Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. EMMANUEL J. PAPIAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza, naunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayofanya na jinsi anavyosukuma gurudumu la maendeleo kwenye nchi yetu. Siku zilizopita kwenye mwaka 2010 - 2015 wenzetu wa Kambi ya Upinzani walikuwa wanasifia sana utendaji wa Kagame. Walikuwa wanasifia sana jinsi anavyochapa kazi na jinsi ambavyo amenyanyua Shirika la Ndege; na ATC yetu imekufa wakiwa wanalaani pamoja na Rais wetu Mstaafu JK. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nashangaa leo, Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amenunua ndege za kutosha, leo anapingwa. Jambo lingine ni kwamba, wakati wanasema anashauriwa na Kagame, wakati anajenga barabara Magufuli akiwa Waziri, swali ni
je, alikuwa anashauriwa na Kagame? Wakati anakamata meli zilizokuwa zinatuibia samaki kwenye bahari kuu, alikuwa anashauriwa na Kagame? Nawaomba, mkikumbuka kudanganya siku nyingine mkumbuke pia namna gani ya kujibu hoja zenu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie jambo dogo tu la Utawala Bora. Leo Jimboni kwangu Kiteto siyo salama sana. Siyo salama kwa sababu ya utawala bora tu, ambao tuna-miss watu ambao kwenye sehemu zao hawafanyi ipasavyo. Kiteto kulitokea mauaji na sasa baada ya Waziri Mkuu kutoka juzi tu miezi miwili wameshakufa watu wawili. Mashamba yameshachomwa zaidi ya thelathini. Tuna viongozi; tuna Mkoa, tuna Wilaya, tuna OCD tuna Mahakama na tuna Ofisi ya DC. Kwa nini vitendo hivi vinaendelea?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niambiwe kwa nini vitendo hivi vinaendelea na Serikali haijachukua hatua? Suala hili ni uzembe wa Watendaji wetu. Excuse ndiyo nyingi. Unaambiwa wamekamamatwa ugoni, wameshikana wapi, lakina umma uliteketea. Siku za hivi karibuni, hapa Jimbo la Kibajaji waliuawa wananchi watatu. Kile kijiji watu walitawanywa, walikamatwa, waliwekwa ndani na Serikali ilionesha jitihada zake. Kwa nini Kiteto hizi jitihada hazifanyiki ili mauaji yaweze kukoma? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba, Kiteto kuna watu wanafikiri kwamba ile amani ilitengenezwa tu. Hata wakati mauaji yanaendelea, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilikuwepo, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ilikuwepo, Watendaji wote wa Serikali walikuwepo. Leo wanatumia camouflage kwamba
wametengeneza. Wakati ule Mbunge alikuwa anaunga mkono hiyo hoja, DC aliyekuwepo alikuwa anaunga mkono, ofisi nzima, ndiyo maana umma uliteketea. Leo amani ipo kwa sababu tumefanya changes za utawala wa pale. Kila anaponyanyuka, nipo. Leo nimetengenezewa zengwe, nashughulikiwa. Nami watakaoshughulikiwa kukamatwa au kuwekwa ndani yawezekana nami nimo. Mimi nitakwenda kama Mandella. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukihisi kwamba naweza kudanganya na kusema uongo, siyo sehemu. Ukihisi kwamba naweza kuulinda uovu, siyo sehemu! Kiteto chama pekee, Kamati ya Siasa ya Wilaya ndiyo iliyookoa na kulaani vitendo viovu na Serikali ilikuwepo. Waziri Mkuu aliunda Tume; tunaomba ile ripoti itoke. Ile ripoti ina mambo mengi ndani yake. Ile ripoti itoke kwa sababu gharama ya Serikali imetumika, lakini kumefanyika heavy investigation juu ya matukio yaliyosababisha ile hali kuwa pale. Inaonesha vitendo vingi ambavyo vimefanywa na baadhi ya Watendaji mle ndani katika ile ripoti. Inaonesha involvement ya wale wanasiasa waliofanya hayo mambo pale ili itusaidie way forward tujue namna gani ya kukabiliana na matatizo yaliyoko pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, Kiteto wanasema imevamiwa sana. Leo wanafukuza watu kule, amani inaanza kupungua. Mtu amekaa miaka 20 au 15, maisha yake yako kule, hajui kwingine kwa kwenda, leo anaambiwa aondoke, anakwenda wapi? Wanasema ni
wavamizi, lakini wanasahau kwamba leo wale tunaowafukuza kule; leo Wilaya yangu nusu ya wafugaji wako Kilindi kwa Mheshimiwa Omari Kigua, naye awafukuze?
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunapozungumza, Kata yangu ya Dosidosi inayopakana na Kongwa, robo tatu ya wakulima wake wanalima Kongwa wakati ni wananchi wa Kiteto. Leo tuwafukuze? Wana zaidi ya miaka 30. Ukikaa unaulizwa, “ehee, leteni document ya shamba; hili shamba lako ulilipata lini?” Mtu ana miaka 30, ameoa, ana wajukuu analima Kongwa; ni mwananchi wa Dosidosi Wilaya ya Kiteto. Leo tufukuze watu kwa miaka 20 waliyokaa pale; kisa ni nini? Kwa sababu kuna mazingira ya rushwa, kwa sababu kuna ukabila. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo naomba mkubaliane nami, Bunge hili ikitokea kafa mtu Kiteto, namba msimame tuahirishe Bunge tuendelee na mchakato. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tulishakutana na vitu vigumu sana kwenye yale mazingira. Ukiona mgogoro hauishi, jua kuna watu wanachochoea huo mgogoro. Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante.