Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipatia hii nafasi. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kunipatia afya njema. Ukimuona mtu mzima analia basi ujue amepatwa huyo mtu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka ni-declare interest kama mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PIC au Uwekezaji. Kwa kweli, kama ingekuwa Wabunge wote wanapata taarifa za mikataba mibovu ambayo imeingiwa na mashirika mbalimbali basi, humu ndani tusingekuwa pamoja tungekuwa tumepata msiba mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitu ambacho nimejifunza katika kukaa katika Kamati ya Uwekezaji, kwanza ni mikataba mibovu ambayo imeifanya nchi isiweze kwenda. La pili, tumeshindwa kusimamia Sheria ya Uwekezaji. Tatu, kulindana kulikopitiliza, matokeo yake wanapewa watu nafasi ambao hawawezi kuzifanyia kazi, iwe Mwenyekiti wa Bodi au awe Mkurugenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na ninakotoka, Mkoa wa Lindi na Mtwara. Mkoa wa Lindi na Mtwara tulikuwa na viwanda vya korosho vinane na wawekezaji au ubinafsishaji wakapewa vile viwanda kwa bei ya kutupa. Tangu walipopewa viwanda vile wamevifungia mpaka leo, je, Serikali ipo, haipo? Serikali ina macho, haina macho? Lakini wamelifumbia macho na kuacha viwanda vile vikifungwa mpaka leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wamewapa wawekezaji, wale wawekezaji wamevifunga vile viwanda, wametoa mashine na kuzipeleka Mozambique ambako wamefungua viwanda vingine na kuwaacha watu wa Mtwara na Lindi wakiwa hawana ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kushangaza watu wale wale wamepewa kazi ya kupeleka korosho nje as a raw material, tujiulize tunajitambua? Kama kweli tunakwenda katika uwekezaji wa viwanda kwa mfumo huu hatutoki, maana mnawajua nani anasafirisha korosho nje, anapeleka ajira nje, anapeleka kila kitu nje, viwanda amevifungia kwa sababu ya nani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Waziri mwenye dhamana atuambie kwa nini viwanda hivi vimefungwa zaidi ya miaka kumi wananchi hawana ajira na korosho inapelekwa nje ajira inapelekwa nje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii haikubaliki ni aibu. Lazima tujitambue na tufunguke, kwa hiki tunachofanyiwa ni aibu. Hata kama utasema tunataka kuwekeza kama mikataba mibovu itakwenda hivi, hakuna uwekezaji hapa. Ina maana tunataka kutoa mfumo wa kukandamiza taasisi zetu kuhakikisha watu wa nje wanakuja kuwekeza hapa na kuleta pollution. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikwenda Amerika ya Kusini; uwekezaji umepelekwa mkubwa sana Amerika ya Kusini; sasa hivi Amerika ya Kusini ni eneo ambalo lina pollution ya hali ya juu. Na Tanzania kwa mikataba mibovu tutakayoendelea nayo nina imani baada ya miaka mitano nchi hii itakuwa polluted yote; na mazingira yote mnayoyaona haya yatakwisha. Tujitambue na tusimamie kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na viwanda vya nguo zaidi ya kumi MUTEX, MWATEX, Urafiki, Sungura Textile, Tabora Textile na Riziki Textile, lakini viwanda vile vyote vimefungwa. Na katika kufungwa bahati nzuri Kamati ilitembelea EPZA, tukaenda kuangalia kiwanda ambacho kinatengeneza nguo za jeans, tukawauliza je mnapata wapi nyuzi? Wametujibu kuanzia sindano, uzi na kila kitu tunapata kutoka China. Tujiulize kweli tuko serious na uwekezaji? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naona ndugu yangu Mwijage wamekupa mzigo mzito kwa vile uliokuwa nao chini hawako serious kukusaidia, utakuwa unakimbia peke yako wataalam wako huku pembeni hawako serious na wewe kabisa. Haiwezekani tumefunga viwanda vya kusokota nyuzi, leo nyuzi zinatoka China, maana yake ni nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka uchumi endelevu, pana uchumi hapo? Wanawaajiri watu kwa miezi mitatu mitatu, Mtanzania huyo atapata faida gani hapa? Ina maana unamchukua miezi mitatu unamuachisha, miezi mitatu unamuachisha, hii nchi haiwezi kwenda katika mifumo ya namna hiyo ya mikataba