Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi hii. Mimi najiuliza kidogo nirudi kwenye Katiba Ibara ya 63 hiyo aliyoinukuu Msemaji aliyemaliza kuongea, maneno ya kusimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano kazi ya Bunge. Sasa najiuliza ili umsimamie mtu na kumshauri lazima huyo mtu awe kwanza anakubali kushaurika, awe anakubali kusimamiwa. Kusimamiwa unaweza ukalazimisha lazimisha vyovyote, lakini habari ya kushauri ni je, huyu anashaurika? Maana kama hashauriki utapata shida sana na huyo unayetaka kumsimamia. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tujiulize je, Serikali yetu inashaurika? Kama haishauriki tunafanya kazi gani Wabunge katika Bunge hili? Hakuna kwenye Katiba hii sehemu iliposemwa ukiwa na chama chako ni tawala wewe ambae ni Mbunge wa Chama Tawala huruhusiwi kuisimamia Serikali yako. Nawaombeni Wabunge tufanye kazi yetu ya kuisimamia Serikali na kuishauri bila kujali itikadi zetu, vinginenvyo hatu-play role yetu kama Wabunge. Nilikuwa nawakumbusha hicho kipengele. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, niende sasa kwenye bajeti na hali ya uchumi. Bajeti yetu ya maendeleo imetekelezwa kwa asilimia 34. Hivi hili linahitaji kuwa wa chama gani na chama gani? Asilimia 34 utekelezaji na asilimia 66 haijatekelezwa kwa nini tusiisimamie Serikali? Siamini kwamba hii Serikali inazo hizi fedha halafu ina roho mbaya haikuzitoa, basi tuisimamie ipate fedha na tunapotoa ushauri wa namna ya kupata fedha, vyanzo mbalimbali vya kupata fedha Serikali itusikilize, sasa isipotusikiliza halafu baadae inakwama inakosa hela.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa donors niliwahi kuongea mwaka jana nakumbuka, donors wetu kabla ya kuleta kwenye bajeti kuu huwa tunaweka ni mkataba gani tunafunga na donors kwamba hawata default ili fedha yote tunayoipata kwenye bajeti iweze kutoka. Tunapanga bajeti kubwa halafu baadae hatupati zile fedha na tunashindwa kuitekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunashindwa kuitekeleza ni kwa nini tupange nyingine kubwa zaidi, tusibaki na bajeti ile ya mwaka jana na tukaweka vipaumbele vyetu ndani ya ile bajeti ya mwaka jana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu haiingii akilini wewe ulitenga shilingi trilioni 29 halafu ikashindikana ukapanga shilingi trilioni 32, ni muujiza gani utakaofanyika tupate hizo fedha? Maana yake bajeti kama ni tegemezi inategemea wafadhili hatutafanya miujiza hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la kilimo. Suala la kilimo tumejipanga kwamba tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda, bila kuimarisha sekta ya kilimo hivi viwanda vitatoka wapi? Malighafi ya viwanda hivyo itatoka wapi? Sekta kubwa kabisa ambayo inaajiri watu wengi ambao wangeweza kumaliza umaskini katika nchi hii lakini ndiyo Wizara inayopewa fedha kidogo kabisa katika nchi hii Wizara ya Kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana pembejeo tulipata wakati mgumu wananchi wanataka kutumaliza, mifuko 30 tunapeleka Kijiji kimoja nani apate mtoto wa Katibu Kata au mtoto wa nani? Mifuko 30 hivi wanaobaki wanakuwa ni wananchi hawatakiwi kulima katika nchi hii?
