Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anayofanya katika kusimamia shughuli za kila siku za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii mambo mengi yaliyomo ndani ya hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu mengi ni mazuri, lakini ningependa kuchangia baadhi ya maeneo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa walimu wa shule za msingi na sekondari, baadhi ya maeneo mengi hasa katika Halmashauri zetu hayana walimu wa kutosha; uwiano wa mwalimu mmoja kufundisha idadi ya watoto inatofautiana. Mfano Mkoa wa Tabora mwalimu mmoja
anafundisha watoto 40 uwiano huo unaonyesha dhahiri kuna ugawaji mbaya wa watumishi hususani katika kada ya walimu naomba suala hili litazamwe kwa umakini na kurekebishwa kwa sababu inarudisha juhudi za Serikali za kutoa huduma sawa kwa wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile suala la usimamizi wa miradi ya maji katika miji yote na Halmashauri zetu kunakuwa na mapungufu mengi. Serikali haina utaratibu ulio imara wa kukagua mradi mingi ya maji ambayo imegharimu Serikali fedha nyingi hali inayopelekea miradi
mingi kutoa huduma chini ya kiwango au kuharibika kwa muda mfupi naishauri kuanzia sasa Wizara ya Maji na TAMISEMI waweke utaratibu wa shughuli zao kila siku ziwe zinafuatilia miradi hii yote ilete matokeo yanayotarajiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali imuongezee CAG uwezo wa kifedha ili afanye kazi ya ukaguzi kwa ufanisi (performance auditing) kwa sababu ukaguzi huu umeonyesha kwa kiasi kikubwa namna gani Serikali inaweza kuufanyia kazi ushauri unaotolewa na CAG. Ukaguzi huu ni muhimu sana kwa sababu unalenga katika kuonyesha je, miradi imetekelezwa kwa ufanisi au la. Je, wakandarasi wa miradi mbalimbali wanatimiza wajibu wao? Na Wizara au Halmashauri nazo zinatimiza utaratibu wao? Kupitia ukaguzi kwa ufanisi Ofisi ya CAG imefanya kazi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naishauri Wizara ya Elimu iimarishe ukaguzi katika shule zote, kitengo hiki hakifanyi kazi sawasawa ndio maana hata baadhi ya shule zote zinafanya vibaya katika matokeo ya mitihani yao, zamani kiwango cha ukaguzi wa shule zetu zilikuwa zikitoa
taarifa za shule leo hii wakaguzi hawana vyombo vya usafiri ambavyo vinaweza kuwasaidia kutembelea shule zote. Wakaguzi hawa wapewe magari, ofisi pamoja na kuwezeshwa posho za mazingira magumu kuwapa moyo na kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuchangia eneo la migogoro ya ardhi baina ya wafugaji na wakulima.
Serikali wakati inafikiria kuleta sheria na mabadiliko juu ya ufugaji wa kisasa idadi ya wafugaji imeongezeka, wananchi wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki.
Nashauri sasa ukifuga mifugo michache kwa njia bora kabisa ya kisasa hii itapunguza migogoro. Lakini vilevile ione kuwa ufugaji bora wa mifugo utasaidia Serikali kuongeza pato lake la Taifa ikijikita katika kutoa elimu ya ufugaji bora. Vilevile elimu itolewe kwa wananchi wafugaji
lakini Serikali iandae miundombinu bora ya zero grazing hii italeta mapinduzi makubwa lakini itapunguza migogoro ya mara kwa mara ya wananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utunzaji wa vyanzo vya maji ni eneo lenye matatizo makubwa wananchi wamekuwa wakilima katika vyanzo vya maji lakini pia wananchi wengi kulima katika maeneo ya milima, ulimaji huu unaleta athari kubwa katika kuharibu mazingira. Lakini mbaya zaidi ukosefu wa mvua maeneo mengi umesababishwa na shughuli zisizo rasmi katika maeneo ya mabonde na milima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu kulima mita 60 kutoka vyanzo vya maji usimamiwe kwa dhati ikiwezekana iwe ni sheria kamili kulinda maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.