Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu, pili nipende kumshukuru pia Mwenyekiti wangu wa Chama cha CHADEMA na nipende kumpongeza kwa hotuba yake nzuri iliyoletwa hapa Bungeni yenye kuonesha dira na mdororo wa uchumi wa Tanzania juu ya bajeti yetu iliyoletwa hapa Bungeni. Bajeti iliyoletwa hapa Bungeni ni bajeti hewa, na nitaendelea kusema kwamba ni bajeti hewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya kwa sababu moja. Ukiangalia Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani ukurasa wa 35, kwenye Wizara ya Kilimo, zimetengwa asilimia 2.22, Wizara ya Viwanda na Biashara imetengwa asilimia nane, Wizara ya Afya asilimia 25. Mheshimiwa Waziri Mkuu, hii asilimia 25 unazipenda kweli afya za Watanzania, maana hii asilimia 25 ndiyo imebeba maisha ya afya zote za Watanzania juu ya
matibabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nianze kwa kuchangia juu ya hii Wizara ya Afya; Serikali ya CCM iliahidi kujenga zahanati kwenye kila kijiji na kata na vituo vya afya. Swali la kujiuliza; kwa bajeti hii ya asilimia 25 fedha hizi zitakidhi kweli vigezo vya afya katika Tanzania yetu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda katika Mkoa wangu wa Mara, Hospitali ya Mkoa wa Mara ni jambo la kusikitisha na ni aibu, tena mahali ambapo anatoka Baba wa Taifa, hospitali haina hadhi kwamba ni hospitali ya mkoa. Mfano mdogo, CT scan, ile hospitali haina CT scan na mtu akitaka kufanyiwa hicho kipimo ni mpaka wampe rufaa kwenda Bugando, Mwanza na Bugando hiki kipimo hakipo, hakipo Bugando wala Sekou Toure, ni aibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipimo cha CT scan kipo kwenye hospitali moja tu tena ni dispensary ya mtu binafsi, inakuwaje mtu binafsi anaweza kununua hii mashine lakini Serikali inashindwa, ni jambo la kujiuliza na ni jambo la kusikitisha. Pia wanapokwenda kufanya hicho kipimo kwenye hiyo dispensary gharama yake ni kuanzia 290,000 kuendelea, je, mwananchi mwenye kipato cha chini hiyo 290,000 ataitoa wapi? Moja kwa moja inaonesha kwamba Serikali haina nia nzuri juu ya afya ya Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakwenda katika Hospitali ya Wilaya ya Bunda. Hospitali hii ni hospitali inayohudumia wilaya tatu, lakini ile hospitali imeandikwa Hospitali ya Wilaya ya Bunda lakini yale madawa yanayopelekwa pale ni ya kituo cha afya. Hakuna madaktari bingwa kisa tu hakuna mortuary. Ndugu zangu tambueni zile wilaya tatu ni wilaya zenye wananchi wengi na hakikisheni kwamba msipoiweka katika
hadhi nzuri ile Hospitali ya Bunda mnahatarisha maisha ya watu wa Mwibara, Musoma Vijijini na Bunda yenyewe na uzuri Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mheshimiwa Bulaya ameshalisemea sana suala la Hospitali ya Wilaya ya Bunda. Kwa hiyo basi, ninachoomba, Serikali iseme kwamba ni lini itaipa hadhi Hospitali hiyo ya Wilaya ya Bunda ili wananchi wa Wilaya ya Bunda na wao wawe na hali nzuri kwa kuona kwamba wilaya yao ina hospitali ya wilaya, inaleta sifa pia kwa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia kuhusiana na suala la maji Bunda; sasa hivi ni takribani miaka 10 Wilaya ya Bunda kila siku wanasema maji yataletwa matokeo yake mpaka sasa maji bado hayajaletwa. Kila siku mnasema chujio, hilo chujio litatengenezwa lini ili wananchi wa Bunda wapate maji salama. Tunaomba mradi wa maji Bunda ukamilike ili wananchi wale na hasa upande wa akinamama,
akinamama wanateseka sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwenda kuhangaika kutafuta maji na wakati maji yapo shida ni chujio. Kwa hiyo, tunachohitaji Wilaya ya Bunda inahitaji ipate maji salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaenda upande wa elimu bure. Naomba tu niseme ukweli, mshaurini tu Mheshimiwa Mtukufu kwamba hili suala tayari sasa hivi limeshashindikana ili liwe wazi kwa wananchi na ikiwezekana pia aombe tu msamaha kwa wananchi kwamba hili suala limeshashindikana ili wananchi wenyewe waweze kuchangia kusomesha watoto wao. (Makofi)
TAARIFA....
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru lakini sitaipokea kwa sababu najua Waziri Mkuu atakuja kujibu hoja, tuseme tu ukweli elimu sio bure, Mheshimiwa Simbachawene.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaenda upande wa hili suala lililopo Tanzania sasa hivi, ni hali ya kutisha hili suala la utekaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utekaji kwa kweli ni suala ambalo linatisha juu ya maisha yetu na juu ya maisha ya Watanzania. Kila mtu
anasimama hapa anaongelea juu ya utekaji, naomba wewe kama Mwenyekiti uliyekalia hiki kiti hapo mjiulize ni kwa nini kila mtu anasimama na kuongelea suala la utekaji? Halafu Waziri mwenye dhamana, Waziri Mkuu hajatamka kitu chochote mpaka dakika hii, kusema ukweli inasikitisha na ni jambo la aibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachoomba, Ben Saanane amepotea ni muda mrefu sasa umepita, Serikali imekaa kimya. Msanii Roma alitekwa lakini cha ajabu yule mtu kapatikana kwenda kujieleza matokeo yake Waziri wa Michezo eti anamsindikiza, unategemea yule msanii ataongea kitu gani cha ukweli? Ina maana Serikali inajua ni kitu gani kilicho nyuma yake.