Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi kuchangia taarifa mbili za Kamati. Kipekee niwapongeze Wenyeviti wa Kamati hizi mbili, Wajumbe wa Kamati lakini kipekee Waheshimiwa Wabunge ambao mmeshiriki kuchangia hizi Kamati mbili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma sana taarifa hizi mbili, lakini nimesoma kipekee taarifa iliyohusu mahsusi suala la viwanda, biashara na uwekezaji. Ninawaunga mkono, nataka niwaambie pale ninapotofautiana na ninyi. Serikali haina mpango wa kutwaa kiwanda na kukiendesha, haijaandikwa mahali popote wala sijawahi kuelekezwa na mkuu wangu wa kazi au tajiri namba moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumewaambia wenye viwanda, vile viwanda vihakikishe vinafanya kazi, wasipofanya kazi tutawapa wengine waviendeshe. Ndugu yangu wa Tabora, kwetu kuna methali moja inasema asiyemhurumia chura anasema chura hafi kwa mpini ukimpiga. Nimekwenda kwa Ndugu Rajan mimi, Rajanialikufa nikamfuata mtoto wake wa Uingereza nikaongea naye, kiwanda cha nyuzi kitaanza. Ndugu Gulamali kila siku ananifuata ili kusudi turudishe Manonga. Igembe Nsabo wanakuja hapa kesho kutwa nifanye nini Mwijage? Kwa hiyo, huo ndiyo msimamo wa viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, msiwaoneshe Watanzania kwamba tuna hali mbaya, nimepewa dhamana hii Novemba, 2015 ngoja niwape taarifa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, TIC wamesajili viwanda 170, BRELA viwanda 180 nina taarifa. Mbali na taarifa ya Kamati na mimi nina taarifa yangu nimefanya nini na nitaiwasilisha. Unapozungumza EPZA viwanda 41, NDC viwanda saba na vitatu vikiwa ni vya dawa. Unapokuja SIDO wameratibu viwanda 1,843 mpaka sasa ninapozungumza nina viwanda 2,169; ndivyo hivyo viwanda. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niwaeleze Watanzania nimefurahishwa na jambo moja kwamba Watanzania tunawahamasisha watu wa nje tunawaacha watoto wa ndani, siwezi kufanya hivyo. Hata nilipokuja hapa saa nane nilikuwa nawahamasisha Watanzania, niwaeleze ndugu yangu Mavunde, kesho kutwa tunakwenda kuzindua kiwanda cha chaki chenye uwezo wa kuzalisha chaki hapa Dodoma, kimetengenezwa kwa gharama ya milioni 20 kitaweza kuzalisha na kiwanda kipo hapa.
Kwa hiyo, ningependa tuzungumze ukweli. Msiwatie hofu ushauri wote utazingatiwa msiwatie hofu Watanzania kwamba hatuendi, tunakwenda mbele.
TAARIFA...
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu ni Mjumbe wa Kamati yangu, taarifa uliyonipa naikubali na naipokea.
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu ni Mjumbe wa Kamati yangu, taarifa uliyonipa naikubali na naipokea. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, dakika zangu zilindwe, kuna kitu kinaitwa mis-conception...
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kinaitwa misconception.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Dkt. Mpango amewaeleza, Serikali haijengi viwanda ila Serikali inaweka mazingira ya kujenga viwanda. Mchuchuma na Liganga ametueleza, Mheshimiwa Ridhiwani amekuambia anakualika ukienda Chalinze usimame uangalie, Mkuranga umealikwa. Mheshimiwa Mchungaji Msigwa hizo nyanya unazolima mimi nina fursa ninaweza nikakupa kiwanda. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu niwaambie kitu kimoja Wabunge waelewe, unajua Wabunge mnajichanganya, mnasema Watanzania wazawa wawezeshwe, wapewe fursa msiagize wageni, lakini ninyi wazawa kuna mzawa kuliko Mbunge, unyanyuke wewe Mbunge. Asubuhi nimejibu swali kuhusu zile taulo za akina dada, niwaeleze kuna Waheshimiwa Wabunge wawili hapa tunahangaika kuleta teknolojia ya kutengeneza vitu, msiogope kuwa na utajiri ilimradi huo utajiri usiuibe. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge mjiandae kumiliki useme kiwanda hiki ni changu na hiki ni changu. Mheshimiwa hapa tumekubaliana alete proposal. Juzi nimeitisha semina hapa ya venture capital nikawaleta hapa, wanasema pesa wanazo. Kuna Wabunge walijitolea wakaja wakaangalia, waliposema dola bilioni kumi kumpa mwekezaji nikawaambia msiwadanganye Wabunge. Mtu akasimama akasema we have money mjitokeze. Hauwezi kulala kitandani ukapewa lift lazima uingie barabarani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie viwanda vilivyobinafsishwa, hali siyo mbaya hivyo, ila yeyote aliyepewa kiwanda kulingana na masharti viwanda vitatwaliwa. Ninayo ripoti ya viwanda kumi ambavyo vinakwenda kwa AG na viwanda vitatwaliwa, Lakini safari yetu ni miaka mitano, ndiyo naanza kazi sasa hivi mnaanza kusema. Hivi unategemea unaweza kujenga viwanda kwa shilingi bilioni 42. Kiwanda cha Mkuranga mnachosikia ni bilioni zaidi ya 80. Serikali haijengi viwanda.Mheshimiwa Mwenyekiti, dakika zangu zilindwe, kuna kitu kinaitwa mis-conception...
