Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Katika dakika zangu tano nitatumia dakika mbili na nusu na mbili na nusu ntampatia Mheshimiwa Sugu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kifupi tu nimwambie kaka yangu pale Mheshimiwa Bilakwate kwamba kwa kumtetea Makonda, Makonda siyo mamlaka ya uteuzi. Kwa hiyo, anatwanga maji kwenye kinu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi nataka kuona Bunge hili linavyoweza kushauri Serikali hasa kwenye mamlaka ya uteuzi. Tumeshuhudia sasa hivi kama tulivyosikia Wakuu wa Mikoa wanaamua tu kukurupuka na kutoa maagizo, kama alivyotoka kusema Ndugu yangu Mheshimiwa Mlinga hapa. Tumesikia pia Mkuu wa Mkoa wa Mtwara naye na nimeona mimi mwenyewe meseji jana, naye anaanza kuwaambia watu kama wanafahamu watu wanaoshughulika na madawa ya kulevya basi wamtaarifu ili na yeye apate kiki kwenye vyombo vya habari kama ilivyofanyika maeneo mengine. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi huu ni uvunjifu wa maadili ya viongozi. Tumeona hapa Bunge likiwa haliheshimiwi, Wabunge wanakamatwa muda wowote, mimi mwenyewe ni mwathirika. Mkuu wetu wa Mkoa wa Mtwara alitoa taarifa kwa kuagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama Wabunge watatu wa Wilaya ya Masasi tukamatwe kwa sababu hatukutaka kuhudhuria mkutano wake aliokuwa anataka kujadili mambo ambayo Waziri Mkuu tayari alikuwa anayafanyia kazi. Bahati nzuri viongozi walituheshimu wakakataa kutekeleza maagizo yake. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kifupi tuone Bunge sasa linasimamia misingi yake. Tusipoweza kuishauri vyema Serikali hasa mamlaka ya uteuzi, tumwachie pia Waziri wa Mambo ya Ndani afanye kazi zake na Mawaziri wote wafanye kazi zao. Wateule wa Rais wameonesha kama wao ndiyo watu muhimu sana kwenye Taifa hili kuliko hata Mawaziri ambao wana mamlaka makubwa kimsingi kuliko Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na wengine. Mheshimiwa Mwenyekiti, napata hofu kwa sababu vurugu kubwa zaidi zitatokea kuanzia mwakani. Hawa wote walioteuliwa na Mheshimiwa Rais ni walewale ambao walikuwa makada na wanataka kwenda kugombea nafasi mbalimbali katika majimbo yao hasa zaidi Ubunge. Kwa hiyo, tutafika wakati misuguano au mivutano itakuwa mikubwa sana katika maeneo yetu, tuliangalie hili jambo kwa wema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.