Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kwa kunipatia hii nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kuwapongeza Mawaziri wote waliowasilisha bajeti zao na kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya, kwa kweli hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna kila sababu ya kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano na hiyo ndiyo kazi yetu kubwa na sababu kubwa ambazo zinafanya tuipongeze ni mambo makubwa ambayo imefanya katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu; katika mwaka mmoja na nusu huu mambo makubwa yameonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kabisa jinsi nchi hii ambavyo sasa tunaibadilisha, kwa kweli hii tunajivunia sana. Lakini hii imeonesha dhahiri namna ya kupambana na rushwa katika nchi hii ambayo ilikuwa ni kikwzo kikubwa sana katika maendeleo yetu ya nchi, kwa kweli hii tunaipongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia imeonesha namna ya kupambana na dawa za kulevya, ni lazima tuziunge jitihada hizi kwa hali na mali ili kuhakikisha kwamba tunairekebisha nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo naomba nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwanza kwa kuanzisha rasmi mkoa wa Songwe, tunawashukuru sana tena sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia naomba niipongeze Serikali katika mambo ambayo yalishindikana miaka mingi yameweza kutekelezeka, suala la elimu bure, lakini suala kubwa zaidi na ambalo hatutalisahau kwenye historia, ni suala la kuhamia Dodoma. Serikali yote imehamia Dodoma. Tumeimba miaka mingi sana, lakini sasa Serikali hii imeonyesha dhahiri kwa vitendo ndani ya mwaka mmoja na nusu Serikali karibu yote imehamia Dodoma na mimi naamini na ninamshauri Mheshimiwa Rais ahamie na yeye mapema kabisa kuliko ile ratiba tuliyoitoa. Kwa kweli tunawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali imefanya mambo mengine makubwa, tumeona kabisa tumeanza kujenga reli kubwa ya kati (standard gauge), reli ambayo tulikuwa tunaimba tu kwa muda mrefu. Hii itachangia katika kuongeza na kupanua uchumi wetu. Kubwa zaidi tumeweza kununua ndege ambazo hazikuwepo. Sasa tunalifufua Shirika letu la Ndege, haya ni mambo makubwa ambayo yamefanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali. Kwa Jiji la Dar es salaam tumeona, tulikuwa hatujawahi kuona flyover Dar es Salaam; sasa flyover zinaanza kujengwa. Sasa tunataka nini zaidi? Ni mwaka mmoja tu na nusu yote haya yameonekana. Kwa hiyo, tunaipongeza sana Serikali kwa yote haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie masuala ya utawala bora. Masuala ya utawala bora nashangaa! Tusiyaangalie katika upana mdogo, tuyaangalie masuala ya utawala bora katika uwanja mpana sana. Masuala ya utawala bora yana mambo mengi. Kwanza kuna misingi ambayo tunaita ni misingi ya utawala bora, misingi ambayo ipo na misingi hii imewekwa kwenye Katiba, imewekwa kwenye mihimili yetu mitatu. Utawala bora ni jinsi ninyi mnavyoliongoza Bunge, mnavyozingatia kanuni, sheria, yote hayo ni utawala bora. Jinsi Wabunge tunavyochangia hapa ndani na watu wanavyochangia mawazo, ni utawala bora, jinsi Mahakama zinavyofanyakazi, ni utawala bora na jinsi Serikali inavyotenda kazi ni utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Serikali duniani inayoweza ikafanya 100 percent, upo upungufu mdogo mdogo, lakini mambo ya msingi yanakwenda lazima tuyafurahie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utawala bora una mambo karibu kama nane hivi ambazo tunaita pillars za good governance. Kuna uwazi, uwajibikaji, demokrasia, ushirikishwaji, Serikali sikivu, kuna utawala wa sheria, kuna ufanisi na tija na kuna haki na wajibu. Haya yote yanasimamiwa vizuri na Serikali yetu. Sasa wapi kuna tatizo? (Makofi)
