Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. IKUPA S. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuchangia machache katika Wizara hizi mbili. Awali ya yote, naomba niiungane na wenzangu ambao wametangulia kumpongeza sana Mheshimiwa Rais, kwa yale makubwa ambayo ameendelea kuyafanya. Pia tumeona mambo mengi yamefanyika ndani ya kipindi hiki cha mwaka mmoja. Kwa kweli napenda nimpongeze sana. Kwa ajili ya muda sitaweza kuyataja, lakini naomba tu pongezi zangu zimfikie mahali popote alipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Simbachawene na Mheshimiwa Waziri Angella Kairuki kwa hizi taarifa zao. Nimezipitia kwa ufupi na uchache, mengi yamefanyika, pongezi zangu ziwafikie.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja kwa moja naomba niongelee ile asilimia kumi ya vijana na wanawake. Naishukuru sana Serikali kwa kutenga hii asilimia kumi kwa ajili ya wanawake na vijana katika Halmashauri, lakini nina ushauri kidogo kuhusiana hii asilimia kumi na pia nimekuwa nikiongea mara kwa mara, naomba niweke msisitizo tena juu ya hii asilimia kumi. Naiomba Serikali na pia Wabunge wenzangu tuungane katika hili, kwamba hii asilimia kumi igawanywe, angalau basi hata asilimia mbili au hata kama ni asilimia moja iwe ni kwa ajili ya watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivyo? Kuna siku niliuliza swali, nikaambiwa kwamba hii asilimia kumi unaposema kwamba wanawake na vijana, inaaccommodate na watu wenye ulemavu, lakini kiuhalisia watu wenye ulemavu huwa hawapewi kipaumbele katika
hii asilimia kumi. Ni malalamiko ambayo tumekutana nayo hata katika ziara mbalimbali; ukifuatia kwamba je, hii asilimia kumi mnanufanika nayo vipi? Wanasema hapana, tunapofika pale tunaambiwa kwamba ni kwa ajili ya vijana na wanawake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe kwamba kuna watu wenye ulemavu ambao siyo wanawake na wala siyo vijana; nafiki hapo naeleweka. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali iliangalie hili; hii asilimia 10 igawanywe either iwe asilimia mbili kwa walemavu, halafu asilimia nne ibaki kwa
wanawake na asilimia nne ibaki kwa vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba niongelee takwimu za watu wenye ulemavu. Kiukweli Tanzania hatuna takwimu halisi. Yaani tunasemea tu kwamba kwa sababu ndivyo ambavyo inajulikana kwamba katika population duniani asilimia kumi inakuwa ni ya watu wenye ulemavu kwa
kila nchi, lakini tunatakiwa kuwa tupate uhalisia wa takwimu halisi za watu wenye ulemavu ili tuweze kupanga bajeti accordingly; kwa sababu sasa hivi tunabaki tu kama tuna hisia hisia, kwa hiyo hata ile bajeti yenyewe ambayo inatakiwa kwa ajili ya mambo fulani kwa ajili ya watu wenye ulemavu, inakuwa ni ngumu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaweza kufanyaje? Kupata takwimu yake, ni rahisi na ambayo inakuwa haina gharama ya aina yoyote. Kwa kuwatumia hao Wenyeviti wa Serikali za Mitaa; nirudie tena kusema kwamba mimi mwenyewe binafsi nimeshawahi kufanya hivyo, yaani ile
kuona kwamba hili jambo linawezekana? Nilimtumia Mwenyekiti wangu wa Serikali ya Mtaa nikamwambia naomba nifahamu, huu mtaa wako una watu wenye ulemavu wangapi? Ilikuwa ndani ya muda mfupi, yule Mwenyekiti akawasiliana na viongozi wake kwa maana ya Mabalozi, kila Balozi akaja na takwimu kwamba mimi katika nyumba zangu nina watu wenye ulemavu kadhaa. Kwa hiyo, mwisho wa siku yule Mwenyekiti akawa na takwimu sahihi kwamba watu wenye ulemavu nilionao kwenye Mtaa wangu ni watu kadhaa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho wa siku sasa hao Wenyeviti wanaweza wakawa wanakusanya zile takwimu wanapeleka kwa Wakuu wa Wilaya; Wakuu wa Wilaya wanazipandisha mpaka kwenye mikoa, hatimaye tunapata takwimu ya nchi nzima, kwamba watu wenye ulemavu wako wangapi, ambayo haitaigharimu Serikali gharama yoyote ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba niongelee suala zima la miundombinu kwenye shule zetu kwa maana kwamba shule za msingi mpaka shule za sekondari. Hapa naongea kwa sababu tunaongelea suala zima la inclusive education, tukiongela suala la inclusive education miundombinu bado siyo rafiki.
Kwa hiyo, naendelea kuiomba Serikali iendelee kuboresha hii miundombinu. Hapa naomba niipongeze sana Serikali kwa sababu kuna baadhi ya maeneo nimetembelea kwenye hizi shule za msingi na kuna fedha zimepelekwa kwa ajili ya kurekebisha ile miundombinu. Sasa kupelekea tu ile fedha, haitoshi; nafikiri wakati zile fedha zinapelekwa, pia liwe linatolewa agizo kwamba hii miundombinu inakarabatiwa. Pia mnapokuwa mnafanya ukarabati, mzingatie mahitaji ya watoto wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika kila shule itakuwa ni vizuri sana kukiwa kuna choo ambacho kinaweza kumsaidia mtoto mwenye ulemavu kujisaidia kwa urahisi. Kwa sababu wakati nafanya hizi ziara, nilijaribu pia kuangalia miundombinu ya vyoo. Miundombinu ya vyoo siyo mizuri
kabisa ukiangalia kuna ulemavu mwingine mtu anakuwa anatambaa chini, sasa ukimchanganya, kwamba aende kwenye vyoo vya public na watoto wenzake, inakuwa ni shida sana. Kwa hiyo, naiomba Serikali izingatie hilo pia kwamba hata kama ule ukarabati wa jumla utakuwa labda unachukua gharama kubwa, lakini pia suala la choo lingeanza, ingekuwa nzuri zaidi kwamba angalau kila shule ipate choo ambacho kitamsaidia mtoto mwenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumalizia, naomba niongelee suala la TASAF. Naipongeza sana Serikali kwa jinsi ambavyo imefanya. Kweli katikati wakati niko kwenye ziara zangu, watu wenye ulemavu walizungumzia sana suala la TASAF kwamba wao wamekuwa wakiachwa na badala yake wanakuwa wakiwekwa watu ambao wana uwezo wao kabisa. Kwa hiyo, naipongeza Serikali, lakini pia naomba katika zile qualifications za kuingizwa kwenye huu mfumo wa TASAF, pia suala la ulemavu liangaliwe kwa maana kwamba ule ulemavu ambao mtu anakuwa hajiwezi kabisa, anakuwa ni maskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mmoja amekuwa akinisumbua sana hata sasa hivi, anasema kwamba yeye hana uwezo; nikajaribu kumwambia kwamba hebu basi awasiliane hata na Mwenyekiti Serikali za Mitaa, anaweza akamsaidia kwamba aanzie wapi au jinsi gani anaweza akaorodheshwa kwenye huu mpango; anasema hapana, hawa watu wanapeana, unakuta sisi ambao tunakuwa tuna shida, tunaachwa, wanapeana watu ambao hawana shida. Kwa hiyo, pia naomba Serikali iliangalie sana hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi, naomba kuunga mkono hoja.