Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia. Na mimi ni-declare interest kwanza ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kusema, kama Taifa tunakabiliwa na mambo matatu makubwa, nina imani sana na Serikali ya Awamu ya Tano, kwamba mambo haya matatu, ukiwa na collective work mambo haya tutayamaliza. Jambo la kwanza ni suala la dawa za kulevya, jambo la pili ni jambo la ushoga, jambo la tatu ni tatizo la elimu ya hovyo kwenye nchi yetu, haya mambo matatu yanaliumiza Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne, Mheshimiwa Rais Kikwete alisema anayo list ya wauza dawa za kulevya, naomba nieleweke Rais Kikwete alisema anayo list ya majina ya wauza dawa za kulevya. Mimi ningeomba kupitia Bunge hili Waziri wa Mambo ya Ndani amfuate Mzee Kikwete pale Msoga akamuombe ile list ili waweze kuungana na kazi ya Makonda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali, kama alivyosema Mheshimiwa Rais, vita ya madawa ya kulevya, na mimi naamini anachokifanya Mheshimiwa Makonda ana-collect taarifa, vita ya dawa za kulevya siyo vita ya Paul Makonda peke yake, ni vita ya Serikali dhidi ya cartel ya dawa za kulevya. Kwa hiyo, naamini hataachwa Makonda na vita hii kama alivyoachwa alivyoanza kuongelea suala la lesbians na ushoga, alibaki nayo peke yake, kwa hiyo naamini kwamba Serikali itamuunga mkono katika jitihada hii aliyoanza, he started somewhere, ninaamini watumiaji wataachiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kwenye issue ya dawa za kulevya, nadhani lazima tuelewe, kama nchi tunataka kupigana vita hii tupigane in it’s totality. Kwa sababu tunatunga sheria dhidi ya dawa za kulevya halafu tunaruhusu kuanzisha vituo vya kutibu watumiaji wa dawa za kulevya, you prohibit in the left hand side, unakataza kwa mkono wa kulia unaruhusu kwa mkono wa kushoto, mnaanzisha vita mnaita sober house. Mimi ingekuwa amri yangu ningefunga sober house na kila mtu anayekula unga akienda hospitali apimwe, akionekana anakula aanze kushughulikiwa yeye kutusaidia aliyemuuzia, distributor ni nani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu; nataka tuangalie hizi takwimu Waheshimiwa Wabunge humu ndani tumeongea sana, kwamba madai ya walimu, walimu wana matatizo. Tatizo la msingi la sekta ya elimu katika nchi yetu ni mfumo. Leo elimu yetu inasimamiwa na almost Wizara tano, TAMISEMI, kama Kamati ya Huduma madai ya walimu anayasema sana Mheshimiwa Mwalimu Bilago kwa sababu ni mwalimu, na dada yangu Mheshimiwa Susan na Wajumbe wengine, lakini hili liko chini ya TAMISEMI. Kwa hatua ya awali Bunge hili liazimie, linapokuja suala la elimu, Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Elimu waje mbele ya Kamati kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu matokeo ya mwaka huu asilimia 93 ya shule zilizofanya vizuri ni shule za private, government ni only seven percent. Lakini division one mpaka division three ni asilimia 28 tu ya wanafunzi, asilimia 72 ni division four na division zero. Hali ya vyuo vyetu vikuu tunasema kwamba tunatanua elimu ya msingi matokeo yake idadi ya watoto wanaofaulu ni kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu tumeweza kuwapa sponsorship au kuwapa mikopo watoto 25,000 tu kati ya karibu watoto 60,000 ambao walikuwa wamedahiliwa kwenda vyuo vikuu, kuna watoto 35,000 hawajapata fursa ya kwenda higher learning institution ni tatizo. Kamati imesema TCU badala ya kusimamia suala la ubora amebaki kuwa dalali wa vyuo vikuu. Nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, East Africa Community iliunda commission ya kupitia vyuo vikuu vinavyotoa elimu ya madaktari, vyuo vinne vimefungwa Tanzania kwa sababu quality ya elimu yake iko chini, this is a crisis! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hatutakuwa serious kwenye suala la elimu ya nchi hii hatuwezi kupiga hatua tunayotaka kupiga na mimi niwaombe Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Spika hapa alisema kuna hoja nilipeleka ya kutazama mfumo wa elimu, basi kwa kuanza tu tuazimie, Serikali ikautazame mfumo wa elimu wa nchi hii wote. Vyuo vikuu angalau by standard, wahadhiri wenye Ph.D wanaotakiwa kuwa kwenye vyuo vikuu, tulionao sasa hivi ni only 25 percent wakati standard ni angalau asilimia 60, lakini vyuo vyetu vina asilimia 25 tu ya wahadhiri wenye sifa ya kuweza kufundisha katika vyuo vikuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sometimes unajiuliza, nimeona takwimu za BEST, ukichukua takwimu za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia za mwaka 2012 mpaka 2016….
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, muda umeisha?
MWENYEKITI: Ndiyo, Ahsante Mheshimiwa Bashe.