Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, uongozi kwenye Wizara za Muungano; pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano kujaribu kutatua kero za Muungano lakini bado kumeibuka kero nyingine ya kuwabagua Wazanzibari kwenye nafasi za uongozi ndani ya Wizara za Muungano. Sasa hivi zipo Wizara za Muungano kama vile ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Wizara ya Fedha zote zinaongozwa na upande mmoja wa Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwekezaji mashirika ya Muungano; kero nyingine ya Muungano inatokana na Mashirika yanayowekeza Tanzania yanafanya uwekezaji wake Tanzania Bara pekee. Natolea mfano wa Shirika la AICC ambalo limefanya uwekezaji mkubwa Tanzania Bara na bado katika mipango yake ya baadaye haijaonyesha nia ya kufanya uwekezaji upande wa Zanzibar. Ikumbukwe kwamba mbali na pato la Serikali linalotokana na uwekezaji wa mashirika pia umekua ukitoa ajira na kunyanyua uchumi wa wananchi katika maeneo husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kero za wafanyabiashara wa Zanzibar; ni muda mrefu sasa wafanyabiashara kutoka Zanzibar wamekuwa wakilalamika TRA kuendelea na tabia yao ya kuwatoza wafanyabiashara wa Zanzibar kodi mara mbili pale wanapotoa bidhaa zao kutoka Zanzibar kuingia Tanzania bara. Tabia hii ni sawa na kupunguza harakati za wafanyabaiashara wa Zanzibar kuingiza bidhaa zao Tanzania bara na kudhoofisha uchumi wa Wazanzibari. Naomba Wizara husika ifanye ufumbuzi wa haraka wa suala hili kwa faida ya pande zote za Muungano. Naomba kuwasilisha.