Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Waziri Mkuu kwa kuja na hotuba nzuri. Naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira kwa vijana. Hivi sasa kuna vijana wengi ambao wamehitimu katika vyuo mbalimbali vya ngazi zote lakini kuna tatizo la vijana kukosa kazi za kuajiriwa ama kujiajiri wenyewe. Tatizo la ajira lina athari kubwa kiuchumi, kisiasa na kijamii. Lazima Serikali ije na mpango mahususi wa kuwaajiri au kuwawezesha kushiriki katika shughuli za kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo; hivi sasa kilimo kinaajiri watu zaidi ya asilimia 75; ili nchi iendelee lazima kutoa pembejeo kwa wakati na kwa bei nafuu. Ahadi ya Waziri Mkuu kuwa na bei elekezi ni muhimu sana. Lakini pia mbegu nzuri, kilimo cha kisasa na umwagiliaji ni lazima kwa
kipindi hiki. Baadhi ya maeneo tuanzishe mashamba makubwa ya kuanzia kilimo na kuleta tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa za kulevya; naipongeza Serikali kwa hatua mbalimbali za kupambana na dawa za kulevya. Ni muhimu vita hii iendelee kwa nguvu zote ili kuiokoa nchi, vijana na Taifa kwa ujumla. Naomba Serikali iongeze nguvu zaidi kuwakamata wauzaji, wasambazaji na watumiaji. Tungependa kusikia Kamishina wa Kupambana na Dawa aongeze kasi na kutupatia taarifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, rushwa; hivi sasa kuna rushwa sana katika maeneo ya Serikali za Mitaa kwa mfano Mbozi hali ni mbaya sana. Naomba vyombo vinavyohusika vichukue hatua za haraka kwani wananchi wanateseka sana.