Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kutoa mchango wangu katika mjadala huu wa kuchangia hotuba ya bajeti ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya, uzima na uhai na kuwa hapa leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu Majaliwa Kasim Majaliwa kwa kazi kubwa anayofanya ya kusimamia shughuli za Serikali kwa weledi, maarifa na utulivu wa hali ya juu. Pia nampongeza Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayofanya ya kumsaidia Waziri Mkuu na wao wenyewe kufika katika Jimbo langu la
Morogoro Kusini Mashariki kwa nyakati tofauti katika kusukuma maendeleo ya watu wa jimbo langu na Watanzania kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa ni mnyimi wa shukrani kama sitamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwatumikia Watanzania na hasa kwa kutuletea maendeleo katika Jimbo langu kama vile Kiwanda cha Sukari katika Kata ya Mkulazi, barabara ya lami toka Ubena Zomozi mpaka katika kambi yetu ya Jeshi la Ulinzi na Usalama, Kambi ya Kizuka na mradi wa maji katika Kijiji cha Fulwe Mikese na mengine mengi katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na cha kupewa hakina nyongeza na kwa kuwa katika kijiji na Kata hii ya Ngerengere kuna kambi tatu za Jeshi kwa maana ya Kizuka na kikosi namba 23 na Sangasanga na kwa kuwa vy ote ni vikosi vyetu na wote ni wapiga kura wangu na hawa wa kikosi cha Sangasanga wasijisikie wanyonge na kubaguliwa na kusahaulika, kwa niaba yao, naiomba Serikali hasa Mheshimiwa Rais kuweka lami pia barabara toka Kizuka mpaka Ngerengere Mjini kupitia Sangasanga mpaka Mdauli ili vikosi vyote vitatu viweze kufikiwa kiurahisi kwa barabara ya lami na walinzi wetu kufaidi matunda ya uhuru kama dhamira njema aliyoonyesha Rais wetu Dkt. John Pombe
Magufuli kwa kuanza kuweka lami katika barabara ya Ubena-Kizuka. Naomba sana hii barabara ya Mdaula-Sangasanga- Ngerengere-Kizuka nayo kuwekewa lami kilometa kumi na tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuanza mchakato wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge ambayo inapita katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki katika Vijiji vya Kidunda, Ngerengere, Kimoko na Mikese ambayo italeta maendeleo
makubwa katika eneo la Morogoro Vijijini na Morogoro kwa ujumla ukizingatia sisi Morogoro ndiko inakoishia awamu ya kwanza ya mradi huu. Tunashukuru sana kwa mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo naomba kuishauri Serikali na kuiomba itoe ufafanuzi rasmi eneo la hifadhi ya reli ni kiasi gani sababu katika kuandaa utekelezaji wa mradi huu, wataalam wametoa notisi kwa wananchi kubomoa nyumba zao kupisha mradi lakini kila
sehemu ina umbali tofauti. Kwa mfano, Ngerengere wameambiwa umbali ni mita 120 kila upande, Mikese mita 90 na Morogoro Mjini mita 30 kila upande. Je, umbali wa hifadhi ni upi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba kutokana na Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999, Sheria Namba 4 na 5 na kanuni zake inasema kama mtu amejenga na kukaa zaidi ya miaka 12 bila kubughudhiwa eneo hilo ni halali yake. Je, kwa sheria hiyo Serikali haioni ina wajibu wa kuwalipa wananchi waliojenga na kukaa zaidi ya miaka 12 bila bugudha ili kutowarudisha nyuma kiuchumi wananchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia muda waliopewa wa mwezi mmoja kuhama ni mdogo sana kwa mwananchi wa kawaida kuhama tena bila ya fidia kupata fedha ya kujenga nyumba mpya. Naomba Serikali kuwapa muda wananchi wa miezi sita ili kupata muda wa kuhama kwa utulivu zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ni muhimu, michezo ni afya na Bunge linatuhimiza kushiriki mazoezi lakini hatuna uwanja wa kufanya mazoezi kwa timu zetu za Bunge. Kwa kuwa Serikali imehamia Dodoma na kutakuwa na mahitaji makubwa ya viwanja vya michezo, naomba kuishauri Serikali na Ofisi ya Bunge kuwaona CDA na Mamlaka ya Halmashauri kulipatia Bunge eneo la michezo kwa Timu za Bunge badala
ya sasa kutangatanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.