Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi hii na mimi niweze kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda huu niliopewa naomba nijikite zaidi katika mazingira na nitajikita katika mazingira hususan katika Mkoa wa Simiyu. Ni dhahiri kwamba athari za mabadiliko ya tabianchi zinaongeza uwezekano wa kaya kuendelea kuishi katika umasikini. Umasikini huu utaendelea kuongezeka kwa miaka ijayo, hususan kwa mwanamke ambaye ni mkuu wa kaya kama hatua mathubuti na endelevu za kukabiliana na athari za tabianchi hazitachukuliwa kwa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanamke wa Mkoa wa Simiyu amekuwa akikabiliana na njia mbalimbali katika kukabiliana na athari ya tabianchi. Mwanamke amekuwa akijishughulisha katika kilimo cha umwagiliaji ambacho ni kidogo na hakina tija. Nikiongelea Wilaya ya Busega, Kata za Kiloleni, Nyashimo, Kabita, Kalemela, kata hizi ziko kandokando ya Ziwa Victoria lakini mwanamke anatumia ndoo kumwagilia katika kilimo chake ambacho hakina tija. Niendelee kuiomba Serikali, itakapoanza kutekeleza mradi wa maji ya Ziwa Victoria, na ninaamini utekelezaji wa mradi huu uko chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, basi itenge maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji ili iweze kumsaidia mwanamke huyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiongelea Kata ya Gambasingu, Wilaya ya Itilima na Kata ya Mwashata, Jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, wanawake wanatumia ndoo kumwagilia maji kutoka Mto Simiyu ambapo kilimo hicho kinakuwa hakina tija. Niiombe basi Serikali kupitia hizi asilimia tano ama shilingi milioni 50 zikianza kutolewa kwa kila kijiji, zianze na Mkoa wa Simiyu ili wanawake waweze kukopesheka na kuweza kununua pampu ambazo zitawasaidia katika umwagiliaji na hivyo waweze kukabiliana na athari ya tabianchi, ikiwemo pia na Kata ya Mwamanimba iliyopo katika Jimbo la Meatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, njia nyingine wanazotumia wanawake kuweza kukabiliana na athari hizi ni kufanya biashara ndogo ndogo; lakini changamoto wanayoipata ni ukosefu wa mtaji pamoja na kujengewa uwezo. Halmashauri hutenga asilimia tano katika bajeti yake kwa ajili ya kuwawezesha wanawake, lakini fedha hizi zimekuwa hazitolewi, zinabaki kwenye makaratasi tu. Niombe basi kuwe na msukumo wa utekelezaji wa utoaji wa fedha hizi, hata kupitia vikao vya RCC iwe ajenda mojawapo ya kufuatilia utekelezaji wa asilimia tano kwa ajili ya akina mama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi lingine, wanawake…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante,