Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nianze kwa kuzipongeza Kamati zote mbili kwa kazi nzuri walizofanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niongezee kwenye maelezo ya Naibu Waziri wa Afya kuhusu suala la viroba na vifungashio vya plastiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili liko chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais na kanuni tuliandika kwa sababu linapigwa marufuku kwa kanuni za chini ya Sheria ya Mazingira. Suala hili ni mtambuka, lina upande wa kodi, kwa maana ya Wizara ya Fedha, lina upande wa viwanda, Wizara ya Viwanda na Biashara, lina upande wa Wizara ya Afya kwa maana ya TFDA na Udhibiti wa Vyakula na Vinywaji, lakini pia upande wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachofanya sasa ni Wizara zote kuandika karatasi ya pamoja ambayo itawezesha hatua tutakazochukua ziweze kutekelezwa kwa msukumo na mtazamo wa pamoja na kutapatikana balance kati ya haja ya kuhakikisha kwamba mapato yanaendelea kupatikana kwa nchi, lakini tunalinda afya za watu wetu na mazingira ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala hili linataka tafakuri ya kina ya pamoja ndani ya Serikali na ndiyo kinachofanyika na taarifa rasmi ya mwisho ya maamuzi hayo italetwa ndani ya Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru kwa kunipa nafasi.