Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. SUSAN A.J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii ya kwanza ili niweze kuchangia hoja hizi tatu muhimu sana ambazo kimsingi zinahusiana na maisha ya Mtanzania. Kipekee nitajikita zaidi kwenye masuala ya elimu, lakini sitaacha kuzungumzia masuala ya UKIMWI, madawa ya kulevya pamoja na masuala ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianzia na masuala ya madawa ya kulevya; hapa kwenye Bunge lako Tukufu mwaka 2005 tulipitisha Sheria ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya na sheria ile ilianzisha Mamlaka ambayo pamoja na mambo mengine ni pamoja pia na kukamata (ku-arrest) pamoja na kushikilia mali zao. Hivi karibuni tunaona ni jinsi gani mamlaka hii inaingiliwa; Mkuu wa Mkoa anaamua tu kutaja majina ya watu bila kufuata utaratibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuliambiwa Mheshimiwa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa na majina hayo na vile vile tukaambiwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Kitwanga amepewa majina hayo. Ni kwa nini tume hiyo au mamlaka hiyo isishughulikie majina hayo ili tupate uhakika wa nani anatumia madawa ya kulevya. Ni kweli kwamba janga hilo ni kubwa sana, lakini lazima utafiti wa kina ufanyike, kwa sababu mtu na brand yake na kujijengea jina ni kazi kubwa lakini kulifuta ni jambo la haraka sana. Kwa hiyo, naomba utaratibu wa kisheria ufuatwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu. Mambo mengi yameongelewa, lakini niseme tu, ni wazi kwamba elimu ndio msingi wa Taifa lolote; hakuna Taifa duniani hapa lililoendelea bila kuwekeza kwenye elimu. Hata hivyo, kwa muda mrefu nchi hii imekuwa ikichezea elimu sijui kama ndio sera ya Chama cha Mapinduzi lakini kwa kweli inasikitisha sana. Amezungumza Mwenyekiti wa Kamati kwamba, Tanzania mfumo wetu wa elimu ni matatizo makubwa sana; hakuna nchi duniani yenye mifumo zaidi ya miwili katika elimu; Tanzania ndio nchi pekee yenye mifumo miwili ya elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani kuwe na shule za msingi ambazo medium of instruction (lugha ya kujifundishia na kujifunzia) ni Kiswahili wakati shule nyingine za level hiyo hiyo medium of instruction ni kiingereza. Pia tukiangalia tuna elimu za aina mbili; tuna elimu bure na elimu inayouzwa na matokeo tumeyaona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii shule iliyokuwa ya kwanza Tanzania Feza ambayo wanalipa takribani milioni tano wanafunzi wametoka na division one na division two; division one 56 na division two wanafunzi watano au sita tu, lakini shule ya mwisho haina division one, two wala three, ina divison four wachache na zero zaidi ya 100.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukiangalia unaona wazi kwamba tuna matatizo makubwa sana ya mfumo wetu wa elimu na ndio sababu nitakuja pia na mapendekezo ya kuona ni jinsi gani tutaboresha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa ni kutokana na fedha kutopelekwa kwa wakati na hata zinapopelekwa zinakuwa zimechelewa; na haya yanajitokeza zaidi kwenye miradi mikubwa; na matokeo yake ni nini! Tuna miradi mikubwa ya hospitali; Hospitali ya Bugando tulitegemea kwamba wataweza kusimika mashine kwa ajili ya uchunguzi wa saratani; tunatambua kuwa kanda ya ziwa ina population kubwa sana; lakini jambo hilo halijafanyika; leo watu kutoka kanda ya ziwa wanakuja ocean road ya Dar es salaam; wakati huo huo tumekuwa na utayari wa kujenga airport Chato ambayo iko kwenye kanda hiyo hiyo ya ziwa. Kwa hiyo ni lazima tuangalie priority zetu ziko wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua juhudi kubwa ambazo zimekuwa zikifanywa na Serikali kwenye maeneo mbalimbali, lakini juhudi hizo ni za watu binafsi, wamekuwa wabunifu. Kipekee nimsifie sana Profesa Mohamed Janabi, amejitahidi sana kwenye Hospitali ya Moyo ya Jakaya Kikwete. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na juhudi hizi binafsi bado Serikali haioni kuwa kuna haja ya kupeleka fedha nyingi. Leo Hospitali ya Moyo ya Jakaya Kikwete imepewa Shilingi milioni 500 tu kati ya Shilingi bilioni nne ambazo wanazihitaji; wakati tunajua kwamba huduma zikiboreshwa kwenye ile hospitali ni rahisi sana watu wetu kutibiwa ndani na kwa maana hiyo Serikali itaweza kupata fedha nyingi sana za ndani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ushauri wangu, nadhani labda ile hospitali ibadilishwe jina iitwe JPM, Rais aliye madarakani sasa badala ya Kikwete labda sasa fedha zitakuwa zinatoka kwa sababu atakuwa madarakani. Naamini labda alivyokuwa Kikwete iliwezekana, kwa hiyo nashauri kwamba labda tukibadili jina likawa la Rais itasaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzngumzia ni madeni ya Walimu, hili suala ni kubwa sana. Na-declare interest mimi ni Mwalimu. Katika kuboresha elimu jambo la kwanza la kuliangalia ni Walimu na si madarasa wala vitabu. Walimu wa Taifa hili wamedharauliwa kiasi cha kutosha, wamenyanyaswa kiasi cha kutosha. Haiwezekani leo Walimu wadai hata kama ni trilioni 1.06 au milioni 800; ni kwa nini hawalipwi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tuulizane, kada gani nyingine hapa Tanzania ambayo ina madeni makubwa kiasi hiki? Yaani leo Mwalimu anaweza kwenda kituoni asilipwe mshahara kwa zaidi ya mwezi mmoja; nani anayeweza kukubali jambo hilo? Kwa hiyo, upole wa Walimu usiendelee kuifanya Serikali iache kulipa madeni yao na kuwafanya kama watu wa mitaani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kubwa zaidi ni hili suala la uhakiki. Mimi sielewi definition yake kwa sababu haiwezekani Walimu waitwe kwenda kusimamia mitihani, wamalize kusimamia mitihani, leo ni takribani miaka miwili wanaambiwa wanafanyiwa uhakiki. Hivi una mhakiki mtu kabla ya kufanya kazi au baada ya kufanya kazi? Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo tunaona yanaleta mushkeli katika elimu yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze, na bahati mbaya sana Mheshimiwa Mwenyekiti wangu wa kamati, kwenye mapendekezo mwishoni kuna mengi hakuyasema lakini niseme; kuna suala la wanafunzi walioondolewa Chuo Kikuu cha Dodoma. Naamini kabisa kwamba kuondolewa kwa wanafunzi wale haikuwa bahati mbaya ilikuwa ni makusudi kwamba majengo yale sasa yawe wizara za Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanini nasema hivyo? Nasema hivyo kwasababu ukiangalia mwaka 2014 uliletwa Muswada wa Mrekebisho ya Sheria ya Bodi ya Mikopo hapa ili tuweze kuwaingiza wanafunzi ambao wataenda kusoma special education kwa ajili ya masomo ya sayansi. Leo hakuna Mbunge humu ndani ataniambia kwamba kwenye Jimbo lake hakuna shida ya walimu wa sayansi; na Mheshimiwa Jenista wakati huo Naibu Waziri wa Elimu alilihangaikia sana hili jambo, lakini leo wanafunzi wale wameondolewa, tunapewa sababu za ajabu ajabu, tunaambiwa walikuwa vilaza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapoambiwa jambo, wewe mwalimu unapoambiwa kuwa wewe ni kilaza; kilaza kwa wale wasiojua hii ni terminology, na watoto wa University of Dar es Salaam huko nyuma, ni watu ambao hawaelewi chochote yaani wajinga. Kwahiyo, unapowaambia walimu wajinga…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa
muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Umemaliza, ni ya pili hiyo. Ahsante sana.