Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza na kuunga mkono hoja na nachangia katika masuala yafuatayo:-
Kilimo, umuhimu wa Sekta ya Kilimo katika uchumi uko wazi; naishauri Serikali kuweka dhamira na mikakati kuongeza uzalishaji tija kuwa kilimo chetu kiwe cha kibiashara. Hivyo yafuatayo yazingatiwe.
(a) Kilimo cha umwagiliaji kwa kuongeza mabanio yaliyopo sasa hususan katika maeneo ambayo yana fursa za uhakika wa mito ya kudumu kwa Mkoa wa Morogoro, Wilaya za Malinyi, Ulanga na Kilombero.
(b) Uwepo wa Soko la kuhakikiwa kwa mazao ya kilimo. Wakulima katika kero kuu zinazowakabili wakulima ni soko la uhakika kwa mazao hususan mazao ya nafaka kama mpunga au mahindi. Mifugo; mwendelezo/ongezeko kubwa la mifugo na ufugaji kiholela wa mifugo aina ya ng’ombe nchini inahatarisha uchumi wa nchi huko siku za usoni. Nashauri Serikali kusimamia na kutekeleza zoezi la matumizi bora ya ardhi ili yatengewe maeneo mahsusi kwa malisho ya mifugo. Aidha, Serikali kuweka miundombinu rafiki wa mifugo kama marambo ya maji na visima katika maeneo ya malisho ya mifugo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa hili utasaidia kwa kiasi kikubwa sana kumaliza changamoto katika mifugo, migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji. Aidha, itainusuru nchi katika kuelekea nchi kuwa jangwa kama tutaendeleza ufugaji/uchungaji wa ng’ombe kiholela.
Ahsante.