Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonyesha kwamba toka mwaka 1980 mpaka 2010 Afrika pamoja na resources tulizonazo tumepoteza kiasi cha dola trilioni 1.4. Takwimu hizi zinaonyesha hii yote imesababishwa na uongozi mbovu katika Bara la Afrika. Mojawapo ya sababu ni
kutokuwepo mwendelezo wa viongozi wanapobadilishana madaraka. Nchi yetu katika Serikali hii ya Awamu ya Tano kumekuwa na changamoto kubwa sana ambazo takwimu hizi zina-cement kwamba na sisi kama Taifa tunaweza tukaendelea tena kupoteza mali tulizonazo kwa sababu ya tatizo la uongozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mtawa mmoja wa Kikatoliki aliishi miaka 1953 kule Marekani anaitwa Bishop Sheen, aliwahi kusema; “Civilization is always in danger when those who have given the right to command have never learned how to obey.” (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu iko kwenye kiza kinene kwa sababu kuna watu wengi sana ambao wamepewa mamlaka ya kuamrisha lakini wao wenyewe hawajawahi kujifunza namna ya utii. Nazungumza haya kwa masikitiko makubwa sana kwamba tatizo kubwa tulilonalo
katika Serikali ya Awamu ya Tano ni poor leadership skills ambayo hii inaweza ikatupelekea tukaingia kwenye matatizo makubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amezungumzia sana masuala ya Chuo cha Uongozi, lakini nina wasiwasi sana kama hiki chuo kina mtaala wa namna ya kuwa-train hawa watu. Kwa bahati mbaya katika nchi yetu uongozi unakuwa defined kwa title au status badala ya
function. Uongozi wa sasa hivi tulionao wa Awamu ya Tano ni uongozi ambao ni bully, ni uongozi ambao ni una-scream, ni uongozi ambao una-shout, ni uongozi unao-intimidate badala ya kuonyesha njia. Kwa sababu ya uongozi huu umeparalyze civil service na tuki-paralyze civil service maana yake itashindwa ku-produce. Watu wako intimidated na uongozi huu hauko based kwenye merit kwa sababu watu hawajawa
trained.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini utanitunzia muda wangu lakini na wewe mwenyewe umechanganya actually, sasa sijui hapo umesemaje, sijui ni Kiswahili hicho?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika society ambayo nimeritocracy the blind cannot lead the sighted, uninformed cannot lead the wise and the unskilled cannot direct the skilled. Katika uteuzi wa Mheshimiwa Rais, amechukua makada wengi wa Chama cha Mapinduzi amewaingiza
kwenye civil servant ambayo hiyo ina-cripple utendaji wa kazi. Haya mambo hatuwezi kuyanyamazia kwa sababu hili Taifa ni la wote na ni kinyume kabisa na utaratibu. Ndugu zangu wote tukumbuke hapa tunapokwenda kwenye uchaguzi watu wote sisi tunakuwaga hatuna madaraka sisi wanasiasa, huwa wanabaki civil service, ukii-cripple civil service maana yake unaua utendaji kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimshauri tu Mheshimiwa Rais ambapo wenzangu wengi wanaogopa sana hata kumshauri, maana yake Mheshimiwa Rais akisema mkikamata watu wanavunja sheria ng’oa matairi kuna watu wanapiga makofi kinyume cha taratibu. Mheshimiwa Rais akisema mimi sikuleta matetemeko wanapiga makofi.
Mheshimiwa Rais akisema mkikutana na jambazi huko hata kabla hajapelekwa mahakamani kinyume cha sheria watu wanapiga makofi, wanadhani kumsifu Mheshimiwa Rais kwa kile anachokifanya ni uzalendo. Tunatengeneza Taifa la waoga ambapo tuna cripple national kama hatuwezi kucriticise viongozi wetu. Tuko hapa kuwafanya viongozi wetu wawe accountable na ndiyo wajibu wetu, (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Thomas Jefferson, Rais wa Marekani aliwahi kusema ukiona wananchi wanaiogopa Serikali jua Serikali hiyo ni ya kidikteta. Ukiona Serikali inawaogopa wananchi jua Serikali hiyo ni ya kidemokrasia kwa sababu Serikali lazima iwe accountable kwa wananchi.
Sisi hapa kama Wabunge tuko hapa kuwawakilisha wananchi, the government must fear us. Serikali lazima ituheshimu sisi kwa sababu lazima iwe accountable kwetu.
