Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana nadhani wasemaji wengi tumechukua mawazo yenu, suala ni umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya hiyo, nadhani kuna hivi viwanda vya mbolea cha Mtwara na cha Kilwa. Ukweli ni huu, tender ilifanyika, Ferrostaal ya Kilwa ikashinda tender. TPDC ikaanza kufanya kazi na kampuni iliyoshinda tender. Kampuni iliyoshindwa Helm ikaamua kufanya taratibu zingine kwenda kujenga kiwanda Mtwara, huo ndiyo ukweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali ya hayo yote sisi hatujatenga kampuni yoyote, niseme tu kwamba tulikaa kikao na Makamu wa Rais, nikapeleka wataalam wangu Mtwara, viwanda vyote vinapewa gesi, sitaki kwenda zaidi ya hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda cha Mkuranga Goodwill cha vigae, mitambo mabomba yamefika, yeye aliyekuwa anaomba gesi hajamaliza kujitayarisha na yenyewe ninaiachia hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye suala la umeme, Waheshimiwa ni kwamba umeme tukubaliane kwamba popote duniani ukitaka kuanza kiwanda sehemu zote duniani, ardhi inakuwepo, maji yanakuwepo, umeme unakuwepo na mambo ya usafirishaji. Tukiri kwamba saa zingine tunavutia watu wanajenga viwanda wakati hivyo vitu vyote vitatu havipo. Kwa hiyo, siyo sahihi kusimama na kuanza kusema Wizara hiyo na hiyo lakini wakati unaenda kujenga kiwanda hukuiuliza Wizara. Japokuwa tuna majukumu ya kupeleka umeme pale, hilo nalo lifahamike hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kama tunavyojenga vyumba watu wanachelewa kutoa viwanja, watu wengine wanaenda kujenga milimani, halafu wanataka mabomba ya maji yaende milimani, umeme uende milimani, kwa hiyo ndiyo hali kama hiyo. Tujengea viwanda kwa mpangilio, badala ya kulaumu kwamba Wizara zina usingizi, katika Wizara inaheshimika dunaini ni Wizara ya Nishati na Madini. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la umeme ni mtizamo naomba ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania tuache mtizamo kwamba dunia ya leo umeme utazalishwa na TANESCO peke yake, haiwezekani. Kwa sababu nikiwapa hapa bajeti yaani makisio ya umeme kati ya mwaka jana na mwaka 2020 tunahitaji dola bilioni 11.6. Kati ya mwaka 2021 na 2025 tunahitaji dola bilioni 5.9, haya mahesabu yatakuja kama Wizara imelala?
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu power per capital twende tunapiga hesabu sasa, power per capital sasa hivi ni unit 138 kwa mtu kwa mwaka. Wakati tutaingia kwenye kipato cha kati mwaka 2025 tukiwa watu milioni 70 na GDP per capital ikiwa 3000 inaamanisha GDP yetu lazima iwe bilioni 211, power per capital lazima iwe zaidi ya unit 500 lakini ni bora ikawa 1400. Kwa hiyo, ndugu zangu nataka kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge huku Wizara ya Nishati na Madini tunaenda kwa mahesabu kweli kweli. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine hatutazalisha tu umeme ndani, ndiyo maana sasa hivi tumemaliza transmission lines, Mheshimiwa Rais akipata muda itabidi azindue, tumeongeza umeme mara mbili unaotoka Iringa, Dodoma, Shinyanga ndiyo maana umeme haukatikikatiki sasa hivi. Transmission line ile imetoka 220kv kwenda 400kv. Unataka matayarisho gani zaidi ya hayo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu tunajenga transmission line kubwa vilevile, mmeona kutoa Singida, Arusha kwenda Kenya, lakini hii ya Kenya, Kenya watajenga kilovolti 400 kuunganisha na Ethiopia, Ethiopia itaunganisha na Egypt n kilovolti 500. Tumeshaanza hata mahesabu ya kununua umeme wa bei ndogo kutoka Ethiopia. Duniani kote kuna kitu kinaitwa power trade hata ingekuwa na Mtanzania anatuuzia umeme wa bei mbaya miaka michache inayokuja hatutanunua. Umeme wa Ethiopia bei ya kwanza bado tunajadiliana nayo ni 7.5 US cents per unit, hatujasaini kwa sababu tutatumia miundombinu inayopita Kenya inaitwa willing charges hatuwezi kusaini hiyo mpaka tujue Kenya watatu-charge kiasi gani kwa unit.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huo umeme wa Ethiopia unaweza kwenda mpaka huku Zambia watautumia na sisi tutawa-charge, halafu tunajenga transmission line ya kutoka Tanzania kwenda Zambia tuungane na power pool ya Kusini. Hakuna usingizi Wizara ya Nishati na Madini hamna kitu kama hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu upande wa Kaskazini huku Bukoba sasa hivi wanatumia umeme wa Uganda ambao ni megawati 18. Ndugu zangu wengine wa Sumbawanga wanatumia umeme wa Zambia megawati Nne, Kenya wanaleta megawati moja. Sasa tunachokifanya na hivi karibuni tutaenda kuzindua ni Rusumo megawati 70 kwa nchi tatu, lakini tunajenga transmission line ya kutoka Rusumu kuja Nyakanazi. Wakati huo huo tunajenga kutoka transmission line kubwa kutoka Mbeya kuingia Sumbawanga mpaka Nyakazani, sasa haya nilivyosema ni mabilioni. Kwa mfano, transmission line kwa miaka minne ninahitaji dola bilioni 3.7. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge, yote haya tunayafanya Wizara na Nishati na Madini tukiwa tunajua kwamba tunakuwa nchi ya kipato cha kati, lakini lazima uchumi ukue na uchumi kukua ni umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapinduzi ya uchumi (industrial revolution) mwaka 1746 yalichukua miaka 100 na yalihitaji vitu vitatu; yalikuwepo makaa ya mawe, chuma zamani ilikuwa ni viwanda vya pamba, baadaye ikaja revolution ya pili ndio ambayo ilienda kwenye mambo ya usafirishaji. Mapinduzi ya viwanda hayasimami, sasa hivi wakati sisi tunang‟ang‟ana na hivi viwanda vya chuma mapinduzi ya viwanda sasa hivi duniani ni non-technologies. Vitu ambavyo vina size ya unywele wako, ndiyo revolution iliyoko duniani sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hii ya kuweka solor panels inaanza kupitwa na wakati, majaribio yanafanyika Sahara watu wachukue umeme kutoka kwenye mchanga. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge nataka kuwathibitishia kwamba umeme wa uhakika utakuja na ndiyo maana napenda nirudie, ndiyo maana mimi nilikataa bei ya umeme kupanda kwa sababu huwezi ukajenga viwanda. Sasa niliyekataa bei ya umeme kupanda halafu eti nashtakiwa tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwa…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Profesa.