Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa Mungu kwa kuniwezesha kunipatia muda huu wa kuchangia ndani ya Bunge lako Tukufu angalau kwa maandishi. Nipende kumpatia hongera sana Mheshimiwa January Makamba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa kazi nzuri anayoifanya, pamoja na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uharibifu wa mazingira na hasa matumizi ya mkaa. Nchi nzima wananchi karibu asilimia 80 wanatumia mkaa na kuni kama chanzo cha nishati. Pamoja na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na ujenzi Serikali ni vyema isimamie kikamilifu kuhusu uharibifu wa mazingira haya la sivyo nchi itakuwa jangwa. Mheshimiwa Waziri ni vizuri atoe tamko na kukumbusha tena wananchi na viongozi husika, kuhusu kusimamia Sheria ya Mazingira. Ni ukweli miti inapandwa, ambayo, miche 1.5 milioni kila halmashauri inapandwa, tatizo ufuatiliaji wa kuona ni mingapi inaendelea kukua kila mwaka baada ya kupanda ni tatizo, ingekuwa vizuri ufuatiliaji wa miche inapoendelea kukua ukajulikana badala ya kujali kufahamu takwimu za upandaji tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mkaa ni vizuri likaangaliwa kwa undani, ni nini kifanyike kunusuru uharibifu unaojitokeza, ukataji miti kwa kibali uendelee kusimamiwa kwa muda wote na viongozi husika. Elimu kwa wananchi izidi kutolewa kuhusu utunzaji wa mazingira. Bado uharibifu wa vyanzo vya maji unaendelea licha ya mikakati yote ya Serikali ya kukabiliana na tatizo hili, ni vyema Sheria ya Mazingira ifuatwe na kusimamiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uharibifu wa vyanzo vya maji unasababisha uhaba wa maji, mabadiliko ya tabia nchi, upungufu wa rutuba ya ardhi na matatizo mengi zaidi ya uharibifu wa ardhi. Uharibifu wa vyanzo vya maji na mazingira kuhusu milima ya Uluguru Mkoani Morogoro, wataalam wa SUA wamejitahidi katika mapando ya kuhifadhi milima hiyo lakini tatizo bado lipo pale pale. Kilimo kisichokuwa na tija na ujenzi wa nyumba kama makazi ya wananchi vinaendelea katika milima hiyo, vyanzo vya maji vimekauka kiasi wananchi wa Morogoro Manispaa hawapati maji ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Serikali yangu sikivu, iweke mkakati maalum wa kunusuru milima hii ya Uluguru ili hali yake ya uoto, kijani na utiririshaji wa maji (mito) irudie kama ilivyokuwa miaka ya 80. Serikali kuu kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa naamini inawezekana kurudisha hali ya milima ya Uluguru ilivyokuwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uharibifu wa mazingira unaotokana na uchimbaji wa madini na mchanga. Nashauri sheria ndogo katika Halmashauri husika na Sheria ya Mazingira zisimamiwe na kufuatwa, wananchi waendelee kupewa elimu tosha kuhusu utunzaji wa mazingira, wananchi wa pande zote za nchi Bara na Visiwani (Tanzania) wapewe elimu ya faida za mazingira ili kudumisha Muungano wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.