Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema na uhai. Vilevile napenda kukishukuru chama changu kwa kunipa nafasi ya kuendelea kuwepo katika Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nielekeze mchango wangu kwenye Wizara hii ya TAMISEMI. Wizara hii kwa kweli ndiyo nchi, ndiyo inayoangalia Taifa zima la Tanzania hasa kwa upande huu wa Bara. Kwanza kabisa, nijielekeze kwenye mpango mzima wa elimu. Katika hotuba ya Waziri wa TAMISEMI, ukurasa wa 23 unaongelea miundombinu. Kwa kweli bado miundombinu katika elimu yetu siyo mizuri kwani upungufu wa miundombinu ni mkubwa sana. Kwanza nijielekeze kwenye upungufu wa vyoo.
Niliangalia kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri aliongelea kuhusu upungufu wa matundu ya vyoo kwa kweli bado ni tatizo kubwa. Sasa kama mpaka sasa hivi tunaongelea upungufu wa matundu 517,600 kwa ujumla wake lakini nikiangalia kabisa upungufu huu 50% upo katika Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na mlundikano mkubwa wa wanafunzi. Vilevile upungufu huu wa vyoo unafanya wanafunzi wetu kwanza wasome in uncomfortable way halafu vilevile unasababisha magonjwa makubwa hasa UTI.
Sasa hivi ratio kwa Mkoa wa Dar es Salaam kwenye tundu moja inaenda kati ya wanafunzi 80 - 100 wanatumia tundu moja la choo katika shule zetu za msimngi. Sasa nijiulize, haya magonjwa kama ya UTI hasa kwa upande wa wanafunzi wa kike yataisha? Hayawezi kwisha. Tunatumia gharama kubwa sana za matibabu ya UTI na kusababisha watoto kutokusoma kabisa.
Mheshimiwa Spika, lakini vilevile niende kwenye vyumba vya madarasa, nako kuna upungufu wa takribani 200,000 na kwenye nyumba za walimu 182,000. Takwimu hizi bado ni kubwa sana, vyumba vya madarasa kwa sasa yaani ni issue. Huu mpango wa elimu bure umesababisha darasa moja sasa liwe na wanafunzi kati ya 200 - 400 hasa kwenye Mkoa wa Dar es Salaam. Mimi naomba kabisa Serikali ije na mkakati wa kupunguza huu uhaba wa madarasa hasa kwenye Mkoa wa Dar es Salaam na Tanzania nzima kwa ujumla, yaani itueleze kabisa itafanyaje? Kama haiwezekani basi Halmashauri zipewe uwezo yaani kusimamiwa ili zikope zianze utaratibu huu wa kujenga vyumba vya madarasa kama ilivyokuwa kwenye madawati. Madawati tumeona kabisa sasa hivi yameenda vizuri mpaka Bunge lenyewe
limechangia madawati, basi sasa sera ya madarasa na matundu ya vyoo ianze upya, tuendelee kabisa kusema kwamba, sasa hivi katika kila wilaya na mkoa lazima huu upungufu wa vyoo na vyumba vya madarasa uishe.
Mheshimiwa Spika, lakini vilevile niongelee uhaba wa walimu. Uhaba wa walimu bado ni tatizo hasa walimu wa hesabu na sayansi kwa ujumla. Kulikuwa na ile programu ya walimu kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma, imeingiliwa, ikavurugwa vurugwa, hatuelewi walimu wale wanamaliza
lini au wataajiriwa lini au itakuwaje. Kwa hiyo, uhaba wa walimu pia ni tatizo hasa katika upande wa masomo haya ya sayansi na hisabati.
Mheshimiwa Spika, nije kwenye masuala ya afya niongelee suala la kujenga Hospitali za Wilaya hasa kwenye wilaya hizi mpya. Kwanza tukiangalia kwenye Mkoa wa Dar es Salaam kuna tatizo kubwa la mlundikano wa wagonjwa hasa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Ilala na Amana.