mibovu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na viwanda vya kukamua mafuta; tulikuwa na Tanbond inatoka Tanzania, Super gee inatoka Tanzania, pride Tanzania na Mara ghee Tanzania; leo viwanda vyote mmefunga. Na wamevifunga tunaagizia blue band kutoka nchi za nje, are we serious? Halafu unapotaka kutuambia sisi tunakwenda katika mfumo wa viwanda vyote tumevifunga tunategemea vya nje hivi vina kasoro gani hata vimefungwa? Nenda Urafiki ni ma-godown, nenda Mtwara ni ma-godown, je, maendeleo haya mnayoyafanya mnayadumaza kwa makusudi halafu mnasema sasa hivi tunataka ulimwengu wa maendeleo ya viwanda, tutafika katika mfumo huo? Hatufiki, mikataba mibovu imefikia mahali ambapo sijui dawa yake ni nini, ni msiba kwa Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelewa na Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), walikuwa na maeneo yao ya madini Tanzania nzima viwanda vya chumvi Lindi, Mtwara na Kigoma. Vile viwanda vyote vimefungwa na walipewa maeneo mengine kama ya uwekezaji ya Mererani. Mererani ina vitalu 29, STAMICO amepewa vitalu viwili tu. Mle ndani watu ni fujo tu na ndiyo maana unaona leo Tanzania tuna Tanzanite lakini inapelekwa nje ni kwa ajili tumesababisha njia za panya. Tunashindwa nini kuwauliza wale watu kwa nini wale watu wote wasishirikiane na STAMICO ili akaweze kupeleka uchumi, lakini imeshindikana yote ni kwa ajili ya mikataba mibovu. Tufike mahali tujiulize tunatakaje maendeleo ya uwekezaji na mikataba mibovu? Hii nchi imekuwa kaputi kabisa kwa ajili ya mitaba mibovu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepewa mradi wa uwekezaji na TANZAMOB ambao wamepewa na STAMICO; yule mwekezaji ni tapeli wa kutupa, ameanza kuchimba madini kwa muda toka mwaka 2011 anasema hajapata faida. Tujiulize, kwa nini hajapata faida na kwa nini anaendelea kuchimba? Miradi yote unayoiona Tanzania haina time frame, anafanya mtu biashara kwa miaka yotote anayotaka yeye. Sasa je, utasemaje tunaenda katika ulimwengu wa viwanda, ulimwengu wa uwekezaji tukiwa katika mfumo mbovu? Aibu. Tujiulize kweli nchi hii tunataka kuikwamua? Haiwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelea National Housing, mwekezaji Kawe alinunua majengo ya Kawe na heka 300 kwa milioni sita, milioni sita Watanzania nawaambia. Kawe ameinunua kwa milioni sita akalipa milioni mbili na laki tano, hakufanya chochote leo ameambiwa ana share na National Housing. Meneja wa National Housing anahangaika kutafuta fund yule anachukua hela ya bure na mapato ya bure, tutafika? Kwa mfumo huu tutafika? Kwa nyumba za bei rahisi mtazipata wapi? Huwezi kuzipata Tanzania anatozwa mpaka tozo la vifaa vya kuingiza kutoka nje kwa ajili ya ujenzi wa nyumba halafu unasema zile nyumba za bei rahisi, Mtanzania wa kawaida hawezi kukaa katika nyumba ya National Housing kwa vile mmeweka mikataba mibovu ya kumfanya National Housing asiendelee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelewa na TANAPA. Kuna wawekezaji wako ndani ya Shirika la TANAPA ambao ni watu wa mahoteli, wake watu ni majambazi sugu ambao hawataki kulipa concession fee, halafu wanachokifanya ni kukimbilia mahakamani wakicheza na mahakama kuhakikisha TANAPA haipati tozo, mahakama iko chini ya nani? Matokeo yake sasa hivi tumeshashinda lakini bado wale watu hawataki kuona Waziri ambaye anafanya kazi wanasema tutamtoa kwa vile anatudhalilisha. Uchumi wa nchi umeshikiliwa na watu wachache ambao wamehakikisha nchi hii haiendi. Tunawajua, tunawafahamu na tunawafumbia macho.
Nchi hata kama mtafika mahali hapo kama hamsimamii sheria zetu, hamuangalii mikataba yetu nina imani kuwa hatutaweza kufika popote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelewa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (Tanzania Airport Authority); Tanzania tuna airport 58 amepewa airport nane tu; 50 zote zipo kwa watu wachache wanafanya shughuli zao huko, madini yanapotea huko, wanyama wanapotea huko na mali zinapotea huko ni kwa ajili ya mikataba mibovu. (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.