Leo tunafika Bungeni tunanyamazishwa eti tusiikemee Serikali, why are we here? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kama kiongozi, wewe kama kiongozi you are accountable to us, Serikali mko accountable kwa Bunge hili. Sasa kila kitu mna-protect, chochote mnachofanya mna-protect, Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ni ku-scream, shouting. Huwezi kujua leo ni msiba au leo ni harusi, huwezi kujua leo wako kwenye matatizo, leadership is about inspiring people, putting people to work is not about screaming and shouting. Tuna uongozi wa Awamu ya Tano ambao una-shout, una-scream unaintimidate everybody kwa hiyo ume-paralyze watu kufanya kazi. Halafu wengine wasomi hapa na ninyi mnakaa kimya mnapiga makofi mambo ambayo ni kinyume na utaratibu wa sheria ya nchi yetu, where we heading? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, the unskilled cannot direct the skilled. Tumekubali kuweka akili zetu mfukoni tunaongozwa na wale ambao ni unskilled. Leo tuna watu kama akina Bashite amesema Sheen hapa, those who have never learned how to obey they have given the right to
command, mtu kama Bashite anachokijua ni kuvaa shati la kijani na kumtukana Lowassa, ndicho alichoweza. Leo anakuwa Mkuu wa Mkoa anatoa amri kubwa halafu tunampigia makofi. Wale ambao ni incompetent wanawaongoza competent, kwa hiyo, utendaji kazi
unashuka wanaona sasa hata maana ya kusoma haipo. Kwa hiyo, mtoto yeyote anachoona ili niwe kiongozi ni kujua kumtukana mtu mmoja wa chama kingine, wapi tunakwenda jamani?
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna wanasheria kwa mfano Mwanasheria Mkuu hapa, wajibu wake mkubwa yeye ni kuhakikisha Serikali inafanya kazi lakini na yeye amegeuka amekuwa Mbunge anatetea Serikali. Badala ya yeye kunyoosha akiona Serikali inakosea anasema Chief Whip
hebu ili jambo tu-withdraw tukajipange vizuri kwa sababu yeye ni kuweka mambo vizuri mwisho wa siku huu ni mtumbwi wa sisi wote lakini kilichotokea ni kati ya upinzani na sisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mtaalamu mmoja anasema Taifa ambalo linazalisha soft minded people linanunua kifo kwa installment cha Taifa lenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mnadiscourage criticism katika Bunge, mna-discourage dialogue mnataka tuwe tunapiga makofi, why are we here? Kama mngetaka tusije hapa mngetuzuia kule kule Iringa wakati wa uchaguzi, the fact kwamba watu wa Iringa wamenileta
hapa I will speak, I will talk.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tuna TISS (Usalama wa Taifa) ambapo kazi yake kubwa ni ku-protect Chama cha Mapinduzi badala ya ku-protect nchi. Ukija kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi robo tatu utawakuta watu wa TISS wamevaa nguo za kijani, they are busy na Chama cha Mapinduzi. Tunazungumza hapa kuna mauaji, utekaji lakini ni kwa sababu wameacha mambo ya msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, in this country kila mtu anaweza akafanya jambo lolote. Jeshi linaweza likakusanya kodi na bunduki, leo tunakusanya kodi na bunduki (with guns). Hujui nani anafanya nini na kwa ajili ya nini ni kwa sababu nchi haina priority, poor leadership.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe ndugu zangu hebu tujipange Serikali ni ya kwenu, tuji-reorg, tujipange vizuri kwa sababu ni kama ubongo ambao uko scattered, you are every where, there is no priority. Mara tunaenda Dodoma, mara leo Bashite anakamata sijui watu gani, mara huyu ametumwa nini na kwa sababu hatuna priorities hatujui tunataka kufanya nini. Ni kama vile wataalamu hawapo katika nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatoa mawazo yetu lengo ni kuifanya Serikali yetu iwe nzuri. Tume-discourage fikra ambazo zina criticize kwa sababu hakuna mtu ambaye hawezi kuwa challenged katika ulimwengu huu. Kuwa challenged ni sehemu ya uongozi ili ujipime, sisi ni mirror yaani sisi ni kioo chenu huwezi kwenda kwenye kioo nywele hujachana unakipiga ngumi kioo sasa utajionaje, mnatupiga sisi sasa mtajionaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ni kioo chenu tunawaona hivyo mnavyofanya, wote mmekuwa waoga (terrified). Mawaziri wote mko-terrified hapo, Wabunge mkoterrified tukitoka huko nje ndiyo mnatuambia ee bwana lakini hapa mnasema kweli na wengine nikitoka nje mtaniambia
lakini humu ndani hamsemi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niombe Usalama wa Taifa wafanye kazi yao vizuri. Tumezungumza mauaji hapa sina muda wa kusema, baada ya Wabunge kusema kuna watu wako-tortured sana kule Mpingo wanafungiwa kwenye kachumba kadogo, wanakojoa humo humo, wanajisaidia
kwenye rambo wanateswa halafu wakionekana hawana hatia wanawadampo kwenye kituo cha mabasi pale wengine wako kwenye Jimbo langu toka Iringa wanaachwa na nauli tu. Hatuna muda wa kusema tu lakini haya mambo yapo watu wanakuwa totured tukisema hamtaki kusikia.