Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Waziri wa Mazingira na Muungano pamoja na timu kwa hotuba yake nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuishauri Serikali yangu Tukufu kuhusu suala la mazingira. Kumekuwa na mabadiliko ya tabianchi kutokana na uharibifu wa mazingira hasa kwa wananchi ambao hawajui suala zima la utunzaji wa mazingira. Niishauri Serikali yangu Tukufu ije na mkakati wa kupanda miti, hasa yale maeneo ambayo misitu imechomwa moto pamoja na vyombo vyote vya maji vipandwe miti na viwe na usimamizi mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuwe na sheria maalum ya kupanda miti katika kila kaya, kijiji hadi kata na kuanzia Wenyeviti wa Vitongoji, Wenyeviti wa Vijiji wapewe sheria hizo ili wazisimamie kikamilifu. Naamini tukifanya hivyo tutakuwa tumeboresha nchi yetu kwa kurudisha uoto wa asili uliokuwepo hapo zamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo wananchi wapewe miche ya miti bure. Kwa hiyo, Serikali itenge mafungu kwa ajili ya kununua miti na kuwapa wananchi. Kwa mfano, katika jimbo langu la Lushoto wananchi wangu wapo tayari kupanda miti kwa wingi, shida ni uwezeshaji wa miche.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.