Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utahudu viwanda na biashara na mazingira.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viwanda; Mkoa wa Mara ni Mkoa ambao ulikuwa na Viwanda vikubwa, lakini sasa hivi vimekufa na viwanda hivyo ni MUTEX. Hiki Kiwanda cha MUTEX kimepoteza ajira nyingi sana za wananchi hasa kwa vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya Taifa hili. Ni vizuri Serikali ikajipanga tena upya kufufua kiwanda hiki. Vile vile ningependa kuishauri Serikali kutoa kipaumbele kwa kufungua mnada wa Tarime mpakani, hii itasaidia kutoa ajira kwa vijana na kuepukana na vitendo viovu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mazingira; kutokana na tabianchi hii inayotokana na Mkoa wa Mara kuwa na wafugaji na upatikanaji wa chakula na maji ya mifugo hiyo na kuhamahama kwa mifugo (wanyama) na wingi wa mifugo hiyo wanakandamiza sana ardhi na kusababisha maji kutokupenya ardhini na kusababisha mafuriko na kutuama kwa maji ambayo yanapelekea mazalia ya mbu na kuleta kipindupindu na madhara mengine kwa binadamu na hata kwa mifugo yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, maoni yangu, hii ni sekta ambayo Serikali izingatie na kuipa kipaumbele.