Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Kipekee, kwanza kabisa kabla ya kuzungumza, nawashukuru sana wananchi wangu wa Jimbo la Arumeru ambao wamenivumila kwa kipindi chote ambacho nilikuwa masomoni nchini Uingereza mpaka sasa
ambapo nimerejea kuja kuendelea na kazi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, dunia inazunguka kwa kasi sana. Kwa nini nasema hivyo? Leo kwenye Bunge hili, Mawaziri wanatuambia tusizungumze habari ya kugusa wala kujadili habari ya Usalama wa Taifa letu. Kwenye mkono huu, ninayo barua hapa yenye kurasa saba iliyoandikwa na aliyekuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, leo hii ni Waziri wa Habari, Mheshimiwa Dkt. Harrison George Mwakyembe. Barua hii
imeandikwa tarehe 9 Februari, 2011. Kwenye barua hii Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe alikuwa anatuhumu baadhi ya watu wakiwemo watu wa Utumishi wa Usalama wa Taifa kutaka kuchukua maisha yake; kutaka kumteka ama vitendo ambavyo vimekuwa vikiendelea kwenye Taifa hili.
Usipoguswa, huyasikii maumivu; ukiguswa unayasikia maumivu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu umesema tusizungumzie habari ya Usalama wa Taifa nitaiacha ila nitaendelea kujadili hotuba hii nikizingatia utaratibu uliofanywa na watu ambao ni wakubwa kwenye Serikali yetu akiwepo mwalimu wangu Mheshimiwa Dkt. Harison
Mwakyembe.
Mheshimiwa Naibu Spika, habari ya usalama naiweka pembeni, lakini kuonesha namna gani dunia inakwenda kwa kasi, ni Mheshimiwa Dkt. Harisson Mwakyembe huyu huyu Waziri wa leo; mwaka 2008 aliongoza Kamati Teule ya Bunge hili Tukufu ambayo ilijadili suala la Richmond. Katika suala lile hakusikiliza upande wa pili kwa maana ya aliyekuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Edward Lowassa, akasikiliza upande mmoja akatoa ripoti kwenye Bunge hili ambayo ilipelekea Mheshimiwa Lowassa kuachia ngazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwakyembe huyu leo amepokea ripoti ya aliyekuwa Waziri kwenye Wizara yake Mheshimiwa Nape yupo hapa; upande wa pili kwa maana ya Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam aliyekataa kuhojiwa, akakimbia kwa mlango wa mbele wakati
amewatuma watu kwa mlango wa nyuma. Leo Mwakyembe anasema ripoti hii haija-balance stori kwa hiyo siwezi kuifanyia kazi. Mwakyembe hiyo balancing of the story ya Mheshimiwa Lowassa na kuachia ngazi uliitoa wapi? Hukumsikiliza Lowassa alikuwa Waziri Mkuu hapa.
Taarifa...
Namheshimu sana mwalimu wangu Dkt. Mwakyembe lakini naomba nimkumbushe pia kwamba taarifa yake siipokei kwa sababu zifuatazo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ya kwanza; ni Profesa ama Dkt. wa kwanza wa PhD kwenye nchi hii ambae aliandika thesis yake ya PhD iliyoonesha ili taifa hili liende mbele lazima kuwe na Serikali tatu na tena wakati wa Bunge la Katiba alikataa thesis yake mwenye hapa ndani ya Bunge hili; mimi nilikuwa Mbunge hapa, huyo hapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru lakini naomba tu niweke upepo sawa; sina shida na mwalimu wangu Dkt. Harrison Mwakyembe napenda sana amenitoa kwenye ujinga; lakini ukweli ni kwamba nilikuwa naikataa taarifa ya Dkt. Harrison Mkwakyembe kwa kutumia reference and the kind of reference I used was his own thesis. Sasa kama mimi natumia reference ya andiko ambalo ameliandika yeye mwenyewe kwa miaka; ninyi mnataka mtu atumie reference gani jamani, mnataka nitumie Mwanahalisi ya Kubenea, Mwananchi au Tanzania Daima? Natumia reference ya alichokiandika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mnapeleka wapi Bunge ninyi watu? Muda wangu tafadhali.
Mheshimiwa NaibuSpika, mimi nimepata nafasi ya kusoma ya kwenye nchi za Magharibi, nchi za Amerika, Ulaya na nchi za Asia, zilizoendelea. Katika kipindi cha miezi tisa iliyopita nimekaa nje ya siasa za Kitanzania, siasa za Kibunge kwa hiyo nimezitazama nikiwa niko nje ya siasa za nchi hii. Nimeona siasa zinatia kichefu chefu; ukiongea ukweli kama huu unakandamizwa. Leo wewe asubuhi ameongea Mzee
Bulembo hapa, kwenye mchango wake hapa amemsema Mbunge wa Siha Dkt. Mollel wa CHADEMA mbona hamjamzuia?
