Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachangia kwa kuanza kuunga mkono hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ione haja ya kutangaza Mkoa wa Ulanga ili kusogeza huduma kwa wananchi. Taratibu zote ngazi za Halmashauri na Mkoa (RCC) zimeshafanyika. Pia itangaze Halmashauri ya Mlimba ambapo wananchi wa Mlimba wanataabika kumfuata Mkurugenzi kilometa 269 na miundombinu mibovu na kushindwa kupata huduma kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara kutoka Ifakara- Taweta - Madeke - Njombe. Takribani kilometa 269 haipitiki, hivi niandikavyo taarifa hii, barabara hiyo haipitiki hata mabasi ya abiria yaliyokuwa yanatoa huduma yamesitisha kutokana na ubovu wa barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nauli zimepanda kutoka sh. 20,000/= hadi sh. 40,000/= kufika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ambako huduma zote za matibabu, mahakama na kadhalika zinapatikana. Hali hii ni mbaya, hivyo naomba
Serikali ione hitaji kubwa la kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hiyo inategemewa sana na wananchi kusafirisha mazao yao ukizingatia barabara hiyo iko kwenye eneo la ghala la chakula (kilimo
kikubwa cha mpunga, mahindi (KPL) pia cocoa, ndizi na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kilio kingine kikubwa kwa wananchi wa Mlimba ni maji safi na salama. Hivyo naomba Serikali ianze na kero kubwa hizi mbili, barabara na maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.