Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana. Kwanza, wiki iliyopita kwa siku mbili mfululizo nimetuhumiwa kuwa nabebwa na kiti chako kuwa natumia nafasi yangu vibaya, kwa hiyo naomba; unapopata tuhuma kama hizi, ninapopata nafasi kama hii inabidi na mimi nijitetee kwa nafasi yangu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ulifanyika uchaguzi wa Wabunge la Afrika Mashariki. Wajumbe walioletwa kutoka upande wa CHADEMA walipata kura nyingi za hapana; lakini naomba nifafanue kupitia mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (The Treaty For The Establishment of East African Community 1999) ambao umekuwa Revised mwaka 2006, Article 50; Election of Member of the Assembly namba moja, inasema hivi "The National Assembly of each Partner State….
KUHUSU UTARATIBU....
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba muda wangu ulindwe, Mheshimiwa dada yangu Halima Mdee amesahau kumalizia Utawala Bora. Naomba niendelee.
Mheshimiwa Naibu Spika, Article 50, election member of Assembly inasema hivi:- “The National Assembly of each partner state shall
elect…”
Mheshimiwa Naibu Spika, wewe ni shahidi kuwa CCM tulikuwa tuna nafasi sita, tulileta watu kumi na mbili. Najenga hoja, najenga hoja nimetuhumiwa.
T A A R I F A....
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Alipokuwa anaelekea Mheshimiwa Nassari ndiyo huko huko ndio nilikuwa naenda. Kifungu namba moja kinasema hivi; a partner state shall elect assembly, yaani kwa Kiswahili Bunge la nchi mwanachama
litachagua. CHADEMA mlichagua huko hapa mlileta tu-approve, hapa tofauti ni lugha. Ndiyo maana nasema CHADEMA mna Wanasheria wengi, lakini hao Wanasheria wanashinda mahakamani kuwatetea watu ambao wanamtukana Rais badala ya kuwasaidia nyinyi humu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ambalo lilipigiwa kelele ni suala la gender. Katika hicho hicho kifungu namba moja ukiendelea kukisoma mbele kimezungumzia gender, interest groups. Nikauliza ninyi mtuambie, mnatulaumu sisi hatujachagua hii kanuni mlisoma? Imezungumzia gender, nikawaambia mniambie kati ya Masha na Wenje nani alikuwa anawakilisha hizo gender? Mmekataa kusema, matusi yangu yako wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nasema hivi tuwe tunaangalia viongozi tunaowachagua, wakati sisi tunachagua Mwenyekiti wetu wa Chama wa PhD, ninyi mlichagua Mwenyekiti wenu wa Chama form six zero.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala langu la pili, naomba niishukuru Serikali kwa uje…
KUHUSU UTARATIBU....
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba muda wangu ulindwe, nimesema sisi wakati tunachagua Mwenyekiti PhD holder wao
walichagua form six zero, sijasema wao nani.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa sababu nilisha-declare humu ndani kuwa yule ni baba mkwe wangu naomba niyafute hayo maneno.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende upande wa Jimbo langu la Ulanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nafasi ya pekee niishukuru Serikali kwa ujenzi wa Daraja la Kilombero. Kwa Waheshimiwa Wabunge ambao
mmeshatembelea lile Jimbo la Ulanga mliuona ule Mto Kilombero, limetusaidia kwa kiasi kikubwa sana. Watu walikuwa wanakufa upande wa pili huku wakiiona hospitali ipo upande wa pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa namna ya pekee kabisa, shukrani za pekee kutoka kwa wana Ulanga. Naiomba Serikali ijaribu kutusogezea kipande cha lami kutoka Kilombero mpaka Mahenge Mjini, hiyo itakuwa imetusaidia sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mvua zinanyesha, kwenye Jimbo langu la Ulanga tumekumbwa na adha kubwa ya mafuriko, madaraja yamebomoka, hamna mawasiliano kutoka Kata moja kwenda nyingine. Naiomba Serikali kwa jicho la pekee walitazame Jimbo la Ulanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Walimu. Serikali ilisimamisha kupandisha madaraja Walimu kwa muda mrefu kwa ajili ya kupisha uhakiki, maajabu yangu yanayokuja, kuna Walimu wamekaa miaka kumi na mbili hawajapandishwa madaraja. Leo hii Serikali imekuja na uamuzi kuwa Mwalimu hawezi kupandishwa daraja mpaka aende mafunzo. Hao waliokaa miaka kumi na mbili wakisubiria kupandishwa madaraja haijatoa mwongozo watawafanyaje? Wengine wanakaribia kustaafu na wamefanya kazi muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu, katika Jimbo langu la Ulanga wananchi wamejitolea hasa Kata ya Ilagua wamejenga shule wameweka watoto wanasoma, wenyewe wazazi wameajiri Walimu, lakini Serikali mpaka leo hii wameshindwa kuzisajili hizo shule. Naomba Serikali kwa fursa ya pekee kabisa muwasapoti wananchi wa Ulanga kwa kuzisajili shule hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la nne, katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga Wakuu wa Idara wengi wanakaimu, hii inachelewesha maamuzi. Kwa hiyo, naomba Utumishi kwa kushirikiana na TAMISEMI, mfanye mchakato wa haraka hawa Wakuu wa Idara wathibitishwe ili kutochelewesha maamuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala langu la tano; katika historia yangu ya maisha nilimsikia mtu mmoja marehemu aliyekuwa anaitwa Kombe. Kombe kwa nilivyosoma kwenye vitabu ni kwamba alipigwa risasi na watu, Maofisa wa Serikali; lakini kwa macho yangu nimeshuhudia hivi karibuni Waziri mstaafu na Katibu Mwenezi Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi alitolewa bastola hadharani, bila kificho na watumishi wanaosadikiwa kuwa ni wa Serikali. Nilitegemea Mheshimiwa Waziri Mkuu atatoa kauli, Mawaziri mtatoa kauli, Wabunge mtatoa kauli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa basi, kama yule Waziri mstaafu ametolewa bastola hadharani Serikali ikakaa kimya, leo hii tutakuwa na uhakika gani hawa wanaoua maaskari si Watumishi wa Serikali?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie kwa kusema hivi; Waheshimiwa Wabunge tuwe tunaangalia vitu vya kutumia kabla
hatujaingia humu Bungeni. Kuna Wabunge wameingia wamelewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina ushahidi Mheshimiwa Nasari ameingia na Konyagi amezuiliwa hapo getini na mpaka saa hizi amelewa.
Naomba tuangalie vitu vya kutumia kabla hatujaingia humu ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.