Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu kwa kutufikisha salama katika Bunge hili. Pia niwape pole wafiwa na majeruhi wa ajali, pia naipongeza Serikali kwa maamuzi yake ya kuhamia Dodoma. Pamoja na juhudi zake za Kasi katika kuinua uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tumedhamiria kuwa na Tanzania ya viwanda, ni vyema sasa Serikali ikajikita kwa kina katika kuhakikisha kuwa umeme wa kutosha unapatikana ili tuweze kuendesha viwanda vyetu especially kwenye umeme wa gesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali kujitahidi kutatua changamoto ambazo zinagusa kwa kiasi kikubwa wananchi, mfano maji, afya na elimu, hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kunyanyua jamii yetu na kuifanya jamii yetu ishiriki vyema kwenye maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la maji pamoja na jitihada kubwa za Serikali kuhakikisha tunapata maji safi na salama, bado kuna changamoto kwa upande wa watendaji hususan katika maeneo ya vijijini. Hii inatokana na utendaji wa mazoea kwa wataalam wa Idara husika.
Mfano unakuta Mhandisi wa Maji amekaa eneo moja kwa zaidi ya miaka kumi na pamoja na kukaa miaka yote hiyo tatizo la maji bado lipo palepale pamoja na kulipwa mshahara na mahitaji mengine. Nashauri kuwe na uhamisho kwa watendaji ambao wamekaa sehemu moja kwa muda mrefu na pia ni vizuri wakaangaliwa performance yao kila mara ili kuona ni jinsi gani wanafanya kazi ya kutatua kero hii ambayo inagusa
kila jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la Elimu; ni vizuri Serikali ikatoa mwelekeo mzuri kwa Halmashauri ni jinsi gani wanasaidiwa na wananchi katika ujenzi wa madarasa mfano kuna mkanganyiko kati ya Halmashauri na wananchi. Tunaambiwa kama wananchi tujenge boma na Halmashauri itaezeka juu. kuna maboma mengi yameshajengwa na wananchi lakini bado Halmashauri zinasuasua katika mpango wao wa kumalizia juu na ukizingatia idadi ya wanafunzi inaongezeka kwa kiwango kikubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa afya, pamoja na jitihada, kubwa kuhakikisha huduma ya afya inaimarika, bado kuna changamoto kwenye ununuaji wa dawa na upungufu wa Madaktari. Nashauri Serikali ihakikishe MSD wanapata dawa ya kutosha ili kuepuka kuonekana
kulemewa na order kwenye hospitali zetu au kuweka utaratibu wa kuziwezesha hospitali kununua dawa maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la upungufu wa Madaktari na Wauguzi ni kubwa sana na lipo nchi mzima. Ningependa kuiomba Serikali ifanye haraka kulishughulikia suala hili, mfano katika jimbo langu, kuna upungufu wa karibia asilimia ishirini ya Madaktari na Wauguzi na ukizingatia hospitali yetu inahudumia majimbo manne. Upungufu huu, unasababisha vifo vya mara kwa mara kutokana na kuchelewa kuhudumiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kuipongeza Serikali kwa uamuzi wa kuyaondoa maduka yote ya watu binafsi (ya dawa) ila iharakishe kuhakikisha maduka ya Serikali yanaanzishwa haraka.