Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba yake nzuri pamoja na Mheshimiwa Jenista Mhagama na Mheshimiwa Antony Mavunde kwa kazi nzuri wanayofanya katika shughuli zao za kumsaidia Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Magufuli pamoja na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa kwa kazi nzuri mnayofanya. Ni mwaka mmoja tu tangu mmeingia madarakani lakini mambo mnayofanya ni mazuri sana, uchumi wa nchi hii umeendelea kuwa mzuri hadi sasa hivi viashiria vyote vya uchumi vinaonekana kwamba tunafanya vizuri sana kwenye uchumi. Pato la Taifa limeendelea kukua hadi sasa hivi linaendelea kukua kwa asilimia saba na mmeweza kuu-contain mfumuko wa bei ukaendelea kukaa kwenye tarakimu moja. Vilevile ni furaha ilioje niliposikia kwamba Tanzania iko kati ya nchi sita the best in Africa ambao uchumi wao unakuwa kwa kiasi
kikubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo mengi ya kujivunia, tumeambiwa TRA sasa hivi makusanyo yameongezeka kutoka kwenye shilingi bilioni 850 mpaka kwenye shilingi trilioni 1.2 ndiyo maana mmeweza kuyafanya mambo makubwa kama kununua ndege. Anayependa apende, asiyetaka
asitake lakini makubwa yanafanyika ndani ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Mmeweza kuwa mnapeleka shilingi bilioni 18.77 kwenye shule kwa ajili ya elimu bure kila mwezi, hongereni sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba yake Mheshimiwa Waziri Mkuu amezungumzia kwamba mabenki yako salama, mitaji na ukwasi upo wa kutosha. Hapa nina wasiwasi kidogo kwa sababu tukienda kule chini, tukienda mijini na vijijini tunaona kwamba mabenki ya biashara
yamepunguza kutoa mikopo. Tunahamasisha wajasiriamali wengi wajitokeze wafanye shughuli mbalimbali, wafanye shughuli za kilimo, biashara ndogo ndogo, tunahamasisha wananchi waanzishe viwanda vidogo na vikubwa, hivi kama mabenki hayatoi mikopo hawa mitaji watapata wapi? Niombe Mheshimiwa Waziri Mkuu atusaidie ili Serikali sasa iweke mpango wa makusudi wa kuziwezesha hizi benki ili zianze kutoa mikopo kama walivyokuwa wanatoa kwa ajili ya wajasiriamali wadogo wadogo waliopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitajikita kwenye suala la kahawa. Kahawa ni zao la muhimu sana katika nchi yetu ya Tanzania, lakini lina umuhimu wa pekee kwa sababu tunaliuza nje linatuletea fedha za kigeni. Bei ya kahawa imeendelea kuwa chini kiasi ambacho inakatisha tamaa na ukilinganisha bei ya kahawa ya Tanzania na nchi jirani ya Uganda unakuta bei ya kahawa ya Uganda iko juu pamoja na kwamba nchi hizi zimepakana, ndiyo kitu kinachoshawishi watu wauze kahawa ya magendo kuitoa Tanzania kuipeleka Uganda. Bei ya kahawa kuwa chini ni kwa sababu bei ya kahawa ya Tanzania imegubikwa na tozo nyingi, ada nyingi, kodi nyingi. Wataalam wanasema hizi kodi na tozo zinafikia hadi 26. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano, kuna kodi na tozo za zimamoto, OSHA, land rent, crop cess pamoja na kwamba sheria inasema crop cess inaweza kuwa kati ya asilimia tatu mpaka tano, sisi halmashauri zinatoza maximum, five percent. Kuna income tax, cooperate tax, VAT kwenye inputs zote zinazoingaia kwenye kahawa, research cess, Coffee Development Fund ambapo hela zinakatwa kwenye kila kilo, lakini sijawahi kuona huu mfuko unakwenda kumuendeleza au kuendeleza kilimo cha kahawa. Kuna labour charge, service levy, property tax, coffee bags duties, coffee industry licence et cetera mpaka zinafika 26.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tozo hizi ziko kwenye ngazi mbalimbali za uzalishaji pamoja na pale wanapouza nje. Ukienda pale mkulima anapouza kahawa kwenye chama cha msingi, kwenye chama kikuu cha ushirika, kule kwenye mnada Moshi ambapo wana-export kahawa kote kuna tozo kila mahali, lakini mzigo mzima anaubeba mkulima. Tozo hizi ndiyo zinasababisha bei ya kahawa inakuwa chini sana. Kwa msimu huu Mheshimiwa Waziri Mkuu, bei ya kahawa kwa Mkoa wa Kagera ni shilingi1,300, mtu anatunza ule mbuni kwa miezi tisa anapalilia, anakatia na kadhalika lakini anakuja kuishia kupata kati ya shilingi 1,100 na shilingi 1,300.
Mheshimiwa Mwenyekti, tukijilinganisha na nchi jirani ambazo ni washindani wetu katika hili zao la kahawa kama Ethiopia wao wanakata 0.04% kama exchange rate sale price, Uganda wanakatwa 1% export levy, Kenya wanakata 3% tu kwa ajili ya cess, lakini Tanzania tuna different cess’s, licence fees, taxes na tozo mbalimbali zinazofikia zaidi ya 26 na kuifanya hiyo bei iwe chini sana na kuwafanya wakulima wa
kahawa wakate tamaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu amefanya mambo mazuri sana kwenye korosho, tumemuona. Ameweza kuifanya bei ya korosho ikapanda kutoka kwenye kilo moja shilingi 1,200 mpaka shilingi 3,800. Tumuombe chondechonde, mimi kama mwakilishi wa wakulima wa Mkoa wa Kagera na nyuma yangu wakiwa Wabunge wote wa Mkoa wa Kagera, tunamuomba hebu aangalie kwenye hili zao la kahawa, watu wamelia ni kilio cha siku nyingi. Hebu aangalie tunatoa ada, tozo na fees gani ili kumwezesha huyu mkulima na yeye mwenyewe aweze kufaidi jasho lake aweze kupata bei ya juu ili angalau kilo moja isiteremke chini ya shilingi 3,000. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati namalizia, unakumbuka kwamba watu wa Mkoa wa Kagera na Mwanza wanafanya biashara na Uganda kwa kupitia Ziwa Victoria. Meli ya Mv Bukoba ilizama, Victoria imezeeka inakarabatiwa kila kukicha lakini wafanyabiashara wanapata matatizo kwa sababu ili waweze kupeleka mazao yale ina… (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.