi nimesikia kwenye redio wakati nakuja, ni jambo jema kwamba sasa kuna chombo maalum kinashughulikia dawa za kulevya ni jambo jema sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mambo mawili tu ya kwa haraka. La kwanza, ukurasa wa 35 wa kitabu hiki cha repoti kinazungumzia Sera ya Mambo ya Nchi za Nje kwamba mpaka sasa tunavyozungumza Sera ya Mambo ya Nchi za Nje inayotumika ni sera ya mwaka 2001. Nafikiri wasemeji waliopita akiwemo Mheshimiwa Zitto nimemsikia na Mheshimiwa Bashe akizungumza shida iko hapo. Kwa mujibu wa repoti hiyo ukurasa wa 35 wanasema sera mpya na mapitio ya sera hiyo ya mambo ya nchi za nje inayozingatia diplomasia ya kiuchumi na mapana yake bado haijafanyiwa kazi. Mimi nilikuwa nafikiria Waheshimiwa Wabunge hapo ndipo kwenye shida. Tuiombe Serikali kama ni kalenda ya miezi sita, ya mwaka mmoja basi wenzetu wa Mambo ya Nchi za Nje wawe wametuletea sera hiyo ambayo inafanyiwa mapitio tangu mwaka 2001, haiwezekani sera ifanyiwe mapitio tangu mwaka 2001 mpaka leo. Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala haya ya kuzingatia diplomasia ya uchumi ndiyo masuala ya msingi ya sera mpya ambayo kila siku tunaisema lakini kwa mujibu wa taarifa ya wenzetu wa Kamati na ndugu yangu Mheshimiwa Balozi Adadi mmefanya kazi nzuri sana kuikumbusha Serikali kwamba lazima tuipe time frame. Kama ni miezi sita, kama ni mwaka mmoja watuletee sera hiyo ambayo imefanyiwa mapitio inayozingatia diplomasia ya kiuchumi. Hoja yangu ya pili nimeshangaa kidogo na Waziri wa Ulinzi uko hapa nimeshangaa kidogo. Ukurasa wa 30 wa repoti hii wanasema, hatuna Sera ya Ulinzi, hilo jambo limenishtua Waheshimiwa Wabunge, kama hatuna sera ya ulinzi tumepelekaje askari wetu Congo, Darfur, Lebanon na kwingineko? Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka nipate maelezo wakati Mwenyekiti unahitimisha ni kwa nini hakuna sera...
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa muda wako umeisha.