Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuweza kunipatia fursa hii nami niweze kuchangia kwenye hotuba ya Waziri Mkuu. Naomba Waheshimiwa Wabunge kama tunatambua ni nini wananchi wametutuma kufanya kwenye Bunge hili Tukufu, basi tuwatendee haki kwa kufanya yale ambayo wametutuma kufanya na kutokujitoa ufahamu na kufanya kinyume na ambavyo tumetumwa na wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hotuba ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni na ninaomba Waheshimiwa Wabunge msome hotuba zote pamoja na kwamba mtakuwa mnayo mengine kichwani, lakini hotuba ya Upinzani kwa kweli imeeleza mengi na mazuri kwa Taifa letu, tuweze kuishauri vema Serikali ili tuweze kusonga mbele kama nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 nilisema kabisa wakati wa bajeti imepitishwa na niliandika kwenye mtandao wa Bunge, nikasema hii bajeti ikitekelezwa hata kwa asilimia
70 tu, nikatwe kichwa changu. Mbunge mmoja, ndugu yangu Mheshimiwa Chegeni akaingia inbox akaniambia unamaanisha nini? Sasa napenda nimwambie nilichokimaanisha ndiyo tunachokiona leo, kwamba mpaka leo bajeti ya maendeleo hata asilimia 40 hatujafika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri kwamba kuliko kuja na bajeti ambazo hazina uhalisia, kama mpaka leo hatujafika asilimia 40, ile bajeti ya mwaka jana, tuchukue nusu yake ndiyo tuilete. Tulete bajeti ambazo zinatekelezeka. Tusiandike matumaini kwenye makaratasi mwisho wa siku hata asilimia 50 tu hamfikishi. Tuwe na uhalisia ili hata unapokuwa umeelezwa kwamba mathalan Mkoa wa Mara Jimbo la Tarime Mjini kwenye maendeleo kwa mwaka wa
fedha 2017/2018 tutaleta shilingi bilioni moja, basi na hiyo shilingi bilioni moja tuweze kuitekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ningezungumzia tuliondoa duty free kwa majeshi kwa maana Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Jeshi la Polisi, Askari wa Uhamiaji, Askari wa Majini na Magereza. Cha ajabu mpaka leo kumekuwa na double standard. Kuna wengine wameshalipwa mara mbili, kwa maana ya kila mwezi laki, laki; wameshalipwa shilingi laki sita. Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Askari Polisi, lakini Askari wa Uhamiaji, Majini na Magereza mpaka leo hawajalipwa. Ndugu zangu, tunataka kujua ni kwa nini kunakuwa na double standard?
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba kabisa Mheshimiwa Waziri Mkuu awaangalie ndugu zetu Magereza, wamekuwa wakionewa sana. Unakuta Askari Magereza ana degree lakini bado analipwa mshahara kama yule askari wa kidato cha nne. Leo mnawalipa hawa wengine, lakini hawa Askari Magereza niliowatja mpaka leo hamjawalipa. Wale watu ni muhimu sana na ikizingatiwa kuna watu mnawapeleka kwa kesi za kubambikwa kule Magereza. Hawa watu wakiamua kugoma, wale watu waliopo magerezani kule kutakuwa hakukaliki. Kwanza mngekuwa mnatumia busara zaidi, mngewalipa wale kabla hata hamjawalipa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Naomba mzingatie hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna madeni wanadai ya mwaka 2012/2013; 2013/2014 mpaka leo hawajalipwa. Leo mfungwa akitoroka, hawa ndugu zetu wanapewa adhabu kutokwenda masomoni, wanapewa adhabu ya kukatwa fedha, maisha wanayoishi ni duni na kipato chao ni duni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu na Waziri husika tunaomba hawa ndugu zetu muazingatie na wenyewe waweze kupata hiyo package ambayo mliiondoa ya duty free nao waweze kupata stahiki zao kama mnavyowapa Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa
Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Waziri Mkuu ametanabaisha kwamba wamejitahidi sana katika kuwawezesha wananchi, lakini ukisoma ameainisha kwamba kuna shilingi bilioni moja sijui pointi ngapi wamewapa vijana kwa mfuko wa vijana na shilingi bilioni 4.6 kupitia
Halmashauri, kwamba ndiyo hapo wamewezesha wananchi. Hatuko serious na Serikali hampo serious. Mlituambia mmetenga milioni 50 kwa kila kijiji au mtaa, mpaka leo mtuambie mmetekeleza vipi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Waziri Mkuu akija akasema kwamba Halmashauri zimejitahidi kupeleka 4.6 billion kuwezesha wananchi ilhali mkijua kuna Halmashauri nyingine hazina kipato cha kutosha, mathalan Halmashauri ya Mji wa Tarime, tumejitahidi, hapo zamani walikuwa hata
hawatoi hela. Kwa mwaka huu, tumejitahidi tumetoa ten million. Ten million only; leo mnasema tunaweza kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali itekeleze ile ahadi yao ya shilingi milioni 50 kila mtaa na kijiji; tumehamasisha wananchi wameunda vikundi mbalimbali na SACCOS tunazihitaji hizo shilingi milioni 50. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye elimu. Mheshimiwa Waziri Mkuu, ndugu yangu amesema kabisa tumejitahidi kutoa elimu bure na vitu kama hivyo. Ni dhahiri baada ya kuja hii elimu bure sijui, wakasema kwamba usipopeleka motto, unafungwa; kweli tumeandikisha watoto wengi sana mashuleni, lakini hatuangalii idadi. Tunatakiwa tuangalie quality ya ile elimu ambayo tunaitoa. Leo mmesajili wanafunzi wengi, lakini walimu wanadai madeni mengi na
hamjawapa mazingira mazuri ya kuwafanya wafundishe watoto wetu waweze kuelewa, hawana motisha yoyote ile, leo mnategemea kutakuwa na ufaulu mzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmesema mmerekebisha madawati. Sawa, madawati kwanza kuna sehemu nyingine bado hayajatosheleza, madarasa hayatoshi. Wananchi wanajenga, Serikali inashindwa kwenda kuezeka, vitabu hamna pamoja na kwamba TWAWEZA jana wamesema ratio ni moja kwa tatu, lakini mimi kwangu darasa la kwanza na la pili ni moja kwa tano; darasa la tatu mpaka la saba, kitabu kimoja; wanafunzi 50 mpaka wanafunzi 100. Hapo tunategemea elimu bure itatoka wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwe serious, kama tunataka tutoe elimu ambayo ni nzuri kwa wanafunzi wetu, elimu bora, tuwekeze na walimu wawe na motisha, wapewe fedha stahiki, walipwe madeni yao na wawe na mazingira mazuri ya kufundishia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee afya. Hospitali ya Mji wa Tarime mmeandika kwamba bado ni Hospitali ya Wilaya ya Tarime, lakini mnaleta OC na basket fund ambazo zinatumika idadi ya wananchi wa Mji wa Tarime, wakati kiuhalisia wanahudumia wananchi wa Wilaya nzima ya
Tarime, watumishi mmepunguza idadi wakati wanahudumia wananchi wa Wilaya nzima ya Tarime, wengine wanatoka Rorya na wengine Serengeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwepo na vigezo stahiki. Kama mnaona ni vyema hospitali ile iwe ya Wilaya, basi tunaomba OC na basket funds zije kwa idadi ya wananchi wa Wilaya ya Tarime na siyo idadi ya wananchi wa Mji wa Tarime. Mnawapa kazi kubwa watumishi, unakuta
daktari anafanya masaa zaidi ya 30 wakati alitakiwa awe kazini kwa saa nane tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye maji. Kuna mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria ambao usanifu ulishafanyika na Benki ya Maendeleo ya Ufaransa wapo tayari ku-sponsor huo mradi ambao unaanzia Shirati, Ingili Juu, Utegi, Tarime mpaka Sirari. Kuanzia mwaka 2011 watu
wamefanya design mpaka leo haujatekelezwa. Napenda kujua ili kutatua tatizo la maji Tarime, ni lini huu mradi utaanza kufanya kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, fidia ya ardhi ya wananchi ambao Jeshi la Wananchi wa Tanzania wamechukua. Nimekuwa nikiimba sana hapa Bungeni na Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba unisikilize katika hili.
Mheshimiwa Mama Ritta Kabati mwache Waziri Mkuu anisikilize, maana nimekuwa nikiimba hii kuanzia mwaka 2007. Jeshi la Wananchi wa Tanzania limechukua maeneo ya wananchi wa Nyandoto, Nyamisangula na Nkende mpaka leo hawajalipwa. (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji). MWENYEKITI: Ahsante,