Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa hizi dakika tano ulizonipa, lakini pia nichukue nafasi hii kuipongeza sana Kamati. Kamati imetoa taarifa nzuri sana na imenikumbusha enzi hizo nikiwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Kamati kwa kweli taarifa yenu ni nzuri na mmetushauri vizuri sana Serikali. Sasa kwasababu ni dakika tano nilizopewa, niseme kwa kifupi haya yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la jinsi ambavyo Serikali ilishughulikia suala la magwangala hasa upande wetu wa mazingira kwa taasisi yetu ya NEMC. Tulichokihakikisha sisi kimefanyika ni kwamba NEMC walishiriki kutoa mwongozo, kwa maana ya kuhakikisha kwamba mahali ambapo yataondoshwa haya magwangala kuna mtaalam na kuhakikisha kwamba wanawapa masharti na vigezo vya kuzingatia kadri ya magwangala hayo yatakapohamishwa kutoka eneo fulani kwenda mahali fulani, na kuhakikisha kwamba kwa namna yoyote ile hakutakuwa na uharibifu wowote ule wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, limezungumzwa suala la ujenzi wa mradi huu wa climate change adaptation program.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema na kuliambia Bunge lako kwamba mradi huu tayari mkandarasi yupo kwa ajili ya miradi yote ya Ocean Road, Pangani, Kilimani pamoja na ya Kisiwa Panza, yote hii mkandarasi ni huyu isipokuwa kwa sasa hivi ndiyo yupo hapo Dar es Salaam pale Ocean Road ndiyo ameanza. Maeneo mengine haya yote ana mobilise resources ili kuweza kupeleka kwenye maeneo hayo ili miradi hii iweze kuanza. Kwa kifupi sana unaweza kuona kwamba huyu contractor anaitwa DEZO Contractor Limited na alianza toka mwezi wa kumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za kutekeleza miradi hii tunazo. Fedha za kutekeleza miradi hii ninayozungumza, mkandarasi yuko site na ataenda kujenga kuta zote zinazotakiwa, sehemu za kujenga mitaro na yenyewe tayari inajengwa kama maeneo yale ya Kigamboni kule kwa Mwalimu Nyerere, Buguruni, mitaro ile inaendelea kujenga; na sehemu zingine tayari tumeshatekeleza kwa mfano Rufiji tayari tumeshapanda mikoko iliyokuwa itakiwa zaidi ya hekta 792 tayari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Wabunge wote wa maeneo mengine ambayo mradi huu unajumuisha kama Pangani, Kilimani, Kisiwa Panza ambako tayari na kwenyewe mikoko tumekwisha kupanda wakae wakijua kwamba mkandarasi yupo na muda wowote ataanza kazi ya ujenzi mara moja. Kama nilivyosema mkandarasi yupo na fedha tunazo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusu suala la Mfuko wa Mazingira. Suala la Mfuko wa Mazingira, hali iliyopo mpaka sasa hivi ni kwamba tayari tumeshapeleka maombi yetu Hazina tena kwa ajili ya kupitisha zile tozo ambazo zinatakiwa zitozwe, lakini vile vile tayari Waziri ameshateua ile Bodi ya Wadhamini ya kusimamia mfuko huu na tayari kikao cha kwanza kimekaa. Kwa hiyo, tunachoomba tu ni kuendelea kuungwa mkono ili tuweze kutekeleza mambo makubwa ya kimazingira kama ambavyo Wabunge mlivyoyazungumza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitake kuwahakikishia kwamba kwa kweli tunajua tatizo la mabadiliko ya tabianchi na nchi hii ya Tanzania inavyosakamwa sasa hivi na mabadliko ya tabia nchi. Tunajua uharibifu wa mazingira unaoendelea, tunahitaji support ya Bunge hili ili tuweze kufanya kazi hiyo ya kuhakikisha kwamba tunayarejesha mazingira kwenye hali yake, tunayazuia mazingira kwenye uharibifu wake na mimi na Waziri wangu pamoja na watendaji wote wa Wizara hii hatuwezi kulala hadi pale mazingira ya Tanzania yatakapokuwa yamerekebishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Leah pale amezungumzia suala la mradi ule wa maji wa Ziwa Victoria ambao unakuja mpaka Jimboni kwangu na mpaka Meatu. Niseme kwamba mradi huo wa umwagiliaji ukweli ni kwamba katika dunia hii ya mabadiliko ya tabianchi, bila wakulima wetu kuwaelekeza katika miradi ya umwagiliaji, bila wakulima wetu kuwaelekeza katika matumizi ya mbegu zinazovumilia ukame na mbegu ambao zinakomaa kwa muda mfupi hatuwezi kufanikiwa katika mapambano haya ya kilimo. Nimhakikishie kwamba mradi huu unaotekelezwa ambao unasimamiwa na Wizara ya Maji na kuratibiwa na Ofisi ya Makamu ya Rais,….
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri.