Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mbaraka Salim Bawazir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MBARAK S. BAWAZIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, NEMC wanachelewesha sana utoaji wa taarifa na kuruhusu ujenzi uendelee, Tanzania ya Viwanda haitaweza kupatikana kwa uratatibu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za vibali kwa mtu anayetaka kujenga kituo cha mafuta ni kubwa sana na hapo hapo mteja anatakiwa amchukue mtaalam kwa gharama zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Viwanda vya Plastic kama vinafungwa vifungwe na kama wanatoa muda watoe kwa wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusimamisha uletaji wa mkaa mjini wakati utaratibu wa matumizi ya gesi kwa kupikia hayajakaa vizuri. Elimu itolewe kwa wananchi madhara ya ukataji wa miti na watumie nishati mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.