Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na kwa namna ya pekee nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge aliyeketi kwa kutoa mchango mzuri ambao hauna unafiki wala ubabaishaji.
Ameeleza vizuri kuhusu utawala bora na Wabunge wa namna hii ndiyo wanaotakiwa ili kuijenga Tanzania kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri iliyofafanua mambo mengi ya msingi kuhusu kilimo, afya, maji na maendeleo mbalimbali ya nchi yetu. Hata hivyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa upande wa afya mmefanya kazi kubwa lakini bado zipo changamoto nyingi sana. Changamoto kwenye majimbo ya vijijini ni kubwa mno. Tukija mijini huku tunawakuta madaktari bingwa wa akinamama na magonjwa mbalimbali lakini vijijini tunakuwa na daktari mmoja halafu huyo ndiyo bingwa wa magonjwa yote. Kwa
hiyo, nataka nichukue fursa hii kuwapongeza sana madaktari wanao-save katika vijiji vyetu, wanafanya kazi kubwa sana kwa sababu magonjwa ya akinamama ni yao, ya watoto ni yao na ya akinababa ni yao. Hawa ndiyo ambao nataka kuwatambua leo kwenye Bunge kwamba ni madaktari bingwa kwelikweli kwa sababu wanashughulika na matatizo makubwa sana ya wananchi vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa uamuzi sahihi wa kuamua kujenga baadhi ya vituo vya afya kwenye maeneo yaliyotengwa sana na maeneo makubwa ya kupata huduma nzuri za afya. Kwa mfano, ukitazama Tarafa yangu ya Mpwayungu, pale usiponipa kituo kikubwa cha afya ni hatari sana kwa akinamama wajawazito, kwa sababu kutoka Mpwayungu mpaka kuja Hospitali Teule ya Wilaya pana kilometa kama 85 niambie barabara ya vumbi, mama mjamzito anafikaje hapo kuja kuwahi operesheni. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa uamuzi wenu sahihi na nina hakika hili mtaliangalia kwa jicho la huruma kwenye majimbo mengi ya vijijini hasa yaliyokosa huduma za msingi za kiwango hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia habari ya Wizara ya ujenzi, itazame vilevile barabara za vijijini.
Tunazungumza sana ujenzi wa barabara za mijini lakini za vijijini tunaacha. Barabara za vijijini zikipitika kwa kiwango kizuri zitarahisisha sana huduma za maendeleo kwa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumie kwa haraka haraka Wizara ya Maji. Maji ni Wizara mtambuka. Tukipata maji safi na salama tutapunguza kwa kiasi kikubwa sana matumizi kwenye Wizara ya afya kwa sababu magonjwa mbalimbali ambayo yanaweza kutibika kwa
kupata maji safi na salama yatakuwa yameji-solve yenyewe na kuruhusu wananchi wafanye shughuli zingine za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na pongezi zangu kwa Wizara zote ambazo Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziwasilisha katika hotuba yake hii, nataka nizungumzie vile vile suala la ulinzi na usalama. Suala la ulinzi na usalama limezungumzwa hapa kwa mapana na marefu lakini nataka nizungumze kwenye kipengele kimoja. Nichukue fursa hii kusema watu wanaotuhumiwa, unajua Wabunge tunachanganya kuna wengine wanasema kuna kikundi kidogo ndani ya Usalama wa Taifa wengine wanasema Usalama wa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwapongeze sana watu wanaofanya kazi kwenye idara hiyo. Idara ya Usalama wa Taifa inafanya kazi kubwa sana, inafanya kazi nyeti sana na kuna baadhi ya watu nitawataja hapa bila kuwepo ulinzi na usalama kwenye maeneo yao wasingekuwepo hapa.
Mnakumbuka wakati wa msiba wa Chacha Zakayo Wangwe, ni watu wa Usalama wa Taifa ndiyo walimuokoa Mbowe pale Tarime nani hajui? Kwa hiyo, wakati mwingine tusiwe tunawalaumu tu pale wanapofanya vizuri tuwasifie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme habari ya kupotea watu mimi mwenyewe ni mhanga, wako ndugu zangu walishapotea siku nyingi wengine walipotea mwaka 1980 na hwakuwa wanasiasa. Tanzania hii hata ukitaka kila Mbunge aorodheshe watu waliowahi kupotea wapo.
Hawapotei kwa sababu kuna kikundi kinapoteza watu, hapana! Kupotea kwa wananchi ni jambo la kawaida ila tunaitaka Serikali
iendelee kutafuta wananchi waliopotea hata wale ambao hawana majina. Kwa sababu nchi hii tusiseme tu akipotea mtu fulani maarufu ndiyo tunaanza kuzungumza. Upotevu wa wananchi ni jambo la siku nyingi. Kwa hiyo, tuitake Serikali, Idara ya Upelelezi ifanyie kazi mambo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnazungumza mnasema eti ooh kuna Mkuu wa Mkoa alisema mtu fulani aliyepotea ataonekana kesho mbona Kubenea alisema kwamba huyu Saanane anafahamika na kila siku anaonekana, mbona hamumhoji Kubenea? Kubenea si huyu hapa mhojini? Mbona alisema kwamba Saanane yupo anatafuta kiki tu? Kwa nini msianze na Kubenea mnaanza kuisakama Serikali? Anzeni na Kubenea atuoneshe Saanane yuko wapi, Kubenea anajua.
Taarifa...
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Wabunge wengi
hawana ofisi. Tunaitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kukamilisha ujenzi
wa ofisi za Wabunge ili Wabunge waweze kufanya kazi zao
kwa ufanisi. Tunaitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia TAMISEMI
isimamie ujenzi wa Ofisi za Wabunge ili Wabunge waweze
kupata Ofisi zao na waweze kufanya kazi zao kwa uhakika,
waweze kuheshimika kwenye majimbo yao tofauti na sasa
ambapo Wabunge wengi wanafanyia kazi zao nyumbani,
hili haliwezekani. Ofisi zimejengwa hazijakamilika, kuna
maeneo fulani mpaka frame zinaanza kung’olewa, kuna
maeneo fulani majumba yanaoza kabla hayajamalizika,
tunaitaka Serikali ikamilishe ujenzi wa Ofisi za Wabunge ili
Wabunge wafanye kazi zao kama sheria inavyotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpongeze sana
Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kipindi cha mwaka mmoja
mmefanya kazi kubwa sana. Mheshimiwa Rais amesimamia
maadili, nidhamu na uwajibikaji. Leo tunapozungumza hapa
Rais anazindua ujenzi wa reli ya standard gauge ambayo
itatumia saa moja kufika Morogoro na baadaye
watakamilisha Dodoma na kuelekea Mikoa ya Kanda ya
Ziwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya kazi kubwa sana kwa vitendo na tunamwomba Rais aendelee kusimamia nidhamu ya uwajibikaji, nidhamu ya mapato na matumizi, aendelee kusimamaia amani ya nchi yetu ili watu tuweze kuishi kwa amani na tufanye kazi kwa bidii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.