Kuna hizi Wilaya mpya za Kigamboni na Ubungo ambazo mpaka sasa hazina hii huduma kabisa ya Hospitali ya Wilaya. Naomba Waziri wakati anapokuja kuhitimisha atueleze atajenga lini Hospitali za Wilaya kwenye hizi Wilaya mpya ikiwemo Ubungo na Kigamboni ziwe au zilizopo zipandishwe mfano Hospitali ya Mbezi. Vilevile Hospitali za Ilala, Temeke, Mwananyamala zimepandishwa kwenda kwenye hadhi ya mkoa sasa Hospitali za Wilaya ziko wapi? Kwa hiyo, namuomba Waziri katika vipaumbele vyake kuwe na Hospitali za Wilaya kila wilaya na ziwe na vifaa vyote muhimu vya afya ikiwemo magari ya wagonjwa, labor zinazoeleweka, vifaa vya kujifungulia ili huduma za afya ziwe sahihi kabisa.
Mheshimiwa Spika, nije katika ujenzi wa majengo ya ofisi katika wilaya. Bado ofisi za wilaya hazina ule mwonekano wa majengo ya Wilaya hasa kwa wilaya mpya. Hivi inakuwaje unaigawa Wilaya halafu unaenda kukodi jengo kwenye majengo ya mtu binafsi? Basi hayo majengo
ya watu binafsi yangekuwa angalau yana nafasi kubwa lakini sivyo. Sasa sasa hivi wilaya hizi zimekuwa kama kitu cha ajabu, hazina majengo yanayoeleweka hasa Wilaya mpya mfano Kigamboni au Ubungo. Unakuta chumba cha 10 kwa 10 kina idara zaidi ya tatu mpaka tano. Mkuu wa Idara yuko humo humo, wafanyakazi wa kawaida wako humo humo kwenye hicho chumba yaani ni vurumai hata mafaili huwezi
kujua yanakaa wapi. Kwa hiyo, mimi naomba kabisa hasa kwenye hizi Wilaya mpya, kwa mfano Wilaya ya Ubungo na Kigamboni, Waziri anapokuja kuhitimishia atueleze majengo haya yatajengwa lini na kama anaendelea kukodi atakodi kwa muda gani? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba sasa niongelee maslahi ya watumshi. Kwa kweli maslahi ya watumishi katika ngazi ya utumishi wa umma kwa kweli bado ni tatizo. Mishahara ni midogo, mmeendelea kupunguza posho, zingine mmeziondoa kabisa, stahiki kwa viongozi pia hazieleweki.
Mnasema kwamba mnakuja kuleta uwiano wa mishahara kwa kuangalia ile mikubwa na kima cha chini, lakini sasa mbona huu mshahara wa kima cha chini hauangaliwi kabisa? Kwa muda mrefu mshahara wa kima cha chini umekuwa mdogo sana. Wafanyakazi wa umma sasa
imekuwa taabu yaani wanafanya kazi kwa mshahara mdogo, hawapandishwi madaraja yaani totally wamekuwa confused, wamekata tamaa hata ya kuwa watumishi wa umma. Madaraja yao hawapandishwi mnasema sasa hivi kwanza tunahakiki, lakini kuhakiki kunazuia mtu kupanda daraja? Inakuwaje mtu miaka mitatu hupandi daraja?
Mheshimiwa Spika, mimi mwenyewe hapa ni-declare interest nilikuwa mtumishi wa umma, nimekaa miaka karibu mitatu sijapandishwa. Naomba suala hili liangaliwe upya. Mtu mpandishe cheo kutokana na elimu yake na anavyoweza kufanya kazi. Bila kumpandisha madaraja hii motive ya kufanya kazi mtu ataipata wapi?
Mheshimiwa Spika, lakini vilevile pia tuangalie mishahara yao bado ni midogo mno. Halafu posho zao nyingi mmezikata yaani hazieleweki. Kama mnakata posho basi muangalie ule uwezekano na maisha halisi ya mtumishi wa umma inakuwaje.
Mheshimiwa Spika, vilevile kumekuwa na mlundikano wa kazi kwenye ofisi hizi za umma kutokana na kutoajiri watu. Vijana wamejaa huko mtaani hawaajiriwi na kazi zimerundikana huku. Hawa watu mmewaondolea hata posho za mazingira magumu lakini mlundikano wa kazi
umezidi kwenye ofisi za umma kwa idara zote hasa Halmashauri yaani unakuta kazi ya watu 10 anafanya mtu mmoja. Vilevile overtime, extra-duty allowance, zote zimeondolewa huyu mtu anafanyaje kazi? Kwa hiyo, naomba kabisa muangalie tena suala hili.
Mheshimiwa Spika,
nakushukuru.