Kama hawatakiwi kulima maana yake hawatainua uchumi wao. Kuna Mheshimiwa amezungumzia habari ya pembejeo, kilimo bila pembejeo ni sawa na kuvaa nguo ambayo haikufuliwa, wewe unaona uko bomba tu unatembea kumbe hakuna kitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo bila pembejeo unategema tuzalishe na wananchi wanatumia jembe la mkono, hili jembe la mkono maana yake wanalima kidogo wanatarajia kuvuna sana katika kidogo wanachoweza kulima. Sasa analima kidogo halafu hana pembejeo kwa hiyo hawezi kuvuna miaka nenda rudi umaskini unajirudia rudia, tunazidi kuwa na watu maskini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati fulani huwa najiuliza hawa maskini wanatengenezwa ili wawe, maana yake mtu maskini kupiga kura ni lazima aelezwe namna ya kupiga. Ukiwa maskini utaambiwa tu fanya hiki, sawa, fanya na kile sawa. Kwa nini tunakubali kundi kubwa la Watanzania ambao ni wakulima waendelee kuwa ni maskini? Pembejeo haziwezi kupatikana kwa wakati kwa nini? Na pembejeo zipo humu nchini, utakuta mbolea… (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimefika kwangu kule Kakonko mwezi Disemba mbolea inakuja na mbegu inakuja tulishalima siku nyingi na tulishapanda ndiyo mbegu zinakuja. Hivi pembejeo ikija mapema ninyi mnapata hasara gani? Wakulima wakapata pembejeo mwezi wa sita, mwezi wa saba akakaa mbegu iko pale na mbolea ipo ili ajiandae kulima msimu unapoanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimewahi kuzungumza mwaka jana kwamba kuna siku tutaleta mbolea ya kuvunia sijui tutaipata wapi. Unaleta mazao karibu yanakoma kabisa wewe ndiyo unaleta mbolea, inanipa wakati mgumu sana. Wakulima hawa tuwahurumie walime kidogo, wavune sana waondoe umaskini ili wawe na uwezo wa kufikiri vizuri hata wakati wa kupiga kura. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee suala la elimu. Upande wa elimu tumetoka kwenye semina ya TWAWEZA, hali ya elimu ni mbaya. Wanafunzi wa darasa la saba wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu ni asilimia 79 “K” tatu zile. Sasa walipewa mtihani wa darasa la pili
wakashinda kwa asilimia 79, ndugu zangu hali ya elimu ni mbaya. Walimu wana malalamiko rundo, walimu wanaidai Serikali shilingi trilioni moja, hawajalipwa na hakuna anayefikiria kuwalipa na kila wanapofikiria wafurukute ili waweze kulipwa ni vitisho vya kufanyiwa hili na lile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeongea na mwalimu mmoja ananiambia mwalimu wakati wa mitihani siku hizi kama mock na nini, hatusimamii kwa kuogopa kufelisha tunawaacha, tunakaa nje waoneshane mle ndani ili pass mark iwe ya juu Mwalimu Mkuu asihamishwe shule hiyo au
kuvuliwa madaraka, hayo ndiyo maelezo wanayoeleza shuleni. Wanachofanya tunasimamia nje kuangalia je, kuna pikipiki inakuja au gari la Afisa yeyote, tukiona ni shwari mle ndani wanaendelea kuoneshana na pass mark zinapanda, hiyo ndiyo elimu ya Tanzania tulipofika. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, halafu tunasema, HakiElimu wamefanya utafiti juzi juu ya elimu bure, wakakuta elimu bure haijatekelezwa kikamilifu, taarifa waliyoitoa front page ya gazeti la Serikali likasema elimu bure imetekelezwa kwa asilimia 100. Hao waandishi wa habari wangekuwa wakati wa Mheshimiwa Nape Nnauye nadhani wangewajibika tu. Hivi asilimia 100 kweli ipo asilimia 100 na mwandishi yule yuko vizuri tu anamfurahisha nani.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii elimu ni mali yetu, tukiongeza wajinga hapa nchini iko siku wajinga watakaa waungane wachague mjinga mwenzao awe Rais wa nchi, tufike mahali tukatae hili, tukatae kabisa, kwamba tunataka elimu iliyo bora na sio bora elimu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulishakubaliana kwenye Kamati yetu, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwamba iundwe Tume ya kuchunguza elimu in totality, hali ya elimu ni mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hussein Bashe aliwahi kutoa hoja binafsi ya kuundwa kwa Tume, yaliyompata sijui ndiyo maana yuko kwenye orodha ile ya watu 11, hata sijui! Lakini hali ya elimu tunakwenda kule ambako Marekani walipofanya utafiti waliambiwa a nation at risk, its where we are going in this country. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.