Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. JOSEPH R.SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Kilimo inaajiri
wananchi wengi katika nchi yetu. Vilevile katika azma ya Serikali ya kukuza viwanda ipo haja kubwa ya kuimarisha sekta hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao mengi ya biashara yanaelekea kukosa msukumo na wakulima kuyaacha. Hali hii inatokana na Serikali kuweka bajeti ndogo katika kilimo na hivyo kuifanya sekta hii kushindwa kuhudumia kilimo chetu. Hivyo, naomba:-
(i) Taasisi za Kilimo za Utafiti wa Dawa, Pembejeo na Mbolea lazima ziimarishwe kwa kupewa fedha za kutosha.
(ii) Bodi za Mazao haya kama Kahawa, Tumbaku, Pamba na kadhalika ziimarishwe ili kuweza kusimamia vyema mazao haya.
(iii) Tafiti za masoko ambayo yatawanufaisha wakulima kwa kuwapatia bei nzuri zifanyike.
(iv) Uhamasishaji ufanyike ili wakulima waendelee kuzalisha mazao haya kwa kuwa maeneo mengi hasa yanayolima kahawa wananchi wanaelekea kukata tamaa.
(v) Kuhusu mazao mchanganyiko Bodi ya Mazao Mchanganyiko iimarishwe.
(vi) Uhamasishaji ufanyike ili mazao yetu yaongezewe thamani ili kuyaongezea bili na pia kuongeza ajira kwa vijana wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika ni vema sasa kama nchi tuachane na kilimo cha msimu kwa kutegemea mvua na badala yake tuimarishe kilimo cha umwagiliaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Jimbo langu la Rombo wananchi wamekata tamaa sana katika kuzalisha zao la kahawa. Hii ni kutokana na gharama kubwa za
uzalishaji na bei kuwa ndogo; hali kadhalika kuyumba kwa Vyama vya Ushirika hasa KNCU. Mali na mashamba ya KNCU yameuzwa kiholela bila kuwashirikisha wanachama. Naiomba Serikali kuingilia kati ili kunusuru mali na mashamba
ya KNCU ili kuifanya iwe na nguvu na uwezo wa kulisimamia zao hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya maji nchini katika majimbo yote ni mbaya sana. Katika Jimbo langu la Rombo wananchi wanateseka sana na ukosefu wa maji. Vyanzo vingi vimekauka na maji yananunuliwa kwa sh. 1000 – 1500 kwa dumu la lita 20.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna miradi iliyoanzishwa, mfano Mradi wa Shimbi Mashariki na Leto. Miradi hii inasuasua kwa sababu ya fedha kutopelekwa kwa wakati. Kama miradi hii ikikamilika itasaidia kwa kiwango fulani kuatua shida hii
katika maeneo ya mradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa water table katika jimbo langu ni zaidi ya mita 300 na kuondoa uwezekano wa visima kuchimbwa katika maeneo mengi, hapa Bungeni Wabunge wote wa Rombo walionitangulia wameleta mapendekezo ya matumizi ya maji ya Ziwa Chala.
Tumekuwa tukipata matumaini miaka yote. Tunaomba sasa
suala hili lifikie mwisho. Ni lini maji ya Ziwa Chala yataanza
kutumika kwa ajili ya wananchi wa Rombo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kuhusu maji tuliomba ianzishwe Mamlaka ya Maji ya Wilaya ya Rombo.
Tunaomba kujua ni lini mchakato huu utakakamilka ili mgao wa maji kidogo tuliyonayo uwanufaishe wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu afya, hivi sasa tuna mchakato wa ujenzi wa jengo la OPD katika Kituo cha Afya Karume ili kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Hivi sasa ujenzi umesimama kutokana na Mkandarasi kutudai. Tunaiomba Serikali katika bajeti hii kutupatia fedha za kukamilisha ujenzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tuna Mradi wa Ujenzi wa jengo la Halmashauri. Hii ni halmashauri kongwe ambayo ina zaidi ya miaka 30, lakini hatuna jengo la halmashauri. Tunaomba katika bajeti fedha zipatikane ili ujenzi uendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu elimu tuna uhaba mkubwa wa Walimu wa sayansi. Tunaiomba Serikali katika mgawo wote wa Walimu wa sayansi tupatiwe kiasi cha
kuweza kutusaidia. Zipo shule ambazo tangu zimeanzishwa hadi leo hazina Mwalimu hata mmoja wa somo lolote la sayansi.