Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti Ninamshukuru Mungu kwa rehema na neema yake. Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri iliyosheheni taarifa zote muhimu zinazogusa kila sekta ya Serikali. Aidha, nawapongeza Mawaziri walio chini ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Jenista Mhagama, Mbunge wa Peramiho na Mheshimiwa Anthony Mavunde, Mbunge wa Dodoma Mjini kwa kazi nzuri wanayoifanya chini ya uongozi wake mahiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ukuaji wa Uchumi; napenda kuzungumzia masuala kadhaa yahusuyo. Naipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kukuza uchumi wa asilimia 7.0 kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Haya ni mafanikio makubwa sana kidunia na inaashiria kuweka mikakati na mipango mizuri ya kiuchumi na kimaendeleo ambayo imetekelezwa ukuaji huu. Pomoja na pongezi hizi, naomba niitakie Serikali kuhakikisha kuwa ukuaji huu wa uchumi unatafsiri kuwa maendeleo kwa mwananchi mmoja mmoja na kwa ujumla. Hii inawezekana kwa Serikali kuhakikisha kuwa inaweka miradi ya kimkakati katika sekta na sekta ndogo ambazo zinagusa moja kwa moja maisha na ufanisi wa wananchi
wetu wa hali ya chini hasa vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kupendekeza kuwa uwepo mpango kazi wa kuhakikisha vikosi vya vijana na wanawake kupitia SACCOs, ushirika na makundi mengine na kuwapatia mafunzo ya kuwajengea ujuzi katika kilimo, ufugaji, uvuvi wa kisasa. Sambamba na mafunzo Serikali iweke mkakati wa kuwapatia mitaji, vitendea kazi na pembejeo, lakini vilevile kuweka mkakati wa kujenga maghala, masoko na miundombinu ya barabara ya kuunganisha uzalishaji na masoko katika mnyororo wote wa thamani kwa kila zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu ndiyo itakayoweza kufanya haya yote kisayansi na kuyasimamia. Hili haliwezi kuachiwa NGOs au watu binafsi kujianzishia vitu kiholela au wananchi wenyewe. Hili ni lazima lisimamiwe na Serikali yenyewe kama mkakati wa kushirikisha wananchi wote katika uchumi (inclusiveness). Mkakati tajwa hapo juu utajihakikishia ajira, kipato cha wananchi lakini na pato la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, afya ni muhimu sana kwenye ufanisi wa nchi. Sekta hii inajumuisha lishe na huduma za afya kwa muda mrefu wananchi wamehamasishwa sana kujenga vituo vya afya na zahanati kwa kujitolea. Nyingi zimekamilika kwa asilimia 80 au zaidi lakini zinahitaji
kumaliziwa. Naiomba Serikali ihakikishe kuwa zahanati na miundombinu hii inamaliziwa na kukamilishwa ili zianze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la lishe bora bado halijazingatiwa na kuwekewa mkakati mahsusi ya kuhamasisha na kutoa mafunzo ya lishe bora. Kwa kutumia maofisa wa ustawi wa jamii. Vipindi vya redio na televisheni, vituo vya afya na ngoma na michezo ya kuigiza. Hii itasaidia
sana kupunguza utapiamlo na huduma kwa watoto wetu takriban asilimia 42. Vyakula vipo ni elimu tu ndiyo inayohitajika kuhakikisha matumizi mazuri ya vyakula mbalimbali ili kupunguza utapia mlo. Huu uwe mkakati mahsusi wa kuboresha lishe ya watoto na wanawake wajawazito.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sekta ya Afya masuala ya vifo vya wanawake wakati wa kujifungua na vifo vya watoto wachanga na wale wa chini ya miaka mitano. Bajeti ya afya itenge fungu maalum la kuhakikisha vifaa tiba na huduma muhimu za wazazi zinakuwepo. Wahakikishe kuwa vifaa vya kupokelea watoto wanapozaliwa hospitali vinapatiakana ikiwa ni pamoja na maji, wodi, wauguzi na vyumba vya kupumzikia wanawake wanapojifunguapamoja na vyumba vya upasuaji. Haya yatapunguza kwa kiasi kikubwa sana vifo vya wazazi na watoto wakati wa
kujifungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu UKIMWI na watu wanaoishi na VVU changamoto kubwa ni mashine za kupima viral load na fedha ya dawa za kurefusha maisha lakini vile vile uhamasishaji kwa wananchi. Wazee bado hawajawekewa mkakati wa kitaifa kwa kuhakikisha matibabu, kupimwa afya, kuelimishwa juu ya maradhi yanayowasibu, lakini pia wazee waingizwe kwenye TASAF wote kupunguza hoja ya kuwapa kipaumbele.