Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. CAPT. GEORGE H. MKUCHIKA - MWENYEKITI KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi tena. Sitamaliza hiyo robo saa kwa sababu Kamati yangu wamechangia watu watatu; hapakuwa na maneno mengi sana. Nadhani hiyo ni kuonesha alama wanazoipa Kamati, nadhani zaidi ya asilimia 90 hawakuwa na mambo ya kusema. Mheshimiwa Mwenyekiti, Wajumbe wawili wamechangia humu ndani, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete na Mheshimiwa Dkt. Semesi. Mheshimiwa Juma Othman Hija alichangia kwa maandishi. Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, yeye ametoa rai kwamba kila Mbunge ajiheshimu mwenyewe kwanza. Sisi tunakubaliana naye na ndiyo msimamo wa Kamati yangu kwamba kama hapa ndani kila mmoja atajiheshimu, nafikiri hata kazi ya Kamati hii itakuwa rahisi sana. (Makofi) Mheshimiwa Dkt. Semesi amependekeza Kamati iwe na Wajumbe 50 kwa 50. Nataka nimweleze kwamba Kamati hizi hapa ndani zinaundwa kulingana na uwiano wa Wabunge kwenye Vyama. Kamati zote zilizomo humu ndani kile Chama ambacho kina Wabunge wengi ndicho kina Wajumbe wengi. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Kamati zote zinategemea hiyo. Ukichambua hizi Kamati, ni yale yale ninayoyakemea kwamba kwa utaratibu wa humu ndani, kama mmoja anaongea, wewe unanyamaza. Nadhani ndiyo mnaona umuhimu wa Kamati yangu, kwamba wako watu ambao lazima tushughulike nao ili hapa ndani pawe shwari. (Kicheko/Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukitoka hapa, nenda kachambue Kamati yote, in reality, ratio iko 7:3 nenda Kamati zote. Kwa hiyo, siyo kwamba hii Kamati ya Maadili isan exception, hapana. Ndivyo ilivyo kwa muundo wa Kamati zote. La mwisho, niseme tu kwamba anayeunda hizi Kamati, sio Wajumbe wa Kamati, ni Mheshimiwa Spika. Mheshimiwa Mwenyekiti, watatu, ndugu yangu hapa, Mheshimiwa Juma Abdallah Juma, yeye amechangia kwa maandishi, anaipongeza kazi ya Kamati na anapendekeza kanuni ziangaliwe upya ili kuwabana wanaofanya fujo ndani ya Bunge. Ninachotaka kusema ni kwamba, Kamati ya Kanuni ndiyo inayotengeneza kanuni, sisi tunafanya kazi kwa kutumia kanuni zilizotengenezwa na Kamati ya Kanuni na kupitishwa na Bunge Zima. Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimalizie tu kusema kwamba sisi kama Kamati ya Maadili, tunatoa rai na kama tulivyosema pale mwanzo, hapa ndani kuna maendeleo makubwa sana. Ukilinganisha vurugu zilizokuwepo mwanzoni wakati Bunge linaanza na tulivyo leo, yapo mabadiliko makubwa. Kwa mtu yeyote ambaye akili yake haina matatizo, anaelewa kwamba tumepiga hatua. Yule ambaye hataki kuelewa, mwache aendelee kutokutaka kuelewa kwa sababu ndiyo watu wengine walivyo, lakini hali ya hapa katika Bunge nadhani kwamba tumeanza kwenda vizuri. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nimalizie... Mheshimiwa Mwenyekiti, si ndiyo haya haya ninayokemea? Mimi si ndiyo nimepewa nafasi hapa kusema? Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimalizie kwa kusema hivi, tukiwa hapa ndani, naomba tuendelee kuheshimiana, kuvumiliana, kuzingatia kanuni, kuheshimu kiti na nimalizie kusema tu kwamba ukizomea wakati mwingine wanasema, haujajenga hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka leo tuondoke wote na msemo huu ambao katufundisha Baba yetu Mwalimu Nyerere. Alitufundisha hivi, argue, don’t shout. Tuondoke na spirit hiyo, Baba yetu katufundisha, “argue don’t shout.” Kama mwenzio anaongea, kapewa nafasi, nawe ghafla bin vup, unabonyeza unasema „nini wewe?” “Mambo gani hayo?” You are shouting. Argue, don’t shout. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba Bunge lako Tukufu likubali kuipokea taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge pamoja na mapendekezo yake ili yakubaliwe na kupitishwa na kuwa maazimio ya Bunge. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.