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimepewa taarifa nakataa taarifa with a reference wewe ni mwalimu wa sheria unajua huyu ni mwalimu mwenzako wa sheria kwa nini unaikataa taarifa yangu kukataa taarifa yake?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuthibitishie kwamba nilipoziangalia siasa za nchi yetu kutoka nje niliona ujinga ufuatao:-
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza; ni mara ya kwanza kwenye historia ya siasa za dunia unamuona mtu mwenye cheo kama cha Ukuu wa Mkoa anavamia kwenye media house tena si media house anaingia kwenye production room akiwa yupo full armed. Mahali pekee kwenye dunia unaona kiongozi mkubwa wa ngazi hiyo anaingia kwenye media house tena production room akiwa na watu wapo full armed na silaha. Kuna mambo mawili; la kwanza ni jaribio la Mapinduzi na la pili ni Mapinduzi yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, Taifa liko kimya, watu wamezungumza hapa; ni mara ya kwanza tunakuta maiti zipo Mto Ruvu watu saba wameuawa zimefungwa kwenye viroba halafu mnasema Bunge lisijadili, mnatetea akina nani kwenye nchi hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni mara ya kwanza kwenye nchi Mbunge anawekwa ndani miezi minne mfululizo. Mimi nimeondoka Arusha nimemuacha Lema yupo magereza; mwezi wa Kumi na Moja nimekuja kumtembelea. Nimeondoka nimerudi, nimemaliza masters yangu;
nimemaliza semester mbili namkuta Mbunge bado yupo ndani kwa sababu Hakimu amefungwa mikono ya kutoa masharti ya dhamana, si dhamana. And you want us to stay quiet?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni Tanzania pekee ambayo Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Shija Lutoja Alexander Pastory Mnyeti ameingia, Madiwani wametengeneza Bajeti ya Halmashauri kwa mujibu wa sheria, wameipitisha. Bajeti ya Halmashauri inajadiliwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama na inaamua kupeleka bajeti mbadala; mmewahi kuona wapi ninyi? Ni mara ya kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimempokea Waziri Mkuu; nipo masomoni Uingereza tunatumiana email anakuja Mkoani kwetu muungwana, Mheshimiwa Waziri Mkuu Majaliwa huyu. Nimekuja kumpokea nimepanda ndege kwa gharama zangu sijalipiwa na Bunge kuja kumpokea; namwambia issues za wananchi ananiuliza tufanye nini Mheshimiwa Nassari? Namwambia ni hili la ardhi na hili na hili; ametoa maelekezo Waziri wa Ardhi aje Jimboni, nikampongeza, mnakumbuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Ardhi amekuja tunakwenda kwenye mkutano wa hadhara wenye matatizo ya wananchi; wananchi waje na mabango na makaratasi, Lukuvi ameagiza. Wanakuja Mkuu wa Wilaya anaongea jukwaani baada ya kuongea hatambui uwepo wa Mbunge, anamuita Waziri jukwaani. Namshukuru ndugu yangu Lukuvi alikataa, he refused. Alisema hapana, hili Jimbo linaye mwakilishi wa wananchi; azungumze kwanza mimi Serikali nitajibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, utawala bora uko wapi? Yaani bajeti ya Halmashauri inajadiliwa kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama; wale wanajeshi wanajuaje wanajuaje kwamba wananchi wa kata 25 za Jimbo langu hawana vyoo, how do they know? Tunaongea, wanatoa miongozo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara ya kwanza kwenye nchi, first time in the history of this country, Bunge linafanya kazi likiwa limeingiziwa hofu. First time in the history of this country, Bunge linatukanwa halafu unataka nikae kimya? Walisema waliotangulia Bunge linapaswa kulindwa kwa wivu wa hali ya juu. Leo unatoa mwongozo hapa kwamba Wabunge wasiguse Usalama wa Taifa; ni kweli sitaugusa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nikukumbushe mwalimu wangu wa sheria; ulimfundisha mke wangu sheria. Nchi hii ina mihimili mitatu; mhimili wa Bunge unasimamia mhimili wa Serikali; Kitengo cha Usalama wa Taifa nchi hii kipo chini ya executive, kinasimamiwa na Bunge.
Vitu ambavyo hatuwezi kujadili kwenye Bunge hili ni nchi ina mizinga mingapi, ina vifaru vimekaaje na vimeangalia kushoto au kulia, lakini habari ya kujadili Waziri kama Nape anatolewa bastola mbele ya kamera za waandishi wa habari, we cannot stay quiet, are you kidding us?
Mheshimiwa Naibu Spika, Taifa linafika hatua vituo vya redio vinavamiwa usiku saa sita na unataka Wabunge tukae kimya? Leo Mfuko wa Jimbo wa Mbunge unaingiliwa na Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya ndiye nayeamua kwamba miradi gani ipewe pesa wakati Sheria ya Mfuko wa Jimbo imesema an MP keeps records.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo asubuhi, nimeumia sana hapa ndani. Kwa historia za Kiafrika mtu mwenye uchungu na watoto, mtu mwenye uchungu na mtu yeyote; kwa sababu kila aliyekaa hapa ndani ni mtoto wa mama, kila aliyekaa hapa ndani ni mtoto wa mwanamke, yeyote, awe na miaka 90 au miaka 80; wenye uchungu na watoto ni akinamama, ni wanawake, bila kujali vyama vyao. Leo asubuhi hapa mama anaongea habari ya watu kutekwa…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
NAIBU SPIKA: Muda wako umekwisha.