Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ALLY M. KESSY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza Waziri Mheshimiwa January Makamba, binafsi kwa ziara yake katika Jimbo langu la Nkasi Kaskazini na kusaidia sana kuelimisha wananchi na baadhi ya Madiwani ambao wanajali maslahi yao ili wananchi wazidi kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na Msitu wa Fili ili tuwe na shida ya maji Namanyere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu, nataka kujua mpango wa kupunguza utoaji wa maji katika Ziwa Tanganyika umefikia wapi na lini utakamilika wa Nchi za Burundi, Zambia, DRC – Congo na Tanzania. Umefikia kurudisha kibanio katika Mto Lukuga uliopo DRC – Congo ili maji yasizidi kwisha ziwani na kuhatarisha viumbe hai. Kwa sasa ziwa linapungua sana tena sana kuanzia 1960 mpaka sasa ziwa limepungua zaidi ya mita tatu za maji alama ziko sehemu ya mawe yaliyokuwa karibu na ziwa.