Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nihitimishe hoja hii muhimu sana katika historia ya maisha ya Tanzania yetu. Tunataka nchi yetu iwe nchi ya viwanda ifikapo 2025.
Ninawashukuru Waheshimiwa Wabunge mliochangia, tulikuwa na wachangiaji 37, kumi na sita wamechangia kwa maandishi na kwa maneno wamechangia Waheshimiwa Wabunge 21 pamoja na Mawaziri, ahsanteni sana kwa michango yenu. Kamati tunashukuru sana kwa hayo yote.
Waheshimiwa Wabunge, suala la kujenga viwanda katika Tanzania ni suala la kufa na kupona na ndiyo maana liko kwenye awamu hii ya Mpango wa Maendeleo. Tulianza kama Mbunge mmoja alivyosema kuweka mazingira. Tulitakiwa tuwe tumeshamaliza kuweka mazingira ya miundombinu halafu tuanze ku-industrialise lakini hatukuweza. Kwa hiyo, sasa tuna-industrialise wakati huo huo tunaweka mazingira. Kwa hiyo, ni jambo letu sisi wote ni jambo la kufa na kupona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningependa kusema ni jambo la coordination, Serikali inafanya kazi individualy mmoja-mmoja. Nishati na Madini yuko kwake, Kilimo yuko kwake, kila mtu yuko peke yake. Mimi nilitarajia maprofesa pamoja na madaktari, Serikali ina madaktari na maprofesa, mkutane wote, Wizara zote mkutane mtengeneze road map ambayo itatupeleka, lakini mnapofanya kazi kila mtu peke yake hatutafika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Profesa Waziri wa Nishati umeeleza vizuri sana juhudi ambazo tunataka kuleta umeme, lakini uko peke yako, hufanyi kazi na wenzako. Mheshimiwa Profesa Waziri wa Kilimo ni Daktari wa Kilimo yule na yeye yuko peke yake. Msipokutana tukatengeneza kitu kimoja hatutafika. Kamati tunadhani mkakati wa pamoja wa Serikali nzima unatakiwa ufanyike, vinginevyo hatufiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la sekta binafsi kuhamasishwa mmesema vizuri sana, Waziri wa Fedha amesema vizuri na baadhi ya Wabunge, huo mtazamo, pamoja na Waziri wa Viwanda hapa, mtazamo wa kwenda kwenye ujamaa hatuutaki. Sasa hivi we are not going back to ujamaa, tunataka sekta binafsi ijenge uchumi. Serikali inaweza kuwa na viwanda vya kimkakati vichache, lakini mnavyofikiria kutwaa viwanda na kuviendeleza, nashukuru Waziri wa Viwanda na Biashara amesema hapa, yeye ni coordinator ili sekta binafsi iweze kujenga viwanda pamoja na Serikali kwa namna ya pekee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pesa kutokupelekwa limesemwa sana. Waziri wa Fedha ameeleza vizuri pale, wanahangaika na kukusanya, lakini ni jambo ambalo tumelipata kwa wadau, tumelipata kwenye Mawizara ni tatizo letu sisi sote, ni lazima tulichukulie kwa upana wake kwamba, fedha lazima zipatikane na zipelekwe. Tunapopanga Bungeni humu, basi tupange bajeti ambayo ni realistic, tutaweza kupata fedha na kuzipeleka, lakini tunapopanga tu bajeti ambayo haina fedha tunakuwa kama tunawadanganya wananchi, siyo jambo zuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu limesemwa sana na wadau. Tunamuomba Mheshimiwa Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, pamoja na juhudi zote hizi lakini tatizo bado lipo. Ukienda kwenye kiwanda chochote utakuta wanasema umeme unakatika katika kweli na wengine mpaka wanafunga viwanda, wengine mitambo inaharibika, kwa hiyo, ni jambo lipo. Pamoja na mikakati ya kisayansi na nini, lakini umeme bado ni shida. Tukubaliane kwa kweli, pamoja tuende ili tufike mahali panapohitajika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo Wabunge wamesema ambalo nataka nili-echo tena, malighafi tutumie, tunapojenga viwanda tutumie malighafi ambazo zinagusa watu, kilimo, uvuvi na mifugo. Ukianzisha kiwanda cha tiles kama cha ndugu yangu kule unaweza ukawanavyo 200, lakini wananchi umaskini unaendelea. Kwa hiyo, kuna suala la maendeleo (growth ya uchumi), lakini kuna suala la economic development pia, maendeleo ni tofauti na kukua kwa uchumi, unaweza ukakuza uchumi, lakini wananchi bado wanahangaika.
Kwa hiyo, ni lazima tutumie hizi bidhaa, malighafi za Tanzania za kilimo, mifugo na uvuvi na zingine tuzijengee viwanda. Hii itatusaidia sana na Wabunge wengi wamesema na mimi naunga mkono jambo hilo.
