Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2017/2018 unaonyesha kwa kiwango kikubwa Serikali inategemea kukopa fedha katika mifuko hii ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo, kukopa sio dhambi, lakini mikopo ambayo inazidi uwezo na kupelekea hatari ya kuua/kufifisha uwezo na kupeleka hatari na lazima Serikali ituambie imejipanga vipi kuhakikisha mifuko hii haifi/kupunguza uwezo wake?
(a) Je, return on investment kwa miradi ya namna hii ambayo inachukua muda mrefu kurudisha faida imetazamwa kwa kiwango gani?
(b) Je, foreseeable risk kwenye operation za viwanda na miradi inayowekezwa imefanyika assessment kina?
(c) SSRA ambaye ni mdhibiti na msimamizi wa mifuko hii inaweka ukomo/kiwango kwa mifuko kutokopa zaidi ya 20%. Hata hivyo kwa taarifa ya Benki Kuu ya mwaka 2016 inaonyesha kuwa proportion ya mifuko kwenye deni la ndani ni 26% kutoka 16% na imechukua nafasi ya mabenki ya biashara. Uhai wa mifuko hii upoje? Kwa nini Serikali iendelee kukopa zaidi kinyume na sheria zilizopo?
(d) Kumekuwa na hoja ya muda mrefu wa kuunganisha mifuko hii ya hifadhi ya jamii. Je, lini Serikali itaanza machako wa kuunganisha mifuko?