Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. OMAR A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa January Makamba kwa hotuba yake nzuri ya Mazingira na Muungano,
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kwa ufupi sana katika suala zima la mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mazingira bado wananchi wanalichukulia kama ni option na sio lazima. Hili linatokana na kutosimamiwa vizuri sheria zake. Naiomba Serikali izingatie kusimamia na kuelimisha watu kuhusu mazingira. Bado elimu inahitajika. Mfano; kuna Sheria ya Kutotiririsha maji machafu kutoka viwandani, lakini mpaka sasa kuna viwanda vingi tu ambavyo vinatiririsha hayo maji bila hata kuyachuja. Hii inaonesha ni jinsi gani sheria bado haisimamiwi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna sheria ya kutokukata miti lakini bado maeneo makubwa nishati inayotumika kwenye kupikia ni mkaa, hakujasisitizwa wale wote wanaozalisha mkaa wawe na vitalu vya miti ili tukamilishe ile panda miti, kata mti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa, napenda kuisisitiza Serikali kuwa, kuna wale watu wanaozalisha miti mbalimbali, iwawezeshe wanapohitaji msaada kwani wao ndio watunzaji wazuri wa species za miti mbalimbali.