Narudia tena kwa kusema ni lazima mwekezaji akija awe wa ndani au nje, ajisikie amepokelewa. Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mheshimiwa Mwijage, wawekezaji wengi bado wanalalamika, pamoja na kwamba upo vizuri, lakini wenzako sasa, mtu akienda ardhi kule anaweza akakimbia, akienda madini kule anaweza akakimbia, akienda kilimo anakimbia, wewe uko vizuri. Kwa hiyo, coordination ni muhimu, lazima m-coordinate mfanye vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ya kufanya biashara wadau wamelalamika sana. Kwa kweli ni jambo letu sisi sote na sisi Kamati hatukutoa hii ripoti kwa sababu ya kuipiga Serikali, hapana. Tumetoa hali halisi tu inavyoonekana huko kwa wadau ili tushughulikie jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, karibu namaliza, jambo kubwa la mazingira. Mazingira ni jambo kubwa kama alivyosema Mheshimiwa Waziri, uharibifu wa mazingira ni mkubwa kuliko tunavyofikiria. Tuna mpango wa kupanda miti lakini hautekelezeki. Tuliliomba Bunge mwaka jana uanzishwe mfuko na fedha za tozo zote ziingie kwenye mfuko. Tumeweka pendekezo, tumeweka Azimio la Bunge kwamba bajeti ijayo tozo zote za kimazingira ziingie kule na mfuko huu uwe na fedha ili tuweze kutunza mazingira, vinginevyo tutaimba sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Ziwa Victoria ni vizuri niurudie, unakamilika mwezi wa 12, lakini effect yake ni ndogo. Naishauri Serikali kama mnaweza kuanzisha mradi mwingine katika viunga vya Afrika Mashariki utakaoshughulikia zaidi mito hii mikubwa ambayo inaleta maji, tunaweza kulitunza ziwa letu vizuri zaidi, lakini uvuvi haramu ni tatizo kubwa sana. Serikali lazima mliangalie hili, Wizara ya Kilimo, wote tushirikiane ili tuweze kuondokana na jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya tabianchi ni jambo kubwa pia. Kuna Mheshimiwa Mbunge mmoja amesema, Tanzania ya mwaka 68 na Tanzania ya leo ni tofauti. Mito imekauka, maziwa yamekauka, vitu vingi vimekauka na sisi wote ni mashahidi. Kwa hiyo, ni lazima tulitazame jambo hili kwa namna ya tofauti na ninaiomba Serikali katika kutengeneza miradi na katika kuzungumza na wadau wa maendeleo ni lazima tupate fedha kwa ajili ya ku-curb jambo hili, tusipolitazama vizuri mambo yetu yataendelea kuwa mabaya zaidi. Nasema suala la mazingira ni mtambuka na lazima tushirkiane kama nilivyosema awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ni maazimio. Haya maazimio tuliyoyapita, naomba ni-echo yale aliyoyasema Mheshimiwa Nsanzugwanko na mimi wakati nawasilisha hapa nilisema. Maazimio haya ni maazimio muhimu sana, hatutaki yakabaki kwenye shelf za Bunge, hebu tutengeneze utaratibu wa kuyafuatilia kama Wabunge. Tukiunda Kamati Ndogo ya kuyafuatilia, tunajadiliana na Serikali maana hili ni jambo letu wote siyo kwamba tunapingana ni jambo letu wote, tusigombee fito. Tutengeneze Kamati ambayo itafuatilia na Serikali itakuwa inatupa mambo kwa uzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa nizungumzie viwanda ambavyo vimesemwa na Wabunge. Mbunge wa Mkuranga kasema ana viwanda sijui vingapi 56 na viwanda 11 jumla 67, pia Waziri anasema ana viwanda 1,149 sijui, kama namba nimeishika vizuri.
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Ni viwanda 1,169.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda 1,169.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme hivi Mheshimiwa Waziri, Kamati yangu haina taarifa kabisa. Interpretation yetu kama Kamati ni kwamba Waziri hushirikiani na sisi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kama kungekuwa na ushirikiano tungekuwa tuna habari, hata kufunguliwa kwa kiwanda cha Mkuranga au wapi, hata Mwenyekiti tu angeenda. Hata Mjumbe mmoja tu hizi habari tungekuwa nazo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge, ninatamuomba Mheshimiwa Rais labda amuongezee Naibu Waziri inawezekana ana shughuli nyingi sana ili tuweze kumpata Waziri kirahisi zaidi. Vinginevyo, Kamati tunafanya kazi peke yetu Mheshimiwa Waziri, sasa hii siyo sawa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa naomba Bunge lako lipokee Taarifa ya Kamati na kuwa maamuzi ya Bunge. Ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.