Mambo yanakwenda!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia sasa hivi uwajibikaji ndani ya Serikali ni mkubwa, ukiangalia tunavyopambana sasa na kuondoa wale wote wenye vyeti hewa ni mapambano mazuri, ni uwajibikaji, ni utawala bora, tunapojenga nidhamu ya utumishi ni utawala bora. Sasa tunataka nini zaidi ili tuseme utawala bora upo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mengine tunayoyasema, dosari ndogo ndogo zipo. Hata mtawala Lee Kuan Yew, Baba wa Taifa wa Singapore, alisema hakuna mtu anayeweza akawa 100 percent perfect na hakuna njia sahihi duniani. Sisi tumeamua kuendeleza nchi, tutaendeleza, tutakwama, tutarudi nyuma, lakini tutasonga mbele, maadamu dhamira yetu iko pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tushirikiane, tuiunge mkono Serikali yetu jinsi ambavyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake. Yapo masuala machache labda niseme madogo yanayohusu wachache wanaokwamisha utawala bora.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, sasa hivi labda niseme, kule Jimboni kwangu Vwawa, hivi tunavyoongea leo tunachangia Wizara ya TAMISEMI. Eti nao Mwenyekiti ameitisha vikao vya Madiwani kule leo, nao wanaendelea eti wanaitisha vikao. Sasa Serikali ilishaelekeza, vikao vya Madiwani vitenganishwe na vikao vya Bunge. Mtaitishaje vikao hivyo? Kwa nini hayo yanafanyika? Yanafanyika kwa sababu ya maovu machache ambayo wanayafanya wengine, wanataka Waheshimiwa Wabunge tusishiriki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Jimboni kwangu kuna matatizo mengine makubwa na hapo naomba Serikali ichukue hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tume ziliundwa kuchunguza upotevu wa fedha zaidi ya mwaka mmoja hazijatoa majibu. Hiyo inakuwa ni dosari, hebu rekebisheni hayo. Pale kwetu kuna shilingi milioni 450 zimeenda kwenye miradi, watu wakagawana. Kuna shilingi milioni 680 za mradi wa maji Harungu, watu waligawana wakafanya uongo uongo, maji hayapo. Kuna shilingi milioni 320 za maji ya Ihanda, maji hayapo, wananchi wanahitaji maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ubadhirifu mwingi! Shilingi bilioni 1.8 yamefanyika Mbozi, hebu tupieni jicho angalieni Wilaya ya Mbozi, angalieni yanayoendelea mchukue hatua ili wananchi waendelee kuipenda Serikali yetu na wakipende Chama cha Mapinduzi na mimi naamini haya yanawezekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hizi naomba sana mtusaidie, kule tunahitaji maji. Kuna vijiji kama kijiji cha Iyula, Kijiji cha Iyula B, Vijiji vya Idiwiri, Igale, Nanyara, Senjere, vinahitaji maji. Huu mradi ulifanyiwa upembuzi yakinifu kwa muda mrefu haujatekelezwa. Tunaomba tusaidieni ili tuweze kuinua mazao mbalimbali likiwemo zao la kahawa tunaombeni sana hilo mtupe ushirikiano. Pia kuna mradi mwingine wa kutoka vijiji vya Lukururu, Mlangali, Mlowo ambao ungesaidia kuimarisha maji katika vijiji kama 14. Naombeni sana hilo mtusaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Mji wa Vwawa pale pana shida ya maji, Makao Makuu ya Mkoa, hebu tusaidieni haya yaishe. Naomba pia sasa hivi kwa kuwa mmetupa Mkoa, naamini Mheshimiwa Waziri unanisikiliza vizuri kwamba umetupa Mkoa na nimewashukuru, sasa mtatupa na Manispaa ya Mkoa wa Songwe ambayo itakuwa Manispaa sijui ya Jimbo la Vwawa au ya Mbozi, yoyote ile. Tunaiombeni hiyo haraka ili tutekeleze majukumu yetu vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba kwenye ule Mkoa barabara za mkoa; barabara ambayo itaunganisha Wilaya ya Mbozi na Wilaya yetu mpya ya Songwe. Tunaomba ile barabara mtupe, mtusaidie ili tuweze kuitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda suala la afya, kwenye Wilaya ya Mbozi wananchi wamejitahidi sana, wamejenga maboma, wamejenga zahanati, wamekamilisha wanahitaji wafanyakazi, wanahitaji dawa, hayo hayafanyika mpaka sasa hivi. Hebu tuungeni mkono, jitahidini kutuletea watumishi wa afya ili angalau tuweze kukamilisha na wananchi wawe na imani kwamba sasa mambo yanakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo ningependa nilizungumzie ni suala la ripoti ya Mkaguzi wa Nje (CAG). Nimeshangaa watu wengi wanaongelea sana hii CAG report. CAG report naomba Kamati maalum za kufuatilia…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nashukuru sana kwa nafasi hii.