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kinaitwa misconception.
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge naomba utulivu!
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Dkt. Mpango amewaeleza, Serikali haijengi viwanda ila Serikali inaweka mazingira ya kujenga viwanda. Mchuchuma na Liganga ametueleza, Mheshimiwa Ridhiwani amekuambia anakualika ukienda Chalinze usimame uangalie, Mkuranga umealikwa. Mheshimiwa Mchungaji Msigwa hizo nyanya unazolima mimi nina fursa ninaweza nikakupa kiwanda. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu niwaambie kitu kimoja Wabunge waelewe, unajua Wabunge mnajichanganya, mnasema Watanzania wazawa wawezeshwe, wapewe fursa msiagize wageni, lakini ninyi wazawa kuna mzawa kuliko Mbunge, unyanyuke wewe Mbunge. Asubuhi nimejibu swali kuhusu zile taulo za akina dada, niwaeleze kuna Waheshimiwa Wabunge wawili hapa tunahangaika kuleta teknolojia ya kutengeneza vitu, msiogope kuwa na utajiri ilimradi huo utajiri usiuibe. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge mjiandae kumiliki useme kiwanda hiki ni changu na hiki ni changu. Mheshimiwa hapa tumekubaliana alete proposal. Juzi nimeitisha semina hapa ya venture capital nikawaleta hapa, wanasema pesa wanazo. Kuna Wabunge walijitolea wakaja wakaangalia, waliposema dola bilioni kumi kumpa mwekezaji nikawaambia msiwadanganye Wabunge. Mtu akasimama akasema we have money mjitokeze. Hauwezi kulala kitandani ukapewa lift lazima uingie barabarani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie viwanda vilivyobinafsishwa, hali siyo mbaya hivyo, ila yeyote aliyepewa kiwanda kulingana na masharti viwanda vitatwaliwa. Ninayo ripoti ya viwanda kumi ambavyo vinakwenda kwa AG na viwanda vitatwaliwa, Lakini safari yetu ni miaka mitano, ndiyo naanza kazi sasa hivi mnaanza kusema. Hivi unategemea unaweza kujenga viwanda kwa shilingi bilioni 42. Kiwanda cha Mkuranga mnachosikia ni bilioni zaidi ya 80. Serikali haijengi viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la EPZA. Tunalitambua suala la EPZA! EPZA inayoniuma ni Special Economic Zone ya Bagamoyo. Maamuzi yametolewa na Serikali namna gani wananchi wa Bagamoyo watakavyoweza kufidiwa. Liko suala la EPZA, Special Economic Zone ya Bunda, timu yangu imekwenda, nimshukuru Mjukuu wangu, wamekwenda Bunda, wamepewa ushirikiano, wale waliokula pesa za Serikali watakamatwa na watajuana na Mheshimiwa Mwigulu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe kitu kimoja Waheshimiwa Wabunge, viwanda tunavyojenga ni kwa ajili yetu, kamateni maeneo kwa ajili ya familia zenu. Mheshimiwa Simbachawene ametoa maelekezo namna gani katika Serikali ngazi za vijiji na mikoa mtakavyoweza kutunza maeneo na kuweza kuwapa vijana wenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la kilimo nusu. Katika viwanda vilivyotengeneza ninavyowaambia kuna Kiwanda cha TAMCO, tumeshakibadilisha kuwa kiwanda cha kuunga matrekta na ninavyozungumza sasa vifaa vya kutengeneza matrekta 340 vimeshafika Kibaha na tunalenga kutengeneza matrekta 2004 Kibaha kabla ya mwisho wa mwaka huu na yote nimepewa dhamana nitayagawa mimi. Sasa kama ulikuwa unalima na jembe, nitakupa trekta, ndiyo namna ya kuongeza tija katika kilimo. Kwa hiyo, viwanda ninavyovihesabu ni cha Urususi cha matrekta kiko TAMCO. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kipekee ambalo baadhi ya Wabunge mmezungumza ni viwanda vya dawa na dhamana hiyo iko chini ya Makamu wa Rais. Makamu wa Rais amenielekeza pamoja na Waziri wa Afya, tuandae wawekezaji juu ya kuwekeza kwenye viwanda tiba, ndiyo kazi ambayo tunawaita wawekezaji kutoka Misri, ndiyo kazi ambayo tunawaita wawekezaji kutoka Uturuki, China and the response is good. Kwa hiyo, Waheshimiwa msijione wanyonge Watanzania, ninyi Wabunge mkijiona wanyonge wananchi wenu watanyong‟onyea! Tanzania sasa tunajenga viwanda, msidhani kwamba hamuwezi na mjifunze kumiliki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuwashukuru watu wa Kigoma. Tunasaidiana na watu wa Kigoma kwenye kilimo cha michikichi na miwa, nichukue fursa hii pia wawekezaji wote waliochukua maeneo ya kulima miwa, kufikia mwezi wa nane atakayekuwa hakufika site nitampeleka kwa Mheshimiwa Lukuvi, tutamnyang‟anya eneo, ikiwemo Kibondo Sugar, ikiwemo Kigoma Sugar. Waheshimiwa kazi zinafanyika, lakini kama nilivyosema hii ni ripoti ya wenyewe na ripoti ya kwangu iko hapa, siku mtakapoiona mtacheka na kufurahi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie mambo mahsusi, suala la Urafiki. Ubinafsishaji wa Kiwanda cha Urafiki una masharti. Upande wangu kwa dhamana yangu, nilishazungumza na watu wa Foreign Affairs yule mwekezaji aondoke, aletwe mwingine kusudi awekeze kwa malengo. Ule ufisadi mnaozungumza ni historia na mimi nimeukuta, lakini mimi siyo expert wa kufukua makaburi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu viwanda vya kilimo, uvuvi na mifugo. Nakushukuru Mheshimiwa Nsanzugwanko, ndivyo Mpango wa Pili wa Miaka Mitano unavyosema. Ndiyo maana kuna mkakati mmoja wa mwaka jana niliou-launch mimi na Ndugu Mwigulu, unasema cotton to clothing, unasema leather and leather by products, unasema kuhusu maziwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbunge wa Njombe anajua, leo nimempa muhtasari wa Kikao cha SAGCOT ambapo ng‟ombe 3,000 wataletwa kupelekwa Njombe ili watoe maziwa, ili maziwa hayo yaweze kutosheleza viwanda vya maziwa vya ASAS na viwanda vya Njombe vya maziwa. Tunafanya kazi, lakini kama nilivyosema asiyehurumia chura, anasema hata ukimpiga kwa jiwe hawezi kufa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mikataba ya Viwanda vya Korosho, kwa kipekee nilikuwa nalishughulikia suala hili, lakini suala hili nakwenda kulimiliki na nitakufa navyo. Viwanda vya Korosho nitakufa navyo, naviperemba nikimaliza nampelekea Waziri wa Fedha ndiye mwenye dhamana. Viwanda vyote vilivyobinafsishwa mwenye navyo ni Treasurer Registrar, kwa hiyo, viwanda vyote tutavishughulikia. Hii kazi nirudie tena, siyo kazi ya mtu mmoja, tukishinda Taifa letu limeshinda na tukishinda tushinde wote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie kwa mara nyingine niwaeleze; Serikali yetu ya Tanzania katika Taarifa ya Kamati kwamba, Serikali ina matatizo na wawekezaji. Mimi ndiye receptionist, wawekezaji wote wanakuja kwangu kila siku, nimehamia Dodoma kila siku wanakuja hapa. Hakuna mwekezaji amekuja kwangu akashindwa kuhudumiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie pale wanapokosea, usijidanganye kwenda kwa tajiri namba moja au Makamu wa Rais au kwa Waziri Mkuu, kama unataka kuwaona wakubwa uje unione mimi. Mimi ndiyo nitakufanyia mpango ukamuone Mheshimiwa Rais, huwezi kutoka huko ukaenda kwa baba bila kupita kwa mwana, njooni hapa nitawafanyia mipango, huo ndiyo utaratibu. Kwa hiyo, Serikali hii ni friendly, inapenda wawekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru binti Katimba kwa sababu ya upatikanaji wa malighafi. Mheshimiwa Katimba ngoja nikwambie, nimepata mwekezaji, muulize dada yako wa Uvinza, tunakwenda kule Itamigaze na ndugu yako Mheshimiwa Zitto, tutapanda Migaze Kigoma, lakini Migaze ya leo haiwezi kuzidi ya kesho. Kuna kipindi kirefu, tutafanya kazi sisi ambayo ni manufaa kwa vijana wetu. Waheshimiwa Wabunge, watu wasikate tamaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru watu wa Kamati mmenipa changamoto, lakini…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, ahsante sana,