Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo heshima kuipongeza Serikali ya CCM kwa kazi nzuri. Kipekee kumpongeza Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anayoijenga Serikali na kuwafanya Watanzania wajisikie vizuri. Naomba nitoe ushauri ufuatao ili kuongeza ufanisi wa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uteuzi wa kada mbalimbali kwa Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Makatibu Tawala na Wakurugenzi uzingatie faida ya wateuliwa hao na ni vizuri wafanyiwe usaili (interview) ili kujiridhisha uwezo wao. Mfano Katibu Tawala Mkoa au Wilaya ni wakuu wa Watumishi wote wa Umma katika maeneo yao. Watendaji wa nafasi hizo ni lazima au vizuri, wawe na ueledi na uamuzi unaoashiria kuwa wao ni Wakuu wa Watumishi wa Umma. Mheshimiwa Waziri Mkuu, DAS wa Makete alikuwa mtunza fedha (cashier) kampuni ya TiGO, ndiye sasa Mkuu wa Watumishi wa Umma wote wa Wilaya ya Makete.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu, yapo madhara hasi kwa kuteua wateule ambao watumishi wa mahali pale wanaona kiongozi wao hatoshi. Morali wa watumishi wa umma inakuwa chini kwa maana wanakuwa hawaungi mkono Serikali. Hili ni kubwa sana kwa kuwa Serikali yoyote lazima iangalie madhara ya kutoungwa mkono. Pamoja na nia nzuri ya Rais wetu na wewe mwenyewe Waziri Mkuu, wateuliwa wanaotoka nje ya mfumo wa Serikali, nachukua muda mrefu kujifunza na hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa letu na kuipunguzia kukubalika Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wateuliwa kama Wakuu wa Mikoa na Wilaya, wanajikuta wanakosa weledi katika kutumikia nafasi zao. Kwa bahati mbaya kila ubaya unaofanywa na viongozi wa Serikali anayeadhibiwa ni CCM. Jambo la pili. ninaomba ofisi yako Mheshimiwa Waziri Mkuu au Ofisi ya Rais iunde timu ya watu waliopewa neema ya kufikiri. Nakumbuka wakati mzee Malecela akiwa Waziri Mkuu mwaka 1991-1994 aliunda Kamati ya Mipango ambayo kazi yake ilikuwa ni kuisaidia Serikali kufikiri. Kufikiri ni kipawa haimaanishi kuwa mtu akiwa na elimu kubwa basi uwezo wake wa kufikiri unaongezeka. Bali ujuzi wa eneo alilojifunza ndio unaongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati hii inaweza kujumuisha watu mbalimbali hata baadhi ya Mawaziri (kama wana zawadi ya kufikiri) ili kuisaidia Serikali kutoa ushauri wa kiuweledi bila kusukumwa na maneno yasiyo na mashiko. Timu hii itasaidia kutoa weledi kwenye uwekezaji, siasa na
kadhalika. Jambo kubwa ni kuwa, moja kati ya changamoto ambazo Serikali karibu zote duniani zinapata, ni uhakika wa taarifa inazozipokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naipongeza sana Serikali yetu ya CCM kwa kuangalia vipaumbele ikiwa ni pamoja na ujenzi wa reli ya kati na barabara mbalimbali katika nchi yetu Tanzania. Nami nawaombea viongozi wote mpate kuwa na afya njema na utashi mkuu. Ahsante.