Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SABREEN H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
Kumekuwa na kero kubwa kuhusu ushuru wa vifaa vinavyopita bandarini hapa Dar es Salaam na bandari ya Zanzibar hali inayopelekea uwepo wa bandari bubu hasa Ukanda wa Pwani. Je, ni lini Serikali itaondoa hizi kodi za kero kwa wasafiri wa kawaida kabisa ambao si wafanyabiashara wanaotumia bandari hizi mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na kero ya mifereji mikubwa hasa maeneo ya mijini kujaa taka hususan wakati wa mvua hali ambayo inahatarisha maisha ya Watanzania. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzuia taka hizi ili zisilete magonjwa ya milipuko hasa maeneo ya mijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kumekuwa na kero kubwa ya ukosefu wa maji hasa maeneo ya mwambao wa Ziwa Tanganyika kwa mfano uwepo wa Kambi kama Bulombola na maeneo mengine Mkoani Kigoma. Ukosefu wa maji kwenye kambi hizo unapelekea uchafuzi wa maji kwa kuwa vijana wengi kwenye kambi hizo wanategemea Ziwa Tanganyika kwa shughuli za kuoga, kufua na kujisafisha. Je, ni lini Serikali itazuia uchafuzi huu